ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 27, 2018

MATUKIO KATIKA PICHA 'NI REAL MADRID MABINGWA TENA UEFA 2018'

Uso kwa uso msindi ni mmoja tu. 
 Kikosi  cha Real Madrid leo kilikuwa; Navas, Carvajal/Nacho, Varane, Sergio Ramos, Marcelo, Modric, Casemiro, Kroos, Isco/Bal, Benzema/Asensio nA Ronaldo
 Liverpool starting XI: Karius, Alexander-Arnold, Lovren, Van Dijk, Robertson, Milner/Can, Henderson, Wijnaldum, Salah/Lallana, Firmino ma Mane.
 Fainali UEFA Champions League 2018
 Kiev 2018
Marcelo v Salah 
Kabla ya kutolewa kutokana na rafu mbaya aliyochezewa na Ramos, Mo Salah alikuwa mwiba dimbani 
 Mashabiki Liverpool
Mashabiki Real Madrid 
Liverpool ilipata pigo mapema tu katika mchezo wa leo, baada ya mshambuliaji wake nyota, Mmisri Mohammed Salah kutolewa nje dakika ya 30 kufuatia kuumia baada ya kugongana na beki na Nahodha wa Real Madrid, Sergio Ramos. 
Hawezi endelea tena na mchezo. 
 Hakuna jinsi.
 Kipa Karius akawazawadia bao la kuongoza Real Madrid baada ya Karim Benzema kumpiga mpira bila uangalifu mbele ya Mfaransa huyo ukamgonga na kuingia nyavuni dakika ya 51. 

Mshambuliaji Msenegali, Sadio Mane akaisawazishia Liverpool dakika nne baadaye, kabla ya Gareth Bale kutokea benchi na kufunga mabao mawili dakika za 64 na 83. 
 Ni goli.
 Farao.

  Karius aliwasili Liverpool akitokea Mainz mwaka 2016 na alikuwa na mwanzo mgumu kabla ya kuzinduka na kuwa kipa chaguo la kwanza mbele ya kocha Jurgen Klopp akimpindua kipa Simon Mignolet. Lakini makosa ya leo ya Karius hayatasahaulika milele. 
  Karius amechangia anguko la Liverpool.
 Benzema akisherehekea.
 Tick tak.
 Goal.....
 It is......
TIMU ya Real Madrid imefanikiwa kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya tatu mfululizo baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Liverpool usiku wa Jumamosi Uwanja wa Olimpiki mjini Kiev, Ukraine. 
PICHA/AFP

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.