ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 24, 2017

MAGAZETI YA LEO:- KIAMA VIWANDA 197, WAPINZANI, NGO WAMUUNGA MKONO MAGUFULI, UJUMBE KUUA POLISI WAZIDISHA HOFU KIBITI, MIMBA ZA SHULENI SASA NONGWA.


Kiama viwanda 197, wapinzani,NGO wamuunga mkono Magufuli,ujumbe kuua polisi wazidisha hofu kibiti,mimba za shuleni sasa nongwa, kigogo TBS asiye raia ahukumiwa.

Mpinzania aitabiria makubwa CCM,Serikali yamwaga ajira mpya tena, kwanini Chenge kila kashfa yumo? JPM apingwa mjadala wa mimba shuleni,Kinana ang’aka CCM.






Friday, June 23, 2017

VIDEI:- KANISA LAENDA KUHIJI......



Waamini wa dhehebu wa kanisa katoliki wametakiwa kuenzi na kuhifadhi maeneo ya kistoria ya kanisa hilo ili historia ya kanisa izidi kuwepo kwa vizazi vijavyo.

Katika safari ya hija ya kumbukumbu ya wamisionarai waliofika Afrika Mashariki wakianzia Tanzania na baadae nchini Uganda mahujaji hao wamesema ipo haja ya historia ya kanisa kuenziwa kwa kuboresha sehemu za historia.

Baada ya wamisionari kutoka Bagamoyo na Zanzibar walifikia hapa KAGEYE mkoani Mwanza  ili kueneza injili kwa kanda ya ziwa na baadae kuingia  nchi jirani Uganda, eneo hili la kageye linabaki kuwa chimbuko la kanisa hili.

Safari ya mahujaji hawa kutoka mkoa wa Mwanza kuelekea nchini Uganda ililenga kutembelea maeneo ya kihistoria ya kanisa katoliki wakianzia Kageye,Bukumbi mkoani Mwanza ambapo kanisa la kwanza la katoliki lilijengwa,  na baadae kuhitimisha na Namgongo nchi Uganda.Pause

Maeneo ya kihistoria ya kanisa inadaiwa kukosa muamko wa waamini kutembelea na kujifunza historia ya kanisa iliyoachwa na wamisionari walifika Afrika kueneza injili ya kikristo.Pause

Ni miaka 150 sasa ya ukristo tangu dini hii ingie Tanganyika baada ya wamisionari  roho mtakatifu kuingia Tanganyika tangu mwaka  1868 kupitia Bagamoyo na Zanzibar ili kueneza dini la kikristo.

VIDEO:- AJICHOMA KISU, KISA KWA UGOMVI WA MAPENZI.

Katika hali isiyo ya kawaida binti mmoja jijini Mwanza amejichoma kisu kwa kile kinachodaiwa kuwa ni ugomvi wa kimapenzi na aliyekuwa mpenzi wake.

Binti huyo anayejulikana kwa jina la MERRY KIGORO amechukua hatua hiyo kataika mtaa wa uhuru baada ya aliyekuwa mpenzi wake kukataa kurudiana naye.

Mapenzi niu hivi ndivyo kuwa kwa binti huyu katika mtaa wa uhuru jijini Mwanza ambaye alijaribu kutoa uhai kwa sababu ya mapenzi  ama kweli kweli mapenzi  yanaua. 


Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walieleza jinsi walivyoshuhudia tukio hili wakaeleze kile walichokiona.

UCHAGUZI KENYA:- MATOKEO YA URAIS KUTANGAZWA RASMI KWENYE MAENEO - BUNGE

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi na mipaka nchini Kenya Bw. Chebukati anasema tume hiyo imejiandaa vyema kwa zoezi la uchaguzi

Mahakama ya Rufaa imeamua matokeo rasmi ya kura za urais yatatangazwa na wasimamizi wa uchaguzi vituo vya kuhesabu kura kwenye maeneo bunge.

Uchaguzi wa Kenya utafanyika tarehe nane mwezi Agosti mwaka huu ambapo Rais Uhuru Kenyatta atang'ang'ana kuhifadhi wadhifa wake dhidi ya mpinzani wake wa jadi Raila Odinga.

Uamuzi huo wa majaji watano wa Mahakama ya Rufaa umeonekana kama ushindi mkubwa kwa muungano wa upinzani.

Jopo la majaji watanao limesema kwamba mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi nchini Kenya IEBC hana mamlaka kisheria ya kuhakiki na kutangaza matokeo ya urais.

Msimamo wa tume ya uchaguzi, ni kwamba lazima maafisa wake wahakiki matokeo yote kutoka maeneo bunge katika kituo cha kitaifa cha kuhesabu kura, na kwamba wana uwezo wa kubadilisha matokeo hayo.

Serikali ilikuwa inaunga mkono msimamo huo, japo upinzani ulipinga.

Kwa muda mrefu upinzani umekuwa ukieleza wasiwasi wake kuhusu uwezekano wa muungano tawala kushirikiana na tume ya uchaguzi kuhujumu matokeo ya uchaguzi.

Tume ya uchaguzi imekana madai hayo.

Uchaguzi wa agosti 8, unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa baina ya rais Uhuru Kenyatta na mpinzani wake mkuu wa muungano wa upinzani NASA, Raila Odinga.

Mahakama hiyo pia ilisema mahakama ya juu ina uwezo wa kisheria wa kutatua mizozo inayotokana na uchaguzi wa urais.

NIMEUMIA KUONDOKA NIYONZIMA, SINA JINSI - MSUVA

KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva amefunguka kuwa, kitendo cha Haruna Niyonzima kuondoka kikosini hapo, kimemuachia maswali mengi yasiyokuwa na majibu, hivyo ataendelea kummisi kila kukicha.

Niyonzima ambaye msimu ujao ataitumikia Simba, ameondoka Yanga baada ya kumaliza mkataba huku akishindwa kuongeza kutokana na kushindwana kimaslahi na viongozi wake hao wa zamani.

Akizungumza na Championi Ijumaa,Msuva alisema, kati ya wachezaji wote wa kigeni aliowahi kucheza nao ndani ya Yanga, Niyonzima ndiye aliyetokea kuendana naye kwa kila kitu.

“Kwa kweli Haruna nilimzoea kupitiliza, alikuwa kama mtani wangu, hivyo basi kwa hali hiyo iliyotokea, kwa upande wangu nimeumia sana lakini sina jinsi.

“Kuondoka kwake haimaanishi kwamba nitashuka kiuwezo, bali nitaendelea kupambana na nitashirikiana na wengine kama nilivyokuwa nashirikiana naye.“Nitamisi vitu vingi kutoka kwake, najua hata yeye huko alipo nadhani anafahamu ameniacha kwenye hali gani, nasema hivyo kwa sababu kati ya wachezaji wa nje niliowahi kucheza nao, yeye pekee ndiye nimevutiwa naye,” alisema Msuva.
Ibrahim Mussa

MAPIGANO MAKALI YARIPOTIWA MASHARIKI MWA CONGO, 16 WAFARIKI DUNIA

Mapigano makali yameripotiwa kati ya askari wa jeshi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na makundi ya waasi huko kaskazini mashariki mwa nchi hiyo na kusababisha mauaji ya watu 16.

Msemaji wa jeshi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo amesema kuwa, mapigano makali yaliyotokea jana kati ya jeshi hilo na makundi ya wanamgambo katika mji wa Beni mkoani Kivu Kaskazini yamesababisha vifo vya watu wasiopungua 16 na kujeruhi wengine wengi.

Duru za polisi katika mkoa huo zimeripoti kuwa, mapigano hayo yalitokea wakati waasi walipojaribu kuwaachia huru wafungwa wanaoshikiliwa na vyombo vya usalama.
Maelfu ya watu wameuawa Congo kutokana na machafuko ya ndani.
Maeneo ya mashariki na kaskazini mashariki mwa Congo yamekumbwa na mapigano makali baina ya jeshi la serikali ya nchi hiyo na makundi ya wanamgambo, na maelfu ya watu wameripotiwa kuuawa na mamilioni ya wengine kulazimika kukimbia makazi yao.
 
Uchunguzi uliofanwya na baadhi ya vyombo vya habari umebaini kuwa, watoto wadogo huko katikati mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ndiyo wahanga wakuu wa vita katika vinavyoendelea katika maeneo hayo.

MOHAMED SALAH AVUNJA REKODI LIVERPOOL.

Jana majogoo wa London klabu ya Liverpool walithibitisha kumsajili winga wa As Roma Mohed Salah ambaye walimtafuta kwa muda sasa kwa dau la euro million 39.

Hii sio mara ya kwanza kwa Salah kucheza katika ligi kuu nchini Uingereza kwani hapo mwanzo kabla hajahamia nchini Italia aliwahi kukipiga na timu ya Chelsea.

Mohamed Salah amesema ujio wake Liverpool ni tofauti na Chelsea kwani kipindi wakati anaenda Chelsea alikuwa bado mtotomtoto lakini sasa anajiona ni bora zaidi.

“Nina uhakika 100% kwamba kila kitu kimebadilika hadi muonekano wangu,kipindi kile nilikuwa na miaka 20 ila sasa nina 24 na nina uzoefu mkubwa zaidi tofauti na hapo mwanzo” alisema Salah.

Mkataba wa Salah na Liverpool utamfanyia kila mwisho wa wiki kuweka kiasi cha euro 90,000 huku akikabidhiwa jezi namba 11 na Firminho akipewa jezi namba 9.

Usajili wa Mohamed Salah wa euro million 39  umevunja rekodi ya usajili ya klabu hiyo ambayo ilikuwa ikishikiliwa na Andy Caroll aliyesajiliwa kwa euro milion 35 mwaka 2011.Na hii ndio orodha ya usajili wa ghali ndani ya klabu hiyo.

1.Mohamed Salah (euro 39m).

2.Andy Carroll (euro 35m).

3.Sadio Mane (euro 34m)

4.Christian Benteke (euro 32.5m)

5.Roberto Firminho (euro 29m)

KATIBU MKUU WA CCM APIGA MARUFUKU WAGOMBEA KUUZIWA FOMU.

TAARIFA MUHIMU:
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana amepiga marufuku uuzaji wa fomu za uchaguzi kwa ngazi zote za uongozi ndani ya Chama.

Taarifa iliyosainiwa na Naibu Katibu Mkuu Bara Ndugu Rodrick Mpogolo kwenda kwa Makatibu Wakuu wa Jumuiya imeeleza kuwa kwa mwanachama yeyote aliyeuziwa fomu arejeshewe pesa yake.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.

MAMA AMUUA MTOTO WAKE.

Mtu mmoja anayejulikana kwa jina la Nyamiji Bahati makazi wa kisiwa cha Nyamanga wilayani Sengerema mwenye umri wa miaka 27 kabila msukuma, amepandishwa kizimbani katika mahakama ya wilaya ya sengerema kwa kosa la kumuuwa mototo wake mwenye umri wa miaka 7.

 Akisoma shtaka hilo mbele ya hakimu makazi bi Subira Mashimbo mwendesha mashtaka Silvester Mwaiseje amesema mtuhumiwa ametenda kosa hilo mnamo tarehe 13/6/2017 majira ya saa saba mchana maeneo ya kisiwa cha Nyamango kilichopo wilayani Sengerema kinyume cha sheria namba 196 na kanuni za sheria kifungu namba 16 na mshtakiwa amerudishwa rumande hadi tarehe 12/7/2017 kesi itakapotajwa mahakamani hapo. 

Thursday, June 22, 2017

VIDEO:- MAZISHI YA SHABIKI WA SOKA ALLY YANGA NYUMBANI KWAO SHINYANGA

HATIMAYE mwili wa aliyekuwa shabiki  kindakindaki wa Dar es salaam Yanga Africans  Ally Said almaarufu Ally Yanga umezikwa hii leo  mkoani Shinyanga kwenye makaburi ya Kiislamu ya Nguzo Nane mkoani hapa.

Mamia ya mashabiki wa soka wa ndani na nje ya nchi wamehudhuria ibada ya mazishi iliyofanyika nyumbani kwao na marehemu maeneo ya mitaa ya   Stendi kuu ya zamani ambako majonzi na vilio vilisikika hii ikimaanisha Ally Yanga alikuwa kipenzi cha watu.

MBUNGE WA CHALINZE ASHIRIKI ZIARA YA RAISI JIMBONI KWAKE.

Mbunge wa Chalinze ameshiriki kwenye Ziara ya Mheshimiwa Raisi Dr.John Magufuli alipofika Wilaya ya Bagamoyo.

Ziara hiyo ya Raisi ambayo ilikuwa na kazi ya Kufungua Miradi ilianza na ufunguzi wa Kiwanda kikubwa cha matunda cha Sayona kilichopo Mboga Wilaya ya Chalinze. Pamoja na kumkaribisha Mheshimiwa Mbunge alimuhakikishia Mheshimiwa Raisi juu ya KUMUUNGA mkono katika hatua anazochukua ikiwemo kupambana na Ufisadi na kuwahakikishoa Watanzania kutawala Uchumi wao. Mheshimiwa Mbunge alimueleza juu ya jitihada ambazo Wana chalinze wanazifanya kujikomboa katika Uchumi tegemezi.

Mheshimiwa Mbunge alimueleza Mh.Raisi jinsi Halmashauri yao ilivyofanikiwa kukusanya fedha kwa kuvuka kiwango cha makusanyo. " Mh. Raisi halmashauri yako hii ya Chalinze imefanikiwa kukusanya zaidi ya Asilimia 102 juu ya makadirio mbayo tulikuwa tumejipangia. Fedha hizi zitapelekwa katika miradi ambayo inagusa wananchi wa chini kabisa ikiwemo kuimarisha huduma za afya, maendeleo ya jamii, mikopo kwa wakina mama na vijana na pia miradi ya maji kwa ajili ya kupunguza makali.
"Mh. Raisi , tumejipanga pia kuhakikisha kuwa halmashauri yetu inajiwezesha yenyewe. Zaidi ya Milioni 200 zimepelekwa kuwasaidia wananchi maskini kimikopo na shighuli za maendeleo.  Kushirikiano na wadau wa maendeleo tumefanikiwa katika haya." Mbunge alieleza.

Pia mbunge alimuomba Mh. Raisi kutumia Chalinze kama sehemu ya ushuhuda wa hatua na jitihada anazochukua kukuza uchumi wa watu na maendeleo ya kweli yanayotazama uelekeo wa kiilani na ahadi zake. Mheshimiwa Mbunge alimueleza Mheshimiwa Raisi kuwa ," kama yupo mtu ambaye ana shaka na utayari wako na uchapakazi wako juu ya sera ya viwanda basi Mwambie aje Chalinze aje kuona jinsi mambo yanavyofanyika." Tunajua wewe ni kazi tu na sisi hapa chalinze ni kazi tu. "

Mheshimiwa Raisi alimshukuru Mbunge na kwa hakika alimpongeza kwa kumfananisha na Baba yake Aliyewahi kuwa Raisi Wa Jamhuri ya Tanzania wakati wa awamu ya Nne. Mheshimiwa Raisi alimfananisha na Nyoka mtoto. "Kwa hakika nimemsikia Mbunge wenu na nimerudhika kuwa Nyoka uzaa Nyoka".Nimekuona na ninakupongez unavyochapa kazi. Hongera sana ."

 
Pamoja na kumshukuru mbunge , Mheshimiwa Raisi aliwakabidhi Halmashauri ya Chalinze majengo ambayo yalitumiwa na Mkandarasi pale Msata wakati wa Ujenzi wa Barabara ya Bagamoyo-Makofia-Masata.

Baada ya kumaliza mkutano huo na kufungua kiwanda cha kuchakata Matunda cha Sayona, Mheshimiwa Raisi alielekea Bagamoyo ambako alifanya mambo mawili makubwa ikiwemo uzinduZi wa Barabara ya Bagamoyo Msata na Kiwanda cha kukausha Matunda kilichopo Mapinga, Bagamoyo.

WAZIRI MKUU AHIMIZA WATANZANIA KULIPA KODI WAKATI AFUNGUA OFISI ZA TRA, WILAYA YA CHATO.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akikata utepe kama ishara ya kufungua jengo jipya la ofisi ya TRA, Wilaya ya Chato, Mkoani Geita katika ufunguzi uliofanyika leo mjini Chato.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa  akipiga makofi baada ya kuwa amekata utepe ambao unaashiria kufunguliwa kwa Jengo la mamlaka ya mapato Wilayani Chato.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akihutubia wananchi wa Chato wakati wa ufunguzi wa jengo la TRA wilayani humo mkoani Geita leo. 

Jengo la mamlaka ya mapato(TRA)Wilayani Chato.

Waziri Mkuu,akiwapongeza na kutoa zawadi kwa kwaya ya Mwagazege  ambao walikuwa wakiimba nyimbo ya kuipongeza serikali ya awamu ya Tano kwa kuendelea kutekeleza Ilani ya chama cha mapinduzi(CCM)

Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga wakipongeza kikundi cha Kwaya kwa wimbo mzuri.
Mkuu wa Wilaya ya Chato,Shaaban Ntarambe akitambulisha wageni ambao walikuwepo kwenye viwanja hivyo.

Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Chato.

Mbunge wa Chato ambaye pia ni Naibu waziri wa Nishati na Madini,Dk Medadi Kalemani akizungumza na wananchi.

Kamishna Mkuu wa TRA Charles Kichere akitoa maelezo ya mradi wa ujenzi wa ofisi ya TRA katika uzinduzi wa ofisi hiyo uliofanyika leo katika wilaya ya Chato, mkoa wa Geita






Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa, amesema kuwa kila mwananchi wa Tanzania anawajibika kulipa kodi kwaajili ya ujenzi wa Taifa na kwamba uchumi  utajengwa na watanzania kwa kufanya kazi kwa bidii na kwa uadilifu mkubwa kwani kufanya hivyo itawaza kusaidia upatikanaji mkubwa wa kodi.

Kauli hiyo ameitoa leo wakati wa zinduzi wa Jengo la mamlaka ya mapato nchini(TRA)Wilayani Chato Mkoani Geita, ambalo ujenzi wake umeghalimu kiasi cha Sh ,Bilioni 1.4.

Waziri Mkuu amesisitiza  kuwa  Kila mwananchi ambaye anastahili kulipa kodi la lazima alipe bila ya kushurutishwa kwani ni jambo la kawaidia na kwamba nchi ambazo zimeendelea ni kutokana na wananchi wake kujenga destuli ya ulipaji wa kodi

Pia ameendelea kueleza kuwa Kutokana na maelekezo ya Ilani,Katika Mwaka 2016/17 Kuanzia Mwezi Julai,2016 hadi kufikia mwezi Aprili ,2017 Serikali imefanikiwa kukusanya Shilingi Trilion 20.7 Sawa na Asilimia 70.1 na kwa lengo la mwaka walijiwekea malengo ya kukusanya Sh,Trilion 29.5,Kati ya makusanyo hayo mapato ya ndani ya kodi yalikuwa ni Sh,Trilioni 11.6 Sawa na Asilimia 77.1 ya lengo la kukusanya Sh,Trilion 15.1

Aidha Waziri Mkuu ametoa Wito kwa Kila mwananchi kuakikisha anadai na kupewa Risiti ya manunuzi ya bidhaa alizonunua na kwamba TRA ihakikishe kila mfanyabishara anakuwa na mashine za kielektroniki.


Kamishina wa mamlaka ya mapato TRA Charles Kichere amesema kuwa  Pamoja na kuboresha miundo mbinu ya majengo Mamlaka imeanzisha mifumo ya ukusanyaji mapato kwa njia za kielekitroniki ambazo zitaunganishwa na ofisi hiyo  ili kutoa huduma kwa urahisi kama ilivyo kwenye ofisi zingine kote nchini. 

"Baadhi ya huduma zitakazotolewa hapa ni kama; Utoaji wa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN),  utoaji wa leseni za udereva, huduma za usajili wa magari, ukusanyaji wa kodi za majengo, na kodi zinginezo ambazo zinasimamiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa mujibu wa Sheria"Alisema Kichere.

"Haya yote yanafanyika kwa lengo la kuhakikisha kodi na tozo mbalimbali zilizopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinakusanywa kikamilifu ili kufikia lengo la makusanyo yanayokusudiwa katika mwaka ujao wa Fedha na kuendelea"Aliseongeza Kichere. 

Jengo hilo ambalo  limefunguliwa  leo lilianza kujengwa mnamo tarehe 13 Julai, 2016 na kumalizika tarehe 12 Juni, 2017 ambapo kazi ya ujenzi ilihusisha ujenzi wa jengo la ghorofa moja kama  ambalo lina nafasi ya kutosha kutoa huduma zote za kodi pamoja na huduma za kibenki ili kuwapunguzia adha walipakodi  kwa kupata huduma zote mahala pamoja.


Kampuni ambayo imejenga jengo hilo ni Wakala wa Majengo Tanzania  (TBA)na mjenzi ni kampuni ya Mayanga Constructions ambapo katika ujenzi huu zimetumika kiasi cha Takriban Shilingi Bilioni 1.4.
IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE

ZIARA YA RAIS MAGUFULI MKOA WA PWANI IMEJAA TIJA



Rais Magufuli amemaliza ziara ya siku 3 mkoani Pwani iliyoanza tarehe Juni 20, 2017 kwa mafanikio yenye tija lukuki kwa Wana wa mkoa wa Pwani na Taifa kwa ujumla.

Katika ziara hiyo, Rais Magufuli amezindua viwanda vitano ambavyo ni viwanda vya vifungashia, kiwanda cha Matrekta, kiwanda cha chuma, kiwanda cha kukausha matunda na kiwanda cha vinywaji baridi cha Sayona.

Uzinduzi wa viwanda hivyo ni muendelezo wa kutekeleza ahadi yake aliyoitoa wakati wa uchaguzi mkuu 2015 wa kuhakikisha Tanzania inakuwa Tanzania ya viwanda. Viwanda hivyo vitasaidia kuondoa tatizo la ajira nchini na pia vitasaidia kupunguza bei za bidhaa husika kwenye soko la kibiashara.

Wawekezaji hao walilalamika juu ya urasimu wakati wa mchakato wa kuanzisha viwanda ambapo Rais Magufuli alitumia ziara hiyo kuagiza urasimu huo ukomeshwe na kuagiza baadhi ya malipo wakati wa kusajilii kiwanda kufutwa ili kuvutia wawekezaji zaidi nchini.

Serikali ya awamu ya 5 ya Dk. Magufuli ambayo ina miaka 2 tangu iingie madarakani imefanikiwa kupata viwanda 393 ndani ya mkoa wa Pwani ambavyo kati ya hivyo viwanda 85 ni viwanda vikubwa. Hakika Tanzania ya viwanda inawezekana

Rais Magufuli huyo huyo amefanya ziara ya kushtukiza katika kiwanda cha kutengeneza dawa za kuulia vimelea vya mbu wanaosababisha malaria kilichopo Kibaha, Pwani ambapo Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Fedha kutoa Sh1.3 bilioni  kwa ajili ya kulipia lita 100 ya dawa  hizo za kuua vimelea vya mbu zilizopo katika kiwanda hicho.

Wizara inatumia gharama kubwa kununua madawa ya kutibu nje ya nchi na kuacha dawa inayozuia maleria ikikosa mnunuzi hapa nchini. Nina uhakika uamuzi huu wa Rais utasaidia kupunguza kuenea kwa ugonjwa wa Maleria hapa nchini.

Katika ziara hiyo, Rais Magufuli amezindua Barabara ya Bagamoyo - Msata ambayo imejengwa kwa fedha zetu wenyewe na walioijenga ni wakandarasi wazawa. Barabara hiyo itasaidia kupunguza foleni ya Barabara ya Dar Kibaha, itaongeza uchaguzi wa njia ya kutoka na kuingia mkoa wa Dar, utasaidia kusafirisha watu na mizigo yao yakiwemo mazao kutoka mashambani na kuyafikisha masokoni kwa gharama ndogo. Hakika Barabara hii ina tija kubwa kwa maendeleo ya Taifa.

Ziara hiyo ya Rais Magufuli imezindua mradi mkubwa wa maji wa Ruvu ambapo utasaidia kuondoa tatizo la maji kwenye mkoa wa Pwani na Mkoa wa Dar es Salaam. Hakika ziara hii imejaa tija.

Katika mkutano wa hadhara wa mwisho wa kuhitimisha ziara yake, Rais John Magufuli amewapa wakazi wa Bagamoyo, eneo la Magereza lenye ukubwa wa heka 65. Alichukua hatua hiyo baada ya wanawake waliokuwa wamebeba mabango, kumtaka awape eneo lao kwa kuwa ni wazaliwa wa Bagamoyo, ni wajane na wana uhaba wa maeneo ya biashara. Amelitaka Jeshi la Magereza kufanya mabadiliko katika hati ili eneo hilo liwe la wananchi.

Pengine bila ya ziara ya Rais Magufuli ni dhahiri wakazi hao wangeendelea kupata mateso yasiyo na kuwasaidia.

Hakika ziara hii ya Rais Magufuli mkoa wa Pwani imejaa tija sana kwa wakazi wa mkoa wa Pwani na Taifa kwa ujumla. Ni wakati sasa wa viongozi ngazi za chini nao kuamua kutoka maofisini na kufanya ziara ili kujua na kujionea matatizo ya Wananchi ili wajue namna gani ya kuwasaidia kuondoa kero zao. JPM ameanzisha mwendo, viongozi wengineo wa ngazi za chini waige mfano huu bora wa JPM kwa jamii.

NAIBU KATIBU MKUU CCM AONGOZA MAZISHI YA ALLY YANGA MKOANI SHINYANGA.



Ibada ya mazishi kwa marehemu iliongozwa na Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Habib Makusanya.

Na Albert G. Sengo

Shinyanga.
HATIMAYE mwili wa aliyekuwa shabiki  kindakindaki wa Dar es salaam Yanga Africans  Ally Said almaarufu Ally Yanga umezikwa hii leo  mkoani Shinyanga kwenye makaburi ya Kiislamu ya Nguzo Nane mkoani hapa.

Mamia ya mashabiki wa soka wa ndani na nje ya nchi wamehudhuria ibada ya mazishi iliyofanyika nyumbani kwao na marehemu maeneo ya mitaa ya   Stendi kuu ya zamani ambako majonzi na vilio vilisikika hii ikimaanisha Ally Yanga alikuwa kipenzi cha watu.

Naibu Katibu Bara wa chama cha Mapinduzi Fredick Mpogoro akitoa salamu za rambirambi za Serikali.
Ibada ya mazishi kwa marehemu iliongozwa na Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Habib Makusanya na kwa upande wa serikali iliwakilishwa na Naibu Katibu Bara wa chama cha Mapinduzi Fredick Mpogoro.

Abdallah Rashidi katibu wa tawi la Yanga Mkoa wa Shinyanga amesema kuwa marehemu alikuwa kiunganishi mkubwa kwa mashabiki wa ndani ya mkoa na nje ya mkoa  na alikuwa mhamasishaji mzuri kwenye masuala ya michezo hata ngazi za kitaifa.

Enzi za uhai wake shabiki  kindakindaki wa Dar es salaam Yanga Africans  Ally Said almaarufu Ally Yanga (mwenye suti)
Mbunge wa Kishapu Suleiman Nchambi (katikati) akiteta na makada wa CCM kwenye  Ibada ya mazishi kwa marehemu Ally Yanga yaliyofanyika nyumbani kwa marehemu mjini Shinyanga.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainabu Telack amesema kuwa serikali imepoteza kijana wa kipekee aliyeunganisha vijana katika uzalendo na kuiasa jamii na vijana waliobaki waige mfano wake.

Naye Naibu Katibu mkuu CCM Fredrick Mporogo akitoa salamu kwa niaba ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania,  Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa Chama kinatambua uwezo wa marehemu katika uhamasishaji kwani kupitia sanaa yake aliweza kuwaunganisha watanzania kuzungumza lugha moja hasa kwenye uchaguzi mkuu wa 2015 hivyo kwa kuliona hilo serikali imetoa ubani kiasi kidogo cha shilingi million 5 ili kuwafariji wafiwa ndugu jamaa na marafiki.
Waombolezaji.
Waombolezaji.
Sehemu ya akinamama waombolezaji.
Sehemu ya akinamama waombolezaji.
Akinamama wakimtuliza dada wa marehemu wakati wa maombolezo.
Huzuni na simanzi vimetawala nyumbani hapa kumpoteza kipenzi cha watu Ally Yanga.
 Awali akisoma wasifu wa marehemu, msemaji wa familia Ali Mwetela amesema marehemu alizaliwa mnamo mwaka 1984 mkoani shinyanga na kupata elimu yake ya msingi kasomea shule ya msingi Mapinduzi hakufanikiwa kuwa na familia.
Mwakilishi wa TFF mkoa wa Shinyanga.


Viongozi, jeshi la polisi, magereza, wapenzi na mashabiki wa soka wamejitokeza hapa kushiriki ibada hatimaye mazishi ya marehemu Ally Yanga.

Mwili wa marehemu ulitolewa ndani ulikohifadhiwa.
Akinamama wakimtuliza dada wa marehemu wakati wa maombolezo.
Mama wa marehemu shabiki  ya Yanga Africans  Ally Said almaarufu Ally Yanga (mwenye kanga ya blue katikati)
Safari ya mwisho ya aliyekuwa shabiki  kindakindaki wa Dar es salaam Yanga Africans  marehemu Ally Said almaarufu Ally Yanga ambaye amezikwa leo kwenye makaburi ya Nguzo nane mkoani Shinyanga.