ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 18, 2017

LEMA NIKO TAYARI KUUZA FIGO KUMTIBIA LISSU.

Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema amesema hata kama gharama za  matibabu ya Tundu Lissu yakifika Trilioni  moja, watakuwa tayari kuuza figo zao.

Akizungumza leo  Novemba 18 katika kata ya Siuyu iliyopo Wilaya ya Ikungi mkoani Singida Lema amesema utekelezaji wa  majukumu ya kisiasa ukiwa upinzani wakati huu ni ngumu kutokana na kuwindwa kila uchao.

Amesema  pamoja na ugumu huo hawajarudi nyuma na kisasi cha wasiopenda mabadiliko na wanaochukia kukosolewa   kimedhihirika  kwa vitendo alivyotendewa Lissu.

"Lissu yupo kitandani risasi mwili mzima, gharama za matibabu yake ni kubwa, lakini hata ikifika trilioni moja na tukawa hatuna fedha tutauza figo zetu kuendelea kugharamia matibabu yake" amesema Lema.

Amesema Lissu amekuwa alama ya haki katika taifa kutokana na kuamua kuwa upande wa haki

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMPA MRAJISI SIKU 7 ZA KWANINI MAGUNIA KUTOFIKA KWA WAKATI


Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji na kata ya Chiungutwa, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara mara baada ya kushiriki mnada wa tano wa Korosho, Jana Novemba 17, 2017. Picha na Mathias Canal
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe Gelasius Gasper Byakanwa akimuonyesha Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa jinsi magunia yalivyopangwa kwa ustadi ktika gala la kuhifadhia Korosho la Mtanda mara baada ya  Mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji na kata ya Chiungutwa, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara mara baada ya kushiriki mnada wa tano wa Korosho, Jana Novemba 17, 2017.
Badhi ya wakulima wa zao la korosho wa Chama cha Ushirika cha Masasi-Mtwara Cooperative Union Ltd (MAMCU) wakifatilia mnada wa tano wa korosho katika kijiji na kata ya Chiungutwa, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara. Jana Novemba 17, 2017.
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe Gelasius Gasper Byakanwa wakiwasili Kijijini Chiungutwa, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara kwa ajili ya kujionea Mnada wa Korosho unavyoendeshwa, Jana Novemba 17, 2017.
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa (Wa Tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wazee maarufu wa kijiji cha Chiungutwa, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara, Wengine ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe Gelasius Gasper Byakanwa (Wa Kwanza Kushoto), na Mbunge wa Jimbo la Mtwara Vijijini Mhe Hawa Ghasia (Wa Kwanza Kulia).
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe Gelasius Gasper Byakanwa wakati wa Mnada wa tano wa Korosho, Jana Novemba 17, 2017.
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akiwa na Mbunge wa Jimbo la Mtwara Vijijini Mhe Hawa Ghasia wakati wa ukaguzi wa ghala la Buko Kijijini Chiungutwa, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara  wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Humo, Jana Novemba 17, 2017
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisikiliza ushauri sambamba na pongezi kwa kushiriki Mnada wa tano wa Korosho Kijijini Chiungutwa, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara  wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Humo, Jana Novemba 17, 2017
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe Gelasius Gasper Byakanwa wakikagua magunia ambayo tayari yamewasili katika Ofisi ya Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya Chama Kikuu cha ushirika mara baada ya kumalizika kwa mnada wa tano wa Korosho Kijijini Chiungutwa, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara.

Na Mathias Canal, Mtwara

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Machuche Mwanjelwa leo Novemba 18, 2017 amemuagiza Mrajisi wa vyama vya ushirika kukamilisha haraka kazi ya uchunguzi kwenye Bodi za vyama vya ushirika vya Mkoa wa Mtwara ili kubaini sababu zilizopelekea kuuzwa kwa magunia kiholela.

Alisema kuwa kumalizika kwa uchunguzi huo kutarahisisha kuchukuliwa haraka hatua kali za kisheri kwa wale wote watakaobainika kukiuka sheria No 17 ya vyama vya ushirika.

Naibu waziri alitoa agizo hilo wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji na kata ya Chiungutwa, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara mara baada ya kugundua kuwa kuna viashiria vya ukiukwaji wa taratibu katika upatikanaji wa magunia ya kuhifadhia korosho wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani humo.

Sambamba na hilo Naibu waziri Mhe Mwanjelwa wakati wote wa mkutano huo ameshuhudia malalamiko kutoka kwa wakulima wa zao la korosho wa Chama cha Ushirika cha Masasi-Mtwara Cooperative Union Ltd (MAMCU) kuhusu ucheleweshwaji wa upatikanaji wa maguni kutoka kwa mzabui, Mapungufu ya kilo kati ya PDA na WHRs ghala kuu, ikiwa ni pamoja na kuchelewa kwa malipo ya wakulima kwa njia ya benki kutoka kwa wanunuzi.

Katika ziara yake hiyo kilio cha wananchi wengi na wakulima walisiitiza zaidi kuhusu kukosekana kwa magunia hayo huku wakieleza kuwa wakati mwingine kuchelea kufika ama kutowafikia kabisa jambo ambalo linachangia kupunguza thamani ya zao la korosho.

“Nataka Mrajisi ufanye na ukamilishe kazi yako ya uchunguzi na baada ya kuipata taarifa hiyo hatua stahiki zitachukuliwa kwa wale wote watakaogundulika kukiuka sheria ya nchi” Amekaririwa Naibu Waziri Mhe Mwanjelwa

Mbali na agizo hilo Naibu Waziri pamoja na wabunge wa Mkoa wa Mtwara walipata nafasi ya kujionea mnada wa tano wa ununuzi wa korosho unavyoendelea.

Hata hivyo Mnada wa tano ulishuhudiwa Kilogramu 7,524,104 za korosho zikiuzwa kwa thamani ya zaidi ya Bilioni 30.

Wakati huo huo Naibu Waziri Mhe Mwanjelwa amesema Wizara itayafanyia kazi haraka mapendekezo ya tume iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe Gelasius Gasper Byakanwa kufanya uchunguzi kuhusu mwenendo mzima wa magunia pamoja na upatikanaji wake.

Friday, November 17, 2017

TAASISI YA DORIS MOLLEL YAZINDUA FILAMU YA MTOTO "NJITI" JIJINI DAR

Mgeni Rasmi katika hafla ya uzinduzi wa filamu fupi ya "Njiti", Waziri wa Madini, Angella Kairuki (katikati) akiwa na Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jaseem Al Najem (kulia) pamoja na Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel (DMF) na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati "Njiti", Doris Mollel baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi huo, uliofanyika katika ukumbi wa sinema wa Cinemax, Dar Free Market, jijini Dar es salaam leo. Filamu hiyo ambayo inaelezea maisha ya Mtoto aliyezaliwa kabla ya wakati "Njiti" imeandaliwa na Taasisi ya Doris Mollel, imelenga kutoa elimu ya uelewa wa namna ya malezi bora kwa mtoto anayezaliwa kabla ya wakati.
Mgeni Rasmi katika hafla ya uzinduzi wa filamu fupi ya "Njiti", Waziri wa Madini, Angella Kairuki akitoa hotuba yake, ambapo alitoa pongezi nyingi kwa Taasisi ya Doris Mollel kwa kufanikisha kupatikana kwa elimu ya uelewa wa namna ya malezi bora kwa mtoto anayezaliwa kabla ya wakati kupitia filamu hiyo.
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jaseem Al Najem akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa filamu fupi ya "Njiti", ambayo inaelezea maisha ya Mtoto aliyezaliwa kabla ya wakati "Njiti" iliyoandaliwa na Taasisi ya Doris Mollel, imelenga kutoa elimu ya uelewa wa namna ya malezi bora kwa mtoto anayezaliwa kabla ya wakati.
Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel (DMF) na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati "Njiti", Doris Mollel akizungumza katika hafla hiyo, iliyofanyika katika ukumbi wa sinema wa Cinemax, Dar Free Market, jijini Dar es salaam leo. 
Sehemu ya wageni waliohudhulia hafla hiyo.

HATMA YA UKUAJI WA SEKTA YA VIWANDA NCHINI IKO MIKONONI MWA VIJANA.



Vijana wengi wanatumia muda mwingi kukaa vijiweni kupiga stori za kuunga unga na kusahau majukumu yao ya msingi hali inayowarudisha nyuma katika maandeleo yao na nchi kwa ujumla.

Lakini kama wakizichangamkia fursa zilizopo ikiwa ni pamoja na mafunzo ya ufundi yanayotolewa kila kukicha na taasisi mbalimbali za serikali na za mashirika binafsi, kuna mapinduzi makubwa yanakuja katika sekta hususani ya viwanda.

Shuhudia kile kilichofanyika hivi karibuni chuo cha DIT (Dar es salaam Institute of Technology) tawi la Mwanza.

WATU 3 WAUAWA, POLISI KENYA WAKIZUIA MSAFARA WA KUMPOKEA RAILA ODINGA UWANJA WA JOMO KENYATTA AKITOKEA NJE YA NCHII.


Polisi wa Kenya wakifyatua risasi dhidi ya wapinzani wa serikali;

 

Gladys Wanga amewapa ruksa polisi kumfyatulia risasi, iwe isiwe atasonga kuingia uwanjani kumpokea Raila.

Jeshi Kenya laua waandamanaji watatu, magari kadhaa yachomwa, Raila arejea nchini

Watu watatu wameuawa hii leo wakati jeshi la polisi la Kenya lilipojaribu kutawanya waandamanaji waliokusanyika kupokea msafara wa kiongozi wa upinzani, Raila Odinga aliyerejea nchini mapema leo akitokea nje ya nchi.


Polisi ya Kenya imetumia gesi ya kutoa machozi na kufyatua risasi angani dhidi ya wafuasi wa Odinga waliokuwa katika barabara inayotoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta wakielekea mjini kati jijini Nairobi.


Waandamanaji wawili wameuawa katika mapigano yaliyotokea baina yao na polisi waliokuwa wakitaka kuzua waandamanaji hao kuingia katika maeneo ya kibiashara mjini Nairobi. 

Ripo zinasema magari kadhaa yameteketezwa kwa moto katika ghasia na machafuko hayo.

TANZIA: ALIYEKUWA KATIBU MKUU (CWT) AFARIKI DUNIA.



Dar es Salaam. Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Yahya Msulwa amefariki dunia jana katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.
Katibu mkuu wa zamani wa chama hicho, Gratian Mkoba ameithibitisha Mwananchi leo Ijumaa Novemba 17 wakati akizungumza kwa simu.

Mkoba amesema, “Ni kweli amefariki jana usiku na alipelekwa jana hiyo usiku kwa mujibu wa ndugu zake walionipa taarifa, maana mimi nilikuwa nina wiki moja hatujawasiliana na sijui alikuwa na anasumbuliwa na nini,”amesema Mkoba.

Amesema hivi sasa yupo njiani kwenda nyumbani kwa marehemu Tuangoma kujua taratibu za mazishi.

Thursday, November 16, 2017

MKUU WA MKOA WA MWANZA AKAGUA UTEKELEZWAJI AHADI ZA MELI ZA MAGUFULI KWA USAFIRI KANDA YA ZIWA NA NCHI JIRANI


Ili kuondokana na adha ya usafiri, Serikali imeanza ukarabati wa Meli ya Mv. Clarius iliokuwa imesitisha huduma za usafirishaji wa abiria na mizigo kwa zaidi ya miaka 10 bila kutoa huduma hiyo kwa wananchi wa Wilaya ya ukerewe mkoani Mwanza wanaozungukwa na ziwa Victoria. 

Akizungumza mara baada ya kukagua meli hiyo na nyingine zilizopo katika bandari ya Mwanza kusini, Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella, amesema kukamilika kwa ukarabati wa meli hiyo na nyingine zilizopo katika mpango wa ukarabati utasaidia kwa kiasi kikubwa kukuwa kwa uchumi .

MUGABE ANG'ANG'ANIA MADARAKA, AU NA UN ZATOA KAULI.

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ambaye yuko katika ncha ya kuuzuliwa amekataa kuachia madaraka akisisitiza kuwa yeye ndiye kiongozi halali wa nchi hiyo.

Duru za habari zimeliambia shirika la habari la Reuters kuwa, Mugabe amekataa upatanishi wa Askofu wa Kanisa Katoliki nchini humo Fidelis Mukonori, ambaye alikuwa anaongoza mazungumzo kati ya rais huyo mkongwe mwenye umri wa miaka 93 na makamanda wa jeshi la nchi hiyo.

Jeshi hilo jana lilitangaza kuwa Mugabe na familia yake wako kwenye kizuizi cha nyumbani na kuongeza kuwa litawapandisha kizimbani wale liliowataja kama "wahalifu" waliomzunguka kiongozi huyo ambao wameisababishia nchi hiyo madhara na hasara za kiuchumi na kijamii.

BREAKING NEWS: WATU WA 3 WAMEKUFA MAJI NA WENGINE 15 WAKIOKOLEWA BAADA YA MELI KUZAMA ZIWA VICTORIA

Watu 3 wamepoteza maisha na wengine 15 wakinusurika baada ya Meli ya Mv Julius kuzama ndani ya ziwa Victoria.

Meli hiyo inayo fanya safari zake Mwanza - Gozba imezama usiku wa kuamkia leo ambapo ilitarajiwa kuingia leo saa 12 asubuhi nazo taarifa za awali zinasema kuwa Chanzo cha ajali hiyo ni meli hiyo ni kutokea hitilafu kwenye injini yake sanjari na meli hiyo kuzidisha mzigo.

Zaidi ya magunia 500 ya dagaa yamezama na meli hiyo umbali wa kilometa 4 kutoka bandari ya Gozba.

Mwandishi wetu Zephania Mandia anafunguka kilichotokea kupitia kipindicha KAZI NA NGOMA kinachorushwa na Jembe Fm Mwanza (BOFYA PLAY KUSIKILIZA)... aa

Wednesday, November 15, 2017

ZAINA FOUNDATION HELP WOMEN TO ICREASE KNOWLEDGE IN CYBER SECURITY

Zaituni explained about password manager and how it can helps to secure  password, and reuse one password for many accounts and how to create strong password.
Zaituni facilitated about Mobile Safety:  She explained mobile rules and advantages and disadvantages of using smart phone and dump phone.
Some of Participants during reflection about day one before we started day 2 agenda.
Group photo with some participants with banners of different agenda of our workshop.


Recently Zaina Foundation hosted two days training about Digital Security for Women’s in Arusha Tanzania with great support from Internews,Defend Defenders from Kampala Uganda and trainers Mr. Paschal Masalu Founder us Elimika Wikiendi and Badru Juma from YUNA Tanzania. . The objective of workshop where to empower women’s and girls to be aware and get knowledge about digital security skills 

In that training twenty (20) participants and Zaituni safe sister fellow in East Africa was a facilitator, stay together and learn several topic about digital security skills and practiced all skills acquired by using their devices also participant learn and practiced new tools like Signal Mobile app in their phone. 

Online Safety was one of the topic covered during the workshop, in this participant learn about hackers who, how and why people get hacked in online this was important because women are at high risk when they are online compared to men, so they get knowledge on password and password manager which will help them to stay safe online.

Also due to the fact that we are in digital world, most of people are using Internet and especially in social media like Facebook, Twitter and instagram which are common to everyone due to this participant trained how to secure their accounts and teach them ten rules of social media and how to use social media in a positive way.

They also get knowledge about two factor authentication which help users to know someone who try to inter/log to your account, Computer hygiene securing computer with antivirus and how to be protected while we are in internet, Mobile Safety this was important because most of internet users they use through their mobile devices.

Other topic where topics were encryptions, full disk encryption, vera crypt and mail velop this was important because they wanted to make sure participants have end to end encryption in their communication in email and chats.

Lastly participants were introduced about cyber law in Tanzania and how to avoid cyber bulling; the law was signed since 2015 and from the workshop it help participants to be more aware about cyber security and they are more safe

WASEMAVYO JEMBE DJYz KUELEKEA 'KIK OF PARTY 2017' CHINI YA KINYWAJI MARIDHAWA 'JACK DANIELS'

 DJ K-FLIP
 DJ MIKE BEATZ
 CHRISS THE DJ
 DJ SCORPION
 DJ JACKO
With Live perfomance kutoka WCB's. @Rayvanny.
Ni Muda wetu huu jicho kwa jicho na Party la Kijanja na La mvuto wake Ndani ya Rock City
MCHONGO Uko Hivi Tarehe 25 Nov 2017 mahali @theCaskbar&Grill

Jackdaniels Holiday Season ONe KICK OFF PARTY Kwa Mara ya Kwanza ndani Ya Mwanza...With Live perfomance kutoka WCB's. @Rayvanny na Ma-Suprizes kibaao kutoka @jembenijembe @jembefm
Huku kwenye Wheels of steels kundi bora la Djz kutoka @Jembefm JEMBEDJZ watakata Kiu ya Burudani Unakosaje sasa?? Mlangoni utaacha 10k powered by @vodacomTanzania @Coca_Cola @jembenijembe #jackDaniels ....
Get your ticket now..
 Sikiliza 93.7 @Jembefm kwa Ma infozz.. zaidi wapi unaweza pata ticket yako... @wcb_wasafi @gsengoTv #wcb #Mwanza

ALIYEKUWA MAKAMU WA RAIS WA ZIMBABWE ATANGAZWA KUWA RAIS WA MPITO.



Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Zimbabwe Emerson Mnangagwa atangazwa kuwa Rais mpya wa chama cha ZANU -PF.
Akaunti ya chama cha Zanu PF inasemama kuwa Emmerson Mnangagwa amefanywa kuwa rais wa mpito.

 
Mnangawa mwenye umri wa miaka 75 alifutwa kama makamu wa rais kutokana na kile serikali ilisema kuwa kutokuwa mtiifu.
Kufutwa kwake kulionekana kama nia ya kumwezesha mke wa Rais Mugabe, Grace, kufuata nyayo za mumewe na kuwa kiongozi wa Zimbabwe.

Awali alikuwa ametoa wito kwa mumewe kumfuta makamu wa rais.

Bw. Mnangagwa ambaye ni mkuu wa zamani wa ujasusi amekuwa mtu ambaye alitarajiwa kumrithi Rais Mugabe 93.

Kufutwa kwake kulimaanisha kuwa Grace Mugabe anatarajiwa kuteuliwa kuwa makamu wa rais wakati wa mkutano maalum wa chama tawala cha Zanu-PF mwezi ujao.

ZAIDI YA MADAKTARI 300 KUWEKA NANGA NCHINI KWAAJILI YA KUTOA TIBA BURE DAR ES SALAAM



NIMEANDIKA HATA KWENYE UKURASA WANGU WA INSTAGRAM

Kipekee nilipo pata bango la tangazo kwa wananchi wakazi wa Dar es salaam kujitokeza kupima afya kwaajili ya zoezi lijalo la afya nilipuuza, na kukejeli kwa hali ya Juu hatua hiyo, mmh....

Lakini sasa, kadri siku zinavyosonga ule mpango mkakati nashuhudia mbona unasonga na nuru kali inaangaza kunionyesha mbele kulivyo...?!!?. . 

Daaaaah kweli #Wagenga walisema "usikatae wito, kataa...... " 

TAARIFA za ujio wa ugeni wa meli yenye hospitali na madaktari zaidi ya 300 kutoka China nao watatoa tiba kwa wananchi wote waliopima na kugundulika kuwa na matatizo iwe yale sugu, makubwa hadi madogo. .

Big up RC @paulmakonda . CC:-@jembenijembe @gijegije @gsengoTv @jacquelineshuma @prince_nzwalla @mackjumanne @deejaykflip #mchakamchaka

NIGERIAN ARTISTE SKALES RELEASES AGOLO & BOOTY LANGUAGE/ANNOUNCES PLANS FOR EAST AFRICA


Top Nigerian afro beats artiste, Skales, known for delivering mega hits like “Temper” and "Shake Body", some of the biggest Nigerian tunes to hit East Africa, is now taking on an East African approach from now on, into 2018. Skales releases two smash hit singles AGOLO and BOOTY LANGUAGE featuring Ghanaian rapper Sarkodie in East Africa, as he plans to launch new singles featuring artists from East Africa.

Speaking on his East Side plan Skales says: “I have decided to spread my brand strategically to East Africa because of the love and attention I get from my fans from East Africa. They have made my songs massive in the region,” adding, “Music is also a universal language and the East African sound and culture continues to inspire my music in a lot of ways.”

AGOLO and BOOTY LANGUAGE are off Skales sophomore album ‘The Never Say Never Guy” and have dominated music airplay across Africa since the album dropped earlier on this year. Skales who tags his album as a masterpiece says, “I believe that East African sounds influenced a huge percentage of my album. This is part of the reason why I am setting aside time to venture into East Africa.”

The Chopstix produced AGOLO is a certified afro pop hit with a perfect blend of Yoruba traditional sounds. The single has already sparked traditional dance steps among fans, just like in the video showcasing the streets of Ojota in Lagos, directed by Lucas Reid. In BOOTY LANGUAGESkales delivers smooth rap bars in a steady flow while appreciating the voluptuous curves of the African woman. Skales described the video boasting an urban setting with colorful graffiti displayed in the background director by Teekay as one of his favorites in recent times - asserting its creativity as incredibly commendable.


Cindy Sanyu, Navio, Nyashinski, Avril, Vanessa Mdee and Joh Makini are among artistes from East Africa Skales is currently feeling. He says: “I’m a huge fan of a lot of East African artistes and through my work with them, I hope to unify the African music culture.” Skales promises that he will be coming to East Africa soon. He concludes: I would like my East African fans to know that I got love for you and I appreciate all the support you have shown me and music this far. There is no other continent that is as blessed as we are so let’s believe more in us and empower us.”

With over 200 songs recorded so far with high-flying collaboration with several top acts including Burna Boy, Sarkodie, Eldee, Jeremiah Gyang, Banky W and Knighthouse, Skales continues to enjoy massive success beyond the African music scene. He recently got featured on Major Lazer’s RUN UP – Afrosmash Remix featuring PartyNextDoor, Yung L, Chopstix and Nicki Minaj.

EDITORS’ NOTES

Skales is a songwriter and performing artiste who propelled to fame following the Pan African success of his hit singles: “Temper”, "Shake Body", "Mukulu", "Keresimesi" and "Komole”. Other monumental singles include his 2009 debut single, "Must Shine" and “Heading for a Grammy” that was inspired by Kanye West’s “Jesus Walks”. Skales has performed in the US, UK, Ethiopia, Seychelles, Canada and Uganda. He is also the first Nigerian artist to Co-headline a major Reggae beach fest in Dubai with Kymani Marley. In 2013 he performed at Felaberation. After departing from Empire Mates Entertainment in May 2014, he established his record label OHK Music. He is also currently signed to Baseline Record Label. In 2015,Skales released his album ‘Man of the Year’. In 2016, his smash hit ‘Temper’ featuring Burna Boy received massive airplay and was featured on a short documentary made by Major Lazer whilst touring in Africa.

FOR MORE

TWITTER: @youngskales
INSTAGRAM: @youngskales
FACEBOOK: @youngskales

To interview Skales on his East African plans and his singles, or to receive more info: kindly request via bookings@anyiko-pr.com.

TUNAWALENGA WAHALIFU SI MUGABE: JESHI LA ZIMBABWE

Jeshi  la Zimbabwe limesoma taarifa kwenye kituo cha runinga cha serikali ZBC, likisema kuwa linachukua hatua ya kuwalenga wahalifu nchini humo.  Hata hivyo, limesema kuwa hayo si mapinduzi ya kijeshi na Rais Mugabe yuko salama.
Milio mikubwa ya risasi ilisikika katika maeneo ya kaskazini mwa mji mkuu Harare mapema jana.  Taarifa hiyo ya jeshi ilikuja saa kadhaa baada ya jeshi kudhibiti kituo cha utangazaji cha  ZBC. Grace Mugabe anaonekana kukaribia kukirithi kiti cha mumewe

Mwanamume mmoja ambaye alikuwa amevaa sare za jeshi alisema kuwa jeshi linataka kukabiliana na watu ambao wanatenda uhalifu unaoleta madhara ya kijamii na kiuchumi nchini Zimbabwe.

“Wakati tutakapomalizia wajibu wetu, tunatarajia kuwa hali itarudi kuwa kama kawaida.”

Taarifa hiyo ilisema kuwa Mugabe,  93, na familia yake wako salama.  Haijulikani ni nani anaongoza hatua hiyo ya kijeshi.  Magari ya wanajeshi waliojihami kwa silaha yalionekana maeneo ya mjini Harare.

Hali hiyo ya wasiwasi wa lolote kuweza kutokea, ilianza  jana jioni, ambapo wanajeshi wakiwa na silaha walionekana wakijipanga katika maeneo kadhaa  na kuzingira ofisi za shirika la utangazaji la Zimbabwe (ZBC).

Hata hivyo, taarifa zinasema kuwa wafanyakazi wa shirika hilo la utangazaji la ZBC, waliambiwa na wanajeshi hao kwamba hawapaswi kuwa na wasiwasi na kwamba uwepo wa vikosi hivyo ni kwa lengo la kulinda eneo hilo.

Chama tawala nchini Zimbabwe kimemtuhumu mkuu wa majeshi Constantino Chiwenga, kwa hatua yake ya madai kuwa jeshi lipo tayari kuingilia mzozo huo wa kisiasa kwa lengo la kulinda wapigania uhuru wa taifa hilo.

Hakuna kauli yoyote iliyotolewa na Rais Robert Mugabe kutokana na hali ya sasa nchini mwake.

Marekani imesema kuwa inafuatilia kwa karibu hali ya Zimbabwe na kutoa rai pande zote kutatua mzozo huo kwa njia ya amani.

Naye Balozi wa Marekani nchini Zimbabwe kupitia ukurasa wake wa Tiwtter amesema kuwa leo watasitisha shughuli za kiofisi ubalozini hapo kutokana na hali ya sasa mjini Harare.

Balozi wa Zimbabwe nchini Afrika Kusini, Isack Moyo, ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa serikali ipo imara katika jambo hilo na kuzuia uwezekano wowote wa kufanyika kwa mapinduzi.

Tuesday, November 14, 2017

BILIONEA MNUNUZI WA NYUMBA ZA LUGUMI AREJEA URAIANI KWA MIKOGO.

Dar es Salaam. 'Bilionea' wa nyumba za Lugumi, Dk Louis Shika ameachiwa na kwenda kupanda daladala kuelekea nyumbani huku akisema mpango wake wa kununua nyumba za Lugumi uko palepale. 
Baada ya kuachiwa na polisi leo Jumanne jioni amesema kwamba bado mpango wake wa kununua nyumba hizo uko palepale. 
Amesema anachosubiri sasa ni fedha kuingizwa kwenye akaunti yake na kulipa asilimia 25 anayodaiwa. "Siku nikipeleka fedha nataka Yono na TRA waite waandishi wa habari waone na wautangazie umma," amesema. 
Amesema vyombo vya habari vimetoa taarifa zake lakini vitaumbuka siku akienda kupeleka fedha hizo.
 Ameendelea kusisitiza kwamba nyumba hizo zinahitajiwa na kampuni yake ambayo hakuitaja. Njiani wakati akielekea kwenye kituo cha daladala cha Mnazi Mmoja, Dk Shika alikuwa kivutio kwa watu aliokuwa akipishana nao.
 Alipopanda daladala la Tabata Mawenzi, kondakta alimkaribisha kwa kumweleza karibu mzee Shika. Kauli hiyo iliwaamsha abiria ambao walikuwa na hamu ya kumwona. Dk Shika alipanda daladala na kusimama huku akionyesha tabasamu lisiloisha.

HAPA NDIPO LULU ANAPO LALA GEREZANI.


Siku ya pili leo inakatika wakati ambapo mwigizaji nyota wa filamu nchini Tanzania Elizabeth Michael 'Lulu' akiwa nyuma ya nondo za gereza la Segerea jijini Dar es salaam, hii ikiwa ni mara baada ya maamuzi wa Mahakama dhidi yake yakimuamuru kutumikia kifungo cha miaka miwili baada ya kukutwa na kosa la kumuua bila kukusudia, aliyekuwa Nguli wa Filamu nchini Steven Kanumba 'The Greatest' 
 
Kanumba alifariki majira ya saa nane usiku,mnamo mwaka 2012 baada ya kutokea mzozo kati yake yake na Elizabeth Michael ambaye inaaminika kuwa walikuwa na uhusiano wa Kimapenzi.


Moja ya maswali kati ya mengi yaliyotawala vichwa vya wengi:-
1. Maafisa magereza walimpokeaje Lulu huko gerezani?
2. Jeh ni kweli kuwa watu maarufu wanapokuwa kifungoni huwa na maeneo yao spesheli yenye full service, Jeh msanii huyo baada ya kutupwa Segerea analala wapi?
3. Mfungwa anapohukumiwa miaka yake kadhaa, Jeh hesabu ya miaka hiyo huwa kwa mtindo upi?
---Jeh Usiku na Mchana huhesabika kama siku mbili au imekaaje?
4. Jeh Lulu ana qualify kupata msamaha wa Rais?

KAZI NA NGOMA ya Jembe Fm chini ya Mwenyekiti Albert G. Sengo naye Katibu Mansour Jumanne inamtafuta Afisa wa jeshi la Magereza ambaye ni Msemaji wa Jeshi hilo Lucas Mboje na kufanya naye mahojiano.

TAKUKURU YATANGAZA DAU LA MILIONI 10 KWA ATAKAYEFANIKISHA KUNASWA KWA FISADI ALIYE TOROKA.

TAKUKURU wanamtafuta Godfrey John Gugai kwa kuwa na maisha na mali yanayozidi kipato chake bila maelezo
Huyu alikuwa mtumishi wa umma TAKAKURU na ameweza kujiptia mali nyingi, mwazoni TAKUKURU walimwita na kumhoji lakini baadae alipoona anakosa maelezo alikuwa anawapiga chenga na kukimbia nchi kupitia njia zisizo rasmi
Mpaka sasa anatafutwa bado hajaapatikana na wametangaza kwa mwananchi yoyote atakayempata atoe taarifa

TAKUKURU watatoa zawadi ya milioni 10 kwa ambaye atafanikiwa kupatikana kwa bwana huyo

Ametaja mali anazomiliki mtu huyo ikiwa ni pamoja na jengo la ghorofa nne lililopo Ununio Kinondoni, Jengo la Kifahari la ghorofa tatu

Ana nyumba za kupangisha Kinondoni, jengo la kifahari lililopo Majita Musoma, Jengo la Kifahari Kiseke Mwanza, Jengo la Kifahari Nyegezi Mwanza

Pia anailiki viwanja maeneo ya Bunju Kinondoni, Kigamboni, Buyuni Temeke, viwanja viwili Kaole Bagamoyo, Kibaha, Kihonda Morogoro, Kiyeheya Morogoro, Lukuvi Morogoro, Kisasa Dodoma, Itege Dodoma, Chidati Ngolo Mwanza, Mgongolo Mwanza, Nyamagana Mwanza, Nyamagana Mwanza, Magarika Mwanza, Makoko Musoma, Gomba Arusha, viwanja 3 Mwambani Tanga, Viwanja 2 Mwakidila tanga, gari aina ya Mitsubishi Canter, Toyota Rav 4,na pikipiki ,

DC KAPUFI"WAFANYABIASHARA WA NYAMA WASIBUGUZIWE NA MTU YOYOTE YULE WAUZE KWA BEI WANAZOTAKA"

(Katikati) ni mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Geita ,Leornad Kiganga Bugomola,akifuatiwa(kulia) na Mkurugenzi wa halmashauri hiyo,Mhandisi Modest Aporinal pamoja na makamu mwenyekiti wa halmashauri hiyo,Costantine Molandi wakati wa kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri hiyo.
Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Geita,Leornad Kiganga Bugomola akielezea tatizo la mfanyabiashara wa nyama ambaye amekuwa akipigwa na wafanyabiashara wenzake.
Baadhi ya madiwani wakiwa kwenye kikao hicho.
Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akisisitiza wafanyabiashara kutokubuguziwa na mtu yoyote kwenye shughuli zao wakati wa kikao hicho cha baraza.
Diwani wa kata ya Kalangalala,Sospeter Mahushi akichangia swala la wafanyabiashara.
Makamu Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Geita pamoja na mkurugenzi wakijadili jambo wakati wa kikao cha baraza la madiwani.
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM)wilaya ya Geita,Barnabas Mhoja Mapande akizungumza na madiwani wakati wa kikao hicho.



Serikali Wilayani Geita imesema kuwa  mfanyabiashara anayehitaji kuwekeza kwenye biashara ya kuuza nyama kwa bei nafuu anaruhusiwa kufanya biashara hiyo sawa na watu wengine bila ya kubughudhiwa na mtu ama kikundi chochote.

Hatua hiyo imekuja kutokana na mfanyabiashara ambaye jina lake halijafahamika mara moja kufungua duka la nyama na kuuza kwa Sh,3500 kwa kilo kuambiwa na umoja wa wamiliki wa maduka ya nyama kuwa afunge kwa kuwa wao wamekuwa wakiuza kwa Sh 6000 kwa  kilo moja.

Amedaiwa kuwa anauza nyama kwa bei ambayo haijazoeleka mjini Geita na kwamba bei hiyo imezoeleka kwenye Kata ya Kasamwa .

Akizungumza wakati wa baraza la madiwani wa halmashauri ya Mji wa Geita,Mwenyekiti wa halmashauri ya hiyo  Bw, Leornad Bugomola alisema kumekuwa na kikundi kinachopanga bei ya nyama mjini humo na hivyo kusababisha kumtoa mwekezaji aliyekuwa akiuza nyama kwa bei ya chini.

“Mkuu wa wilaya kutokana na watu kuhangaika  kufuata nyama Kasamwa sisi tulionelea tumuombe mtu aje afungue Bucha ambayo itakuwa na Bei nafuu hivyo alikubali lakini kimezuka kikundi ambacho kimekuwa kikimpinga muwekezaji huyu na kwamba afunge bucha yake kutokana na wao kutokuafiki bei hiyo ili swala nimeona nikwambie ili uweze kulishughulikia”Alisema Bugomola

Kutokana na maombi hayo mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl  Herman Kapufi alisema katika wilaya anayoiongoza anataka kitu bora na kwamba suala la bei haliwezi kuwafanya watu kutowekeza kwenye wilaya yake na kama kuna watu wengine ambao wanauza bei nafuu ya nyama ni vyema wakapatiwa maeneo ya biashara hiyo kwani hakuna mtu ambaye anaweza kuingilia biashara ya mtu mwingine. 
Baadhi ya wakazi wa mjini Geita wamepongeza uamuzi huo wa serikali kwa kuwa wengi hawana uwezo wa kumudu bei ya nyama ya sasa.