ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 21, 2017

VIJANA WAZALENDO WAUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS MAGUFULI MJINI DODOMA LEO.

Mhe Jordan Rugimbana Mkuu wa mkoa wa Dodoma akikabidhiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM ( UVCCM ) Shaka Hamdu Shaka Taarifa ya  Tamko la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kutokana na kazi nzuri anayoifanya ya kulinda Rasilimali Za Nchi lilifanyia mkoani Dodoma
Kaimu katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi ( UVCCM ) Shaka Hamdu Shaka ( MNEC ) akitoa Tamko la Vijana wazalendo la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kutokana na kazi nzuri anayoifanya ya kulinda Rasilimali Za Nchi(picha na Fahadi Siraji wa UVCCM )
Mhe Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana ajira na Mbunge wa jimbo la Dodoma Mjini Anthony Mavunde akizungumza na Vijana wazalendo  katika
Hafla fupi ya Kukabidhi tamko  la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kutokana na kazi nzuri anayoifanya ya kulinda Rasilimali Za Nchi Mjini dodoma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Lugimbana akizungumza na Vijana wazalendo mara baada ya  kupokea taarifa ya Tamko la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kutokana na kazi nzuri anayoifanya ya kulinda Rasilimali Za Nchi

baadhi ya mabango yakiwa na ujumbe mbalimbali za kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kutokana na kazi nzuri anayoifanya ya kulinda Rasilimali Za Nchi. ( Picha na Fahadi Siraji wa UVCCM )
Vijana wakiwa katika burudani.(picha na Fahadi Siraji wa UVCCM )
Vijana wakiwa katika burudani.(picha na Fahadi Siraji wa UVCCM )

MWALIMU COMMERCIAL BANK, (MCB), YASHIRIKI BONANZA LA MICHEZO LA WALIMU WA MICHEZO DAR



NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
TIMU ya soka ya wafanyakazi wa Mwalimu Commercial Bank,(MCB), plc, imefungwa mabao 3-1 na kikosi mchanganyiko cha walimu wa jijini dar es salaam, katika pambano la kirafiki ikiwa ni sehemu ya mafunzo ya wiki moja ya walimu wa michezo yaliyofanyika chuo kikuu cha dar es salaam.
Pambano hilo lililopigwa kwenye uwanja wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, leo Oktoba 21, 2017, haikuwa kazi rahisi kwa kombaini ya walimu kushinda mchezo huo dhidi ya “mabenker” hao wa MCB, kwani hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, timu zote zilitoka sare ya bao 1-1.
Katika kipindi cha pili tena dakika za lala salama, wafanyakazi wa MCB walielemewa na kujikuta wanatundikwa mabao mawili ya haraka haraka.
Hata hivyo kocha wa MCB, Lufingo Mwakilasa, aliwasifu wachezaji wake kuwa wamejitahidi kucheza vizuri licha ya hali ya hewa kuwa mbaya (joto kali), lakini pia asili ya kazi yao ambayo muda mwingi huwa wanautumia wakiwa maofisini kuhudumia wateja ukilinganisha na wenzao ambao ni walimu wa michezo na muda mwingi huwa wanafanya mazoezi.
Akizungumzia pambano hilo la kirafiki, Mkuu wa Kitengo cha Biashara na Masoko cha benki hiyo, Valence Luteganya alisema, kwa takriban wiki moja walimu hao wa michezo walikuwa wakishiriki semina ya mafunzo chuo kikuu ambayo MCB ilidhamini semina hiyo.
“Mchezo huu ni wakujenga ushirikiano wa karibu na wenzetu walimu, ambao nao ni wateja wetu wakubwa.”alisema Lutenganya.

 Kombania ya walimu wa michezo wa jiji la Dar es Salaam, ambao walimenyana na wafanyakazi wa MCB katika pambano la soka la kirafiki.
Mchezaji wa MCB, (Kulia), akimenyana na mwenzake wa kombania ya Walimu.
Priva Audax wa MCB, akijikunjua kufumua shuti.

 Kocha mkuu wa MCB, Lufingo Mwakilasa
Wachezajiwa MCB (kulia), wakisalimiana na wwenzao wa Kombania ya walimu wa Dar es Salaam tayari kuanza mchezo huo.
 Kipa wa MCB, akiruka kuokoa mpira
 Kipa wa MCB, akipangua mpira
Priva Audax wa MCB










MCHAKATO TAMASHA LA SZIFF WAACHA VUMBI MWANZA.

 Mmoja wa waratibu wa Tuzo za Sinema Zetu 'Kichaka' akizungumza na kipindi cha Kazi na Ngoma ya radio Jembe Fm akifunguka mchakato wa kusaka vipaji ulivyopangwa. 

MCHAKATO WA TAMASHA LA SZIFF WAACHA VUMBI JIJINI MWANZA.
 
 Kikosi kazi cha Sinema Zetu kipo kimekuwa Jijini Mwanza kwa ajili ya kukutana na wadau wa filamu, ambapo kilifungua milango kwa kwa wadau hao wa Jiji la Mwanza kukutana nao siku ya ijumaa katika ukumbiwa CF Mayi Hotel na kujadili nao jinsi ya kuboresha kazi zao kuelekea tuzo za kimataifa za filamu#SZIFF
 Kutoka kushoto ni Mtangazaji wa Kazi na Ngoma G. Sengo akiwa na wadau wa SZIFF Zamaradi na Babu Wambura.
 Kazi kazi na Kikosi Kazi.
 SZIFF wakifanya mahojiano na mtangazaji wa Kazi na Ngoma Mansour Jumanne.
 Karibu tena.....Asante!
Mastori tyme.

HELIKOPTA YAANGUKA NCHINI KENYA.

Nakuru, Kenya. Helikopta imeanguka katika ziwa Nakuru nchini Kenya muda mfupi baada ya kuruka kutoka katika hoteli moja mjini humo.
Gazeti la Nation limemnukuu ofisa wa serikali, Joshua Omukata akithibitisha kutokea kwa ajili hiyo na kusema kulikuwa kukisubiriwa boti ya uokoaji kuelekea katika eneo la tukio.

Taarifa ambazo hata hivyo zilikuwa bado hazijadhibitiwa zilisema helkopta hiyo ilikuwa imebeba watu wanne.

Seneta wa Nakuru, Susan Kihika amesema baadhi ya timu yake inayohusika na masuala ya mawasiliano walikuwemo kwenye helikopta hiyo.

Helkopta hiyo ilikuwa imeruka kutoka Hoteli ya Jarika na baadhi ya duru za habari zinasema ilikuwa ikiruka katika usawa wa chini kabla ya kuanguka.

Ripoti zinasema helkopta hiyo baadaye ilipanga kuwachukua waandishi wa habari kwa ajili ya kampeni za uchaguzi wa marudio utakaofanyika Oktoba 26. Waandishi hao walikuwa kwenye hoteli hiyo wakati ndege hiyo ilipoanguka.

INGAWA MIGOGORO YA ARDHI MIJINI BADO MWIBA LAKINI NITAPAMBANA NAYO:- ASEMA MONGELA



NA ZEPHANIA MANDIA WA G.SENGOBLOG

Migogoro ya ardhi katika sehemu za mijini bado zimekuwa mwiba kwa wananchi wengi kutokana na ongezeko la watu katika sehemu hizo.

Manispaa ya ilemela ni moja ya wilaya zinazokabiliwa na changamoto hiyo,ambapo mara kadhaa mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongela ameingilia kati ili kutatua migogoro hiyo.

Ni mwezi mmoja na siku kadhaa zimepita tangu mkuu wa mkoa wa Mwanza JOHN MONGELA aliposikiliza na kutatua kero za ardhi zilizokuwa zikiwakabili wananchi wa wilaya ya Ilemela na Nyamagana mkoani mwanza.

Mongela akapata  fursa ya  kusikiliza kero za ardhi amabazo bado hazijatatuliwa tangu alipotoa maagizo kwa idara husika.

Mongela ameigeukia  idara ya ardhi na kuitaka kuunga jitihada za mkoa za kutatua migogoro na sio kuwa chanzo cha kuzalisha migogoro mingine.

Baadhi ya wananchi wameonekana kupongeza jitihada zinazo oneshwa na mkuu wa mkoa wa mwanza wa kusikilizana kutatua kero za ardhi ambazo zimekuwa zikiwakabili kwa muda mrefu.

Kikao hiki cha mkuu wa mkoa wa mwanza kimeweza kutatua migogoro kadhaa huku akitoa mwezi mmoja kwa idara ya ardhi ya wilaya ya ilemela pamoja na idara ya ardhi kanda ziwa kumaliza kabisa migogoro iliyosalia.

Friday, October 20, 2017

SUKUMA DANCE NGOMA TOKA USUKUMANI



Furahia muziki wa watu kabila la Sukuma (Wasukuma) toka mkoani Shinyanga ndani ya Maadhimisho ya sikukuu ya mavuno Bulabo yaliyofanyika viwanja vya michezo Kisesa mkoani Mwanza.

Kilinuka balaaa

‘HALMASHAURI ZIMUUNGE MKONO RAIS MAGUFULI KWA KUNUNUA VITANDA VYA KUJIFUNGULIA’, DKT NCHIMBI.

 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akifungua moja kati ya vitanda 14 vya kujifungulia vilivyotolewa na Rais Magufuli mapema leo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida.

Wauguzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida wakifurahia mara baada ya kukabidhiwa vitanda vya kujifungulia vilivyotolewa na Rais Magufuli.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Aisharose Mattembe akizungumza na wauguzi, madaktari na Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) mkoa wa Singida kabla hajakabidhi vitanda 14 alivyopewa na Rais Magufuli ili avifikishe kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Emmanuel Kimario akimshukuru Rais Magufuli kwa kuwapatia vitanda vya kujifungulia ili kupunguza uhaba wa vitanda kwa Mkoa was Singida.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akisaidiana na wataalamu wa afya pamoja na Mbunge wa Viti maalumu Aisharose Mattembe kufunga moja kati ya vitanda 14 vya kujifungulia vilivyotolewa na Rais Magufuli mapema leo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida.

Halmashauri saba za Mkoa wa Singida zimeagizwa kununua vitanda kumi kwa ajili ya akina mama kujifungulia ili kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli za kuboresha afya ya mama na mtoto.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi ametoa agizo hilo mapema leo katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida mara baada ya kupokea vitanda vya kujifungulia 14, magodoro 20 na mashuka 50 vyenye thamani ya zaidi ya milioni 121 kutoka kwa Rais Magufuli.

Dkt Nchimbi amesema halmashauri zinatakiwa kuiga mfano wa Rais Magufuli anayojali afya kwa ajili ya wananchi hivyo wanapaswa kutenga kiasi cha shilingi milioni kumi na tatu kwa ajili ya kununua vitanda hivyo kwa mwaka huu wa fedha.

“Tumezoea kupokea tu na tumepokea sana vifaa tiba kutoka kwa rais wetu mpendwa Magufuli, hebu tujifunze upendo wake kwa wananchi, hivyo naagiza kila halmashauri inunue vitanda kumi vya kujifungulia nadani ya mwaka huu wa fedha”, amesisitiza Dkt Nchimbi.

Amengeza kuwa akina mama wajawazito wanatakiwa kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma za afya kwakuwa kuna huduma bora zaidi huku akiwataka wakunga wa jadi wawasaidie wajawazito kufika katika vituo hivyo.

Aidha Dkt Nchimbi amemshukuru Mbunge wa Viti Maalumu Singida Aisharose Mattembe aliaminiwa na Rais Magufuli na kumtuma kufikisha vitanda hivyo Mkoani Singida huku akimtaka kuanzisha tunzo ya wakunga watakaosaidia kufikisha akina mama wajawazito katika vituo vya kutolea huduma za afya.

“Natoa shukrani zangu za dhati kwa niaba ya wananchi wa Singida kwa Rais Magufuli kwa kuendelea kutujali wana Singida, pia nakushukuru kwa uaminifu wako mbuge wetu Mattembe kwa kufikisha vifaa hivi salama ila naomba uanzisishe tunzo ya wakunga wa jadi watakaowashauri vizuri na kuwafikisha katika vituo vya kutolea huduma za afya akina mama wajawazito”, amesema Dkt Nchimbi.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Emmanuel Kimario amemshukuru Rais Magufuli kwa vitanda hivyo vitakavyosaidia kupunguza uhaba wa vitanda, hasa kwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa ambapo wajawazito wengi wanapenda kujifungulia kwakuwa na imani napo kutokana huduma bora zinazotolewa.

Dkt Kimario amesema mpaka sasa bado kuna akina mama wanajifungulia nyumbani na kwa wakunga wa jadi jambo linalohatarisha afya ya mama na motto hivyo wafuate ushauri wa kufika katika vituo hivyo mara tu wanapo hisi kuwa na ujauzito.

‘Takwimu za kuanzia kipindi cha mwezi wa saba mpaka wa tisa mwaka huu zinaonyesha kuwa akina mama waliojifungulia ni 12,431 ambapo kati yao 190 wamejifunguliwa nyumbani, akina mama 78 wamejifunguliwa kwa wakunga  na wengine 258 wamejifungulia njiani”, amesema Dkt Kimario.

Kwa upande wake Naibu Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Maulidi Kiaratu amewapongeza wauguzi na madaktari wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa kwa huduma nzuri wanazotoa hadi kusababisha wagonjwa wengi kukimbilia hapo.

Amesema, “unakuta mgonjwa anaacha aspirini pale kituo cha afya Sokoine na kuja hapa Hospitali ya Mkoa akiwa na imani kubwa hata akipewa dawa ile ile hapa atapata nafuu, hivyo nawapongeza sana na muendelee na moyo huo wa kuwahudumia vizuri wagonjwa hata kama tunapata changamoto akati wa kuwalaza wanapokuwa wengi”, amesisitiza Kiaratu.

Ameongeza kuwa Mbunge wa Viti maalumu Singida Aisharose Mattembe amekuwa mstari wa mbele katika kusimamia afya ya mama na mtoto inaboreka Mkoani Singida huku akijitolea vifaa mbalimbali kama vitanda na mashuka,  jambo ambalo ni faraja kwa akina mama na wananchi wote.

TADB YAJADILIANA NA BENKI YA MAENDELEO YA CHINA NA MFUKO WA MAENDELEO YA AFRIKA WA CHINA

Katibu Mkuu wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Prof. Adolf Mkenda akisisitiza jambo wakati wa Kikao cha Pamoja kati wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Mfuko wa Maendelo ya Afrika wa China (CADFUND) kilichofanyika Shangrila Hotel, Guangzhou China juzi. Kushoto kwake ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB Bwn. FRANCIS Assenga na kulia kwake ni Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki na Afisa Ubalozi wa Tanzania nchini China Bwn. Lusekelo Gwassa.

PICHA YA PAMOJA ya baadhi ya Washiriki wa Kongamano la Ushiriani wa Biashara na Uwekezaji kati ya China na Tanzania likilofanyika Guangzhou China Oktoba 2017. Katikati ni Katibu Mkuu wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Prof.  Adolf Mkenda aliyekuwa Mgeni Rasmi wa Kongamano hilo, kulia kwake ni. Mhe. Adam Kimbisa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki; Katibu Mkuu wa Biashara Viwanda na Masoko wa Zanzibar Bw. Juma Alli Juma; Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki; na Mkurugenzi wa Uwekezaji wa Sekta Binafsi (TPSF) Bw. Akaro. Kulia kabisa aliyesimama ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo Tanzania (TADB) Bw. FRANCIS Assenga.

Baadhi ya Washiriki wa Kongamano la Biashara, Viwanda na Uwekezaji lililofanyika Guangzhou China Oktoba 2017 wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi wa Kongamano hilo Pro. ADOLF Mkenda (Katibu Mkuu wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji anayeshughulikia Uwekezaji. Wa pili kushoto kwa Prof. Mkenda ni Bwn. FRANCIS Assenga, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB na kulia kabisa wakiokaa ni Bwana Du Chuan, Mkurugenzi wa Biashara ya Mihogo wa Shirika la Sinolight International Holdings la China linayojishughulisha na uzalishaji na uagizaji wa mihogo toka nje.

Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Bwn. FRANCIS Assenga; Katibu Mkuu wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Bwn. ADOLF Nkenda; Makamu Rais na Naibu Mtendaki Mkuu wa CADFUND Bwn. Wang Yong na Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki, mara baada ya kumalizika kwa kikao cha pamoja
Ujumbe wa Tanzania wakiwa kwenye Picha ya Pamoja na Makamu Rais wa Mfuko wa Maendeleo ya Africa wa China 'CADFUND".
Na Mwandishi wetu,
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imefanya mazungumzo na Taasisi mbili muhimu za kifedha na kiuchumi nchini China kwa ajili ya upatikanaji wa fedha za uwekezaji mkubwa kwenye miundombinu na viwanda nchini Tanzania hususan kwenye Sekta ya Kilimo.

Majadiliano hayo yalifanywa kati ya Ujumbe wa TADB ulioongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki , Bw. Francis Assenga alipokutana na Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya China (CBD) kwenye Mkutano uliofanyika Shangrila Hotel, Guangzhou China wakati wa Kongamano la Pamoja la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na China.

Pande zote mbili zilikubaliana kuendelea na kuimarisha ushirikiano  utakaowezesha kupatikana kwa fedha kwenye uwekezaji wa miundo mbinu ya kilimo na viwanda vidogo vidogo vya uongezaji thamani kwenye mazao ya kilimo kwa wakulima nchini.

Katika ziara hiyo TADB pia ilifanya  majadiliano ya kina na Mfuko wa Maendeleo ya Africa wa China (China African Development Fund) ambao hufanya uwekezaji mkubwa wa miradi ya maendeleo na ya kibiashara (Equity investmenta) kwenye nchi za Afrika ikiwemo Tanzania.

Mazungumzo hayo yalihudhuriwa na Ujumbe wa ulioongozwa na Makamu Mtendaji wa Rais na Naibu Mtendaji Mkuu wa 'CADFUND' Bwn. Wang Yong aliyefuatana na Mkurugenzi Mkuu wa Sekta ya Viwanda, Kilimo, Afya na Uwekezaji, Bw. Lei Ma; Mkurugenzi Mkuu wa Maendeleo ya Masoko na Huduma Elekezi Bw. Henry Liu; na Meneja wa Uwekezaji wa Viwanda, Ardhi na Kilimo Bw. Luo Zhongquan.

Ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Katibu Mkuu wa Viwanda Biashara na Uwekezaji (UWEKEZAJI), Prof. Adolf Mkenda. Wengine waliohudhuria ni Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki; na Afisa Ubalozi wa Tanzania nchini China Bw. Lusekelo Gwassa.

Katika mazungimzo hayo, pamoja na mambo mengine CADFUND walikubali kuendelea kutoa fedha kwenye miradi ya kiuchumi na uwekezaji mkubwa kwenye nyanja kuu nne zikiwemo kilimo; viwanda; madini; na miundombinu kama ya maji na umwagiliaji.

Aidha CADFUND na TADB ziliainisha maeneo kadhaa ya ushirikiano kama vile Uhakiki na Usimamizi wa miradi; Utafiti; Ukaguzi; na Ujengaji wa Uwezo.