ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 22, 2018

KASESELA, ASIA JUMA WATINGA KARIAKOO DAR ES SALAAM, LEO, KUPATA UZOEFU WA NAMNA BORA YA KUSIMAMIA VEMA MACHINGA

 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera akisalimia wananchi baada ya kutambulishwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema (watatu kushoto) alipowapeleka Kasesera na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Juma Abdallah katika eneo la biashara za Machinga katika Mtaa wa Kongo, Kariakoo jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kupata uzoefu wa namna Wilaya ya Ilala ilivyofanikiwa katika kuboresha mazingira na kuwaweka pamoja machinga hao katika shughuli zao. Wapili kushoto ni Katibu Tawala wa Ilala Edward Mpogolo.
 Baadhi ya kinamama wakimweleza kero Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema alipokuwa na ugeni huo.
 Kasesera akiwa na Mwenyekiti wa Machinga wa kariakoo katika ziara hiyo
 Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesera akitazama bidhaa za machinga ambazo alisema hadhi ya bidhaa hizo inaonekana ni zaidi na za machinga
 Kasesera akitazama sampuli ya baadhi ya vifaa vya jikoni vinavyofanya kazi ambavyo anauza Machinga.
 Machinga ambaye ni mtaalamu wa programu za kompyuta namoyo Yusuf, akimpa maelezo Kasesera ya namna ambavyo Umoja wa Machinga unavyohifadhi kumbukumbu zote za machinga katika komyupta. Kulia ni Mbunge wa Kilolo Asia Juma akifuatilia kwa karibu
 Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Juma akimweleza jambo Ofisa katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya walipokuwa kwenye ofisi hiyo ya Machinga Kariakoo
 Kasesera na ujumbe wake wakitoka katika Ofisi ya Machinga
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera na Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Juma wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Machinga wakati wa ziara hiyo
 Kasesera akimfurahia Ustadhi ambaye ni mmoja wa machinga Kariakoo
 Kasesera akifurahia jezi la Timu ya Machinga baada ya kuzawadiwa katika ziara hiyo 
 Kasesera na Amina wakichagua nguo kwenye vitalu vya biashara za Machinga wakati wa ziara hiyo
 Kasesera akilipa fedha baada ya kuchagua nguo alizopenda. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.