ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 29, 2017

AIRTEL YATOA MAFUNZO YA TEHAMA KWA WALIMU DAR.

Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando (kushoto) akiangalia namna walimu wa Shule ya Msingi Kijitonyama wanavyojifunza kompyuta katika maabara ya “Airtel Fursa Lab” Dar es Salaam jana.

Meneja Matukio wa Airtel Tanzania, Jane Matinde (kushoto) akiangalia namna walimu wa Shule ya Msingi Kijitonyama wanavyojifunza kompyuta katika maabara ya “Airtel Fursa Lab” Dar es Salaam jana.


Airtel yatoa mafunzo ya TEHAMA kwa Walimu Dar

Kampuni yasimu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na Atamizi ya Teknohama ya Dar es Salaam (DTBi)  imeanza kutoa mafunzo ya Tehama kwa waalimu katika maabara ya kompyuta iliyopo katika shule ya msingi kijitonyama Manispaa ya Kinondoni.

Mafunzo hayo kwa waalimu yameanza kufuatia Airtel na DTBi kutangaza kuanza kwa mafunzo hayo na kuwaalika vijana kuanzia ngazi ya shule za msingi,sekondari, vyuo vikuu na wafanya biashara kujiandikisha na kufaidika na mafunzo haya yatakayowasaidia kuvumbua application mbalimbali, kuwapatia vijana ujuzi katika mswala ya Tehama na pia kuwawezesha vijana wajasiriamali kuendesha shughuli zao za kibiashara kwa kutumia technologia za kisasa

Akiongea kuhusu kuanza kwa mafunzo hayo, Meneja Mradi wa Airtel Bi Jane Matinde alisema,
‘Hapo awali tulikuwa tumeanza kutoa mafunzo ya Tehama kwa wanafunzi lakini tumeona ni bora na waalimu wa hapa shule hii Kijitonyama nao waanze kupata mafunzo. Hii itasaidia kwani kwa baadae ndio watakaokuwa wakitoa mafunzo kwa wanafunzi na hii itatupa nafasi ya kuendelea kuwezesha shule zingine.
Waalimu wamepokea hatua hii kwa furaha na wanao hamasa kubwa kwenye mafunzo. Hii inathibitisha nia ya kampuni ya Airtel ya kutoa fursa kwa kila Mtanzania, aliongeza Matinde.
Hata hivyo, Matinde alisema kuwa mafunzo kwa wanafunzo ambao walikuwa washaanza yataendelea vile vile. ‘Utaratibu wa kutoa mafunzo kwa wale wanafunzi ambao walikuwa washaanza utaendelea vile vile. Kilichofanyika ni chukua hatua ya ziada ya kuwapa walimu mafunzo ya Tehama ili nao waweze kuwa kwenye nafasi ya kutoa mafunzo kwa wanafunzi hawa’ alisema Matinde.

Matinde aliongeza kuwa bado tunapokea maombi ya kujiunga hivyo tunatoa wito kwa vijana wa sekondari , wale waliomaliza darasa la saba , wafanyabiashara kutumia vyema maabara hii yenye lengo la kuwezesha jamii  hususani vijana kuongeza ujuzi na ueledi kwenye maswala ya technologia na Tehama kwa ujumla.

Kwa upande wake Meneja wa maabara ya Airtel Fursa, Agape Jengela alisema “ Tayari tumejipanga kutoa mafunzo kwa walimu wa shule ya Kijitonyama. Tuhahakisha kuwa walimu wamepata mafunzo na kuelewa kabisa ili nao waanze kutoa mafunzo na elimu kwa wanafunzi.

Jengela alisema mafunzo hayo ni pamoja na lego Robotics, program za uhuishaji kwa watoto(ziitwazo scratch) na ubunifu na uchapishaji wa“3D objects”  msingi wa kompyuta, uelewa wa kompyuta, kutengeneza program mbali mbali

Bado tunapokea maombi,   Tunato wito kwa wazazi na walezi kuwaandikisha vijana wao kwa kupitia  www.teknohama.or.tz na  www. airtelfursa.com  au kwa kutembelea maabara  iliyopo katika shule ya msingi kijitonyama

JAFO: WATENDAJI MSILETE LELEMAMA USIMAMIZI MIRADI YA MAENDELEO

 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua Kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni, Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu na Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki (CCM) Mhe Daniel Mtuka
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakikagua chumba cha kuhifadhia maiti katika kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akitembelea na kukagua mradi wa maji Kintinku/Lusilile wilayani Manyoni
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akimshukuru Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo kwa ukaguzi wa miradi ya maendeleo.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua mradi wa maji Kintinku/Lusilile wilayani Manyoni
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua chumba cha dawa katika Kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni, Mwingine ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu
  
Na Mathias Canal, Singida

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Tamisemi) Mhe Seleman S. Jaffo (Mb) amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida kuanza haraka Mradi wa Ujenzi wa Chumba Cha upasuaji, na Ujenzi wa wodi ya kisasa.

Naibu Waziri Jaffo ametoa maagizo hayo wakati alipokuwa akizungumza na watumishi wa kituo Cha afya Kintinku mara Baada ya kutembele na kujionea uduni wa upatikanaji wa Huduma katika kituo hicho.

Alisema Mradi huo utaambatana na Ujenzi wa maabara kwa ajili ya vipimo kwa wagonjwa, Ujenzi wa eneo la kuchomea taka na Ukarabati wa eneo la kuhifadhia maiti.

Jafo ameonyesha kukerwa na ucheleweshwaji wa kuanza Ujenzi huo licha ya serikali kupeleka fedha kiasi cha shilingi milioni 500 katika mwaka wa fedha 2017/2018 zitakazotosha kukamilisha Ujenzi wote.

Alisema katika awamu ya Pili zitatolewa fedha kiasi cha shilingi milioni 220 zitakazotumika kununua vifaa vyote katika Chumba Cha upasuaji na vifaa tiba kwa ujumla.

Naibu Waziri Jafo alisema kitendo Cha kuchelewa kuanza Ujenzi huo kinachelewesha kuwapatia huduma bora wananchi ambayo inahubiriwa na serikali ya awamu tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli.

"Haiwezekani Rais anatoa fedha kwa ajili ya kuboresha sekta mbalimbali nchini ikiwemo sekta ya Afya halafu kuna watu wachache wanashindwa kusimama vizuri fedha Hizo Jambo ambalo linapelekea serikali kulaumiwa na wananchi" Alisema Jaffo

Katika hatua nyingine Mhe Jaffo alimuagiza mhandisi wa Maji Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Vijijini Eng Gasto Mbondo kutekeleza mpango wa shughuli za utoaji wa Huduma ya maji kupitia Mradi wa kisima Cha Kintinku/Lusilile kilichopo Kijiji Cha Mbwasa (Mbwasa Well Field) kwani eneo Hilo linaonekana kuwa na maji ya kutosha.

Akikagua mradi huo Mhe Jaffo alisema tatizo kubwa kwa wananchi Ni pamoja na changamoto sugu ya upatikanaji Huduma za maji hususani vijijini na kukamilika kwa mradi huo utapunguza umbali na muda wanaotumia wananchi kutafuta maji. 

Awali Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Eng Gasto Mbondo akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za utoaji wa Huduma ya maji alisema kuwa Mradi huo wa maji wa Kintinku/Lusilile utakapokamilika unatarajia kuhudumia watu wapatao 45,417 kwa kuongeza 19.2% kutoka 42.1% iliyopo mpaka 61.3% na utakuwa na Vituo 81 vya kuchotea maji (DPs).

Naye Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Alisema kuwa utekelezaji wa miradi hiyo utasimamiwa kwa karibu na ofisi yake ili kuongeza Hamasa na tija.

Pia alisema katika Mradi wa Ujenzi wa majengo kwa ajili ya kituo Cha Afya Kintinku asilimia kubwa ya mafundi watatoka katika Wilaya ya Manyoni ili kutoa ajira kwa wananchi husika.

KIITEC LAUNCHED SOLAR POWER PLANT AND SOLAR LABORATORY

Excellency Malika Berak, Ambassador of France in Tanzania (C) cuts a ribbon to officiate the launch of Solar Power plant and laboratory at KIITEC in Arusha, others in photo are senior officials from the partners institutions supporting the Institute.
FTE President Fransis Bronchon,(R) briefing invited guests on Solar Project at KITEEK during the launch event at Arusha.
Excellency Malika Berak, Ambassador of France in Tanzania(C) got briefing on project from, Albert Mtana, (R)-Teacher of Electrical and Solar Photovoltaic System (L) is Michel Ramser-VP Strategic Marketing and Sponsorship (ADEI).
The Kilimanjaro International Institute for Telecommunications, Electronics and Computers (KIITEC) has launched 30KW solar power plant and solar laboratory at its training centre in Arusha recently.

The Guest of Honour at launch event was Her Excellency Malika Berak, Ambassador of France in Tanzania, also the event brought together the partners that have supported KIITEC for many years. These are: Schneider Electric East Africa, the Schneider Electric Foundation, ADEI, EDF Help and the Foundation for Technical Education (FTE).

Speaking during the event, KIITEC Director of studies, Mr. Daniel Mtana, said the opening of this solar power plant speaks to the accomplishment of institute’s vision to become the centre of training excellence for renewable energy, particularly solar photovoltaic systems in East Africa. “Committed to true hands-on experience, KIITEC has now invested heavily in photovoltaic solutions and strives to be recognized as the premier provider of quality technical education in a student-centered community.”

General manager at Schneider Electric East Africa, Mr. Mr. Edouard Heripret, said in most sub-Saharan countries, the rate of enrolment in formal secondary technical and vocational training and education (TVET) does not exceed 5%. “Vocational training has always been at the heart of Schneider Electric’s DNA. In East Africa, we have been committed to support technical training since 2009. Kiitec was one of our first training partners and I am pleased today to participate in the inauguration of the solar plant and laboratory, as these new components will allow students to have a full set of competencies to enter the labour market and will support access to energy for everyone.”

Mr. Heripret added “At Schneider Electric, we are building sustainable communities through energy knowledge and leadership, thanks to the Schneider Electric Foundation. Its aim is to contribute to the development of people and societies through education, innovation, awareness-raising and vocational training related to energy. It acts, anywhere in the world where the company is present, through its three programmes.

KIITEC is an international technical institution, was founded in 2004 by French engineers and has produced some of the most competent technicians in the country. Two NGOs, the Foundation for Technical Education (FTE-Swiss) and Action Development Education International (ADEI-French), support the institution. Schneider Electric assists ADEI in its support of KIITEC.

The institute is a pilot centre, with the goal of transposing and exporting its model from Tanzania, to Kenya. It provides its students with the basic skills in telecommunications, electronics, information science, networks and industrial automation systems. The training lasts over two years. It comprises lectures complemented by practical training, project design, and a three-month outplacement in a company. As of today, 350 young people, comprising 90% of the students, have obtained their diploma, the ‘National Technical Award’, which is recognized by the local government, and have all found jobs, mainly in the industrial maintenance sector.

MEYA CHADEMA NJE NDANI.

MEYA wa Ubungo, Boniface Jacob (Chadema), amehojiwa kwa saa tatu na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, kwa madai ya kutumia ofisi za umma kufanya vikao vya chama.

Akizungumza baada ya kumaliza kuhojiwa jana jijini Dar es Salaam, Jacob alisema, alitoa utetezi wake kuwa hakufanya kikao isipokuwa alitembelewa na wageni wa chama, lakini kama wanaona anastahili kuwajibishwa wafanye hivyo.

Kadhalika Jacob alisema alitoa ushaidi wa matumizi mabaya ya ofisi za umma, yanayofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Nimewaeleza Sekretarieti kuwa,  pia CCM, kimekuwa kikifanya vikao vyake Ofisi za Ikulu na wamenieleza hakuna aliyewahi kulalamika. Hivyo nimelazimika kuandika barua ya malalamiko juu ya kitendo hicho,” alisema.

Kuhusu shauri lake la vyeti feki aliloliwasilisha mahakamani Mhe. Boniface amefunguka "Nikiwa hai nikiwa mfu ningependa shauri lifike kwenye baraza la maadili" 

Kuitwa na kuhojiwa kwa Jacob na Sekretarieti hiyo kumetokana na kitendo chake cha kumkaribisha ofisini kwake Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na Mwenyekiti wa chama hicho Kanda ya Pwani.

Thursday, September 28, 2017

MTO MIRONGO WAFUNGUKA LEO BAADA YA ZAIDI MIAKA TISA

NA ZEPHANIA MANDIA WA G.SENGOBLOG TV.


Ongezeko la idadi ya watu katika sehemu za mijini imekuwa chanzo kikubwa cha uzalishaji wa taka kutokana na shughuli mbalimbali za kibinadamu zinazofanywa katika maeneo hayo hivyo kupelekea gharama kubwa ya usafishaji KIOMONI KIBAMBA kurugenzi wa jiji la mwanza amesema mto huo unazaidi ya miaka tisa bila kufanyiwa usafimkubwa kama huo.


Ikiwa ni muda mchache kufikia majira ya mvua za masika mkurugenzi wa Jiji la Mwanza KIOMONI KIBAMABA ameanza jitihada za kusafisha maeneo korofi ya jiji la Mwanza kwa kuanza na Mto Mirongo uliyopo katikati ya jiji la Mwanza.


Takataka pamoja na mchanga unaotoka katika maeneo mbalimbal za jiji la Mwanza hupitia katika mto Mirongo ambao humwaga maji yake katikaziwa victoria.


Mkuruenzi wa jiji la Mwanza KIOMONI KIBAMBA anasema ameamua kuwa mfano wa kusafisha mto huu ili kuepukana na madhara mafuriko yanayosababishwa na uchafu unaopita katika mtoa huo.


Wananchi mbalimbali walioshuhudia mto huo ukisafishwa waliipongeza halamahuri ya jiji mwanza kwa kusafisha mto huo ambao kwa kiasi kikubwa umekuwa na madhara kwao.


Kila mwezi jiji hilo ulipa milioni 250 kwa ajili Usafi wa mazingira wa jiji la mwanza hivyo kufanya  eneo hilo kuchukua kiasi kikuwa cha mapato ya jiji hilo kwa kuwalipa watendaji na kampuni zinazo jihusisha na usafi w jiji hilo,G.SENGO TV imefika katika mto huo nakushudia mkurugenzi KIOMONI KIBAMBA akisaidiana na watendajiwake kuhakikisha mto huo unafungunguka maramoja kabla ya mvua za masika.

MAGUGU MAJI MAKUBWA KAMA YALE YALIYOSIMAMISHA SAFARI ZIWANI VICTORIA MWAKA 2015 YAVAMIA ENEO LA JEMBE BEACH.

Ni kama msitu mnene au kama kisiwa kinachotembea ambacho ghafla kimeizinga ghati ya Jembe Beach Resort kwa upande wa maji mbele. 

Wadudu na wanyama wakali kama mamba, nyoka, kasa, chatu hata nyani wa msituni huishi kwenye magugu haya yaliyo changanyika na magugu aina ya matende. 


Taswira hii imetanda kwa takribani siku 3 hadi hii leo ambapo imehama na kuelekea upande wa pili wa fukwe na kujikita.

Pamoja na kuwa na faida kama sura ya Utalii pia magugu haya yanasifika kama chanzo cha mazalia ya samaki wa aina mbalimbali.

Moja kati ya athari kubwa inayojitokeza pindi magugu haya yanapotanda ni pale yanapoathiri shughuli za usafiri na usafirishaji kwani hukinga njia za boti na meli zinazosafiri ziwani, ilitokea mwaka 2015 eneo la Kigongo wilayani Misungwi mkoani Mwanza kiasi cha kutatiza shughuli za usafiri na usafirishaji ambapo zaidi ya magari 200 ya mizigo yalikwama kusafiri katika eneo la Kigongo na Busisi na kuleta athari kubwa kwa wananchi, wafanyabiashara na wasaka huduma.

Magugu maji yalitanda ziwa Victoria eneo la kivuko hicho kwa ukubwa kwa hekari nne na kusababisha vivuko kutofanya kazi.

Mbele ya ghati ya Jembe Boat.

Kwa wale wananchi wanaoteka maji, kuoga, kufua au kufanya shughuli zozote za kijamii  kando kando mwa ziwa Victoria huwa hatarini kuliwa na mamba + nyoka wanaoweka makazi yao chini na ndani ya magugu maji.... 

Habari iliyosikikika katika #KAZINANGOMA @mansourjumanne @gsengo @djscorpion

Kutoka upande wa pili na muonekano wa Mbele ya ghati ya Jembe Boat na Jembe Beach uliofichwa na magugu hayo.

WANAHABARI WATEMBELEA MITAMBO YA UZALISHA MAJI YA DAWASCO YA RUVU CHINI NA JUU.

Baadhi ya Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wamefanya ziara ya siku moja katika Mitambo ya Uzalishaji Maji ya Ruvu Juu na Ruvu Chini  iliyopo Mlandizi na Bagamoyo mkoani Pwani ,ziara iliyoandaliwa na Shirika la Maji safi na Maji taka Dar es Salamaa (DAWASCO) kwa lengo la kujifunza namna matibabu ya maji yanavyofanyika kuanzia yanapotoka mto Ruvu.
Mbali na kutembelea Mitambo ya uzalishaji maji pia Wanahabari hao wametembelea ofisi za Dawasco mkoa wa Tabata kujionea utendaji kazi kwa watendaji wa Shirika hilo ,kituo cha Tabata. 
Meneja wa Dawasco Tabata, Victoria Masele akiwakaribisha wanahabari ofisi kwake mara baada ya kumtembelea.
Meneja Biashara wa Dawasco Tabata, Jamal Chuma kifafanua jambo kwa wanahabari.
Vifaa vilivyopo katika ofisi za Dawasco Tabata.
Mtambo wa kuzalisha Maji Ruvu Juu.
Maji yakiingia katika mitambo.
Kina cha maji kinavyoonekana.
Meneja 
Meneja wa Mtambo wa Ruvu Juu, Edward Mkilanya akiongea machache na wanahabari.  
Mhandisi wa Mtambo wa Ruvu Chini, Emaculata Msigali akitoa ufafanuzi jinsi unavyofanya kazi.