ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 3, 2017

WATOTO 15 WAMEKUFA BAADA YA CHANJO YA SURUA KWENDA MRAMA SUDANI YA KUSINI.

Watoto 15 wamepoteza maisha Sudan Kusini baada ya kampeni ya chanjo ya surua ya tarehe 10 hadi 14 Mei kwenda mrama.

Shirika la Afya Duniani WHO limesema limesikitishwa na taarifa ya vifo vya watoto 15 katika kijiji cha Nachodokopele Mashariki mwa Kapwete nchini Sudan Kusini, vinavyohusiana na kampeni ya chanjo ya surua ya tarehe 10 hadi 14 Mei kwenda mrama.
Kwa mujibu wa taarifa ya pamoja iliyotolewa Alhamisi na WHO, Shirika la Kuhudumia watoto UNICEF na Wizara ya Afya ya Sudan Kusini ,baada ya uchunguzi wa kina wa vifo hivyo imebainika kwamba kampeni hiyo ya chanjo ilihusika na vifo vya watoto hao. Tariki Jasarevic msemaji wa WHO amebaini kuwa makosa ya kibinadamu yamechangia vifo hivyo.
Mtoto akichanjwa.
Amesema sababu kuu vifo hivyo ni kutumiwa wahudumu wasio na ujuzi ambao hawakupata mafunzo ya jinsi ya kutoa chanjo kwa viwango vinavyotakiwa na kutofuatiliwa na kusimamiwa ipasavyo utoaji chanjo hiyo.
Ameongeza kuwa bomba moja la sindano lilitumika kutoa chanjo kwa siku zote nne badala ya kutupwa baada ya kutumika mara moja jambo ambalo ni kinyume na viwango vya afya na usalama vya WHO, na kusababisha dawa ya chanjo kuchanganyika na vitu visivyotakiwa na kuwadhuru watoto hao.

PART ONE:- BONANZA LA KIPINDI CHA MICHEZO JEMBE FM 'SPORTS RIPOTI' LILIVYOAMSHA JIJI LA MWANZA.

Kikosi cha Jembe Fm kabla ya kushuka dimbani kupepetana na Gold Krest Fc na kutolewa katika mchezo wa mtoano baada ya kunyukwa bao 3-1 Katika dimba la Nyamagana jijini Mwanza, Bonanza la kutimiza miaka miwili ya kipindi cha 'SPORTS RIPOTI' ya Radio Jembe Fm.
Kikosi cha Gold Krest Fc Katika dimba la Nyamagana jijini Mwanza, Bonanza la kutimiza miaka miwili ya kipindi cha 'SPORTS RIPOTI' ya Radio Jembe Fm.
Kikosi cha Mkolani Fc.
Kikosi cha Bodaboda Fc.
Mtafutano.
Mashambulizi.....dah....dah....dah
Mtangazaji wa Sport Ripoti ya Jembe Fm Vanessa akitimbwirika na ratiba ndaniya Bonanza.
Mkolani baada ya kuwaondosha Bodaboda.
Moja kati ya mitanange iliyokuwa na ushindani wa kweli ni kati ya Mkolani dhini ya Bodaboda kuwania ubingwa wa Sports Ripoti Bonanza Cup 2017.
Kasi,ufundi na umakini vilitawala.
Mtu na mtu......
Moja kati ya vinogezho ilikuwa ni burudani kutoka kwa meza ya Jembe DJz wakuitwa Deejay Kflip hapa akifanya yake.
Mmoja wa wachezaji toka Mkolani Veteran akitafuta mbinu za kuwatoka wachezaji wa Mwana All Star Veteran.
Hapiti mtu....
Aksante Mwanza kuitikia katika Bonanza la Sports Ripoti ya Jembe Fm.
Ukisikia kuuzwa ndiyo huku.
Mkurugenzi wa Jembe Media Group Dr. Sebastian Ndege (kushoto) akifuatilia mchezo pamoja na Mgeni Rasmi
Tigo walishiriki vyema katika Sports Ripoti kuadhimisha miaka miwili, sherehe zilizofanyika uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza na kufana.
Wakali wa 'Town' Mjengoni Fc katika picha kabla ya mchezo wao wa nusu fainali dhidi ya Tigo.
Tigo Fc walipata bao kunako dakika za awali tu za mchezo, hata hivyo Mjengoni Fc walifanikiwa kurudisha goli hilo na mchezo kwenda kwenye hatua za matuta.
Mtu na mtu........

MAKAMBA AFUNGUA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA BUTIAMA

Live Updates kupitia 93.7 @jembefm kutoka Butiama maadhimisho ya Siku ya Mazingira yanaendelea hapa kwenye Ukumbi wa Roman Catholic Mwitongo karibu na Familia ya #MwalimuNyerere Waziri @jmakamba2015 ndiye amefungua Rasmi Maadhimisho aya, @mansourjumanne yupo kukujuza kila kinachoendelea

CHINI YA KAULI MBIU #Tanzaniabilamkaainawezekana CC:- @mbabavc @jembenijembe @harith_jaha @mzairebokilo_93.7jembefm @bobwhite_pamba @mkuryamstarabu

MAMIA WACHANGAMKIA OFA YA KUINGIA HIFADHINI BURE.

ARUSHA. Mamia ya watu wamejitoza kutembelea Hifadhi ya Manyara na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kutokana na ofa ya kuingia bure hifadhini, iliyotolewa na Serikali.

 Baadhi ya wananchi waliojitokeza kutembelea hifadhi hizo jana (Jumamosi), wameipongeza Serikali kwa ofa hiyo iliyowawezesha kushuhudia vivutio vya utalii.

 Cecilia Magandila, mkazi wa Mto wa Mbu wilayani Monduli, amesema ameshuhudia vivutio vingi katika hifadhi ya Manyara ambavyo hakuwahi kuviona.


“Nimeona wanyama, chemchem za maji ya moto na mazingira mazuri ambayo sikuwahi kuyaona,” amesema.


 Mpishi mkuu wa hoteli ya Serena Manyara, Gervas Mhina na wafanyakazi wenzake kwa nyakati tofauti wakiwa katika lango la kuingia Hifadhi ya Ngorongoro na Serengeti wamesema uamuzi wa Serikali utasaidia kuwafanya Watanzania kupenda uhifadhi.

 
 Mhina amesema ni jambo la aibu kwa watalii kutoka Ulaya kuja kutembelea hifadhi na Watanzania hata wanaoishi jirani, hawajawahi kuingia hifadhini kushuhudia vivutio vya utalii.

 Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Manyara, Dk Noelia Myonga amesema kumekuwa na mwitikio mkubwa ambao kwa siku mbili zaidi ya Watanzania 300 wametembelea hifadhi hiyo.


Myonga amesema kujitokeza kwa watu hao kutasaidia kujua umuhimu wa kutunza mazingira na kutembelea vivutio vya utalii.


 Ofisa wa Idara ya Uhusiano ya Hifadhi ya Ngorongoro, Nickson Nyange amesema zaidi ya watalii 400 wametembelea hifadhi hiyo kwa siku mbili na hifadhi imeandaa waongoza watalii kusaidia wanaofika.


Nyange ametoa wito kwa Watanzania kutumia fursa ya ofa ya bure kutembelea hifadhi za Taifa ili kuona umuhimu wa kutunza mazingira na kujionea vivutio vya utalii

JPM ATEUA MWINGINE KUTOKA ACT - Wazalendo KUWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO.

 Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mgombea Urais kwa tiketi ya chama cha Act - Wazalendo, Bibi Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Thursday, June 1, 2017

MWILI WA SHABIKI WA SIMBA SHOSE FIDELIS WAAGWA LEO DAR



















Na Abog: JEMBE FM
Mashabiki na viongozi  wa klabu ya Simba leo wameungana na wanafamilia wa aliyekuwa shabiki kindakindaki wa klabu hiyo Shose Fidelis Masao, kuuaga mwili wake kwenye Ibada iliyofanyika majira ya Saba hadi saa Tisa mchana, kwenye kanisa la Roman Catholic Magomeni jijini Dar es salaam.

Shose alifariki kwa ajali ya gari Mei 29, eneo la Dumira mkoani Morogoro alipokuwa akitokea Dodoma kuishabikia klabu hiyo kwenye mchezo wa fainali ya kombe la shirikisho. Katika gari hilo alikuwa na kiungo na nahodha wa Simba Jonas Mkude ambaye alinusurika pamoja na wengine wawili.

Rais wa klabu ya Simba Evans Aveva amesema klabu itamuenzi shabiki huyo na watamkumbuka daima kwani msiba wake umewagusa wanasimba wote pamoja na jamii ya wapenda soka wote Tanzania.

Marehemu Shose alizaliwa 1988, Ilala, Dar es salaam na mwili wake utasafirishwa kwenda mkoani Kilimanjaro kwa mazishi. Bwana ametoa na Bwana ametwaa, Jina lake lihimidiwe. Amen.

KAMANDA MWANDAMIZI WA AL-SHABAAB AJISALIMISHA KWA SERIKALI SOMALIA.

Kamanda mmoja mwandamizi wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab amejisalimisha kwa jeshi la taifa la Somalia.

Kamanda mkuu wa jeshi la Somalia, Jenerali Ahmed Mohamed Tredishe amesema mwanachama huyo wa al-Shabaab anayejulikana kwa jina Bishar Mumin Afrah amejisalimisha kwa jeshi hilo katika mji Buloburte eneo la Hiran, yapata kilomita 200 kaskazini mwa Mogadishu, mji mkuu wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
Inaarifiwa kuwa, kamanda huyo mwandamizi wa genge la kigaidi la al-Shabaab amejisalimisha kwa vyombo vya usalama sambamba na kukabidhi bunduki mbili aina ya AK47 na shehena ya risasi.
Hivi karibuni Rais wa Somalia, Mohamed Abdullahi Farmajo alitoa msamaha wa siku 60 kwa wanamgambo wa al-Shabaab ambao wataweka silaha chini na kujisalimisha kwa serikali.
Rais Mohamed Abdullahi Farmajo wa Somalia.

Mapema mwezi uliopita wa Mei, Wizara ya Habari ya Somalia ilisema kuwa, Moalim Osman Abdi Badil, kamanda wa ngazi za juu wa al-Shabaab pamoja na wanamgambo wengine watatu wa genge hilo waliuawa katika mapigano na jeshi la Somalia kwenye eneo la Shabelle ya Chini.
Katika hatua nyingine, walimu wawili wa Kenya wameripotiwa kutekwa nyara na wanamgambo wa al-Shabaab katika mji wa Fafi kaunti ya Garissa usiku wa kumkia leo baada ya magaidi hao kuteketeza moto shule moja katika eneo hilo la kaskazini mashariki. Kadhalika magaidi hao wameng'oa na kuiba mlingoti wa mawasiliano ya simu ya mkononi (rununu) katika eneo hilo.

Ripoti: WANAJESHI WA ISRAEL WAMEUA WATOTO ELFU 3 WA KIPALESTINA.

Wizara ya Habari ya Palestina imesema, watoto zaidi ya elfu tatu wa Kipalestina wameuliwa na jeshi katili la Israel tangu ilipoanza Intifadha ya Pili mwezi Septemba 2000.

Kwa mujibu wa ripoti iliyochapishwa leo na wizara hiyo kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya Kuwalinda Watoto ambayo huadhimishwa Juni Mosi kila mwaka kote duniani, mbali na watoto elfu tatu kuuawa, wengine zaidi ya 13 elfu wamejeruhiwa na wanajeshi hao.
Ripoti hiyo imebainisha kuwa, watoto wasiopungua 72 wameuliwa na askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel tangu mwezi Oktoba 2015, wakati ilipoanza Intifadha ya Tatu ya Quds.
Wizara ya Habari ya Palestina imefichua kuwa, mtoto mdogo zaidi aliyeuliwa shahidi na wanajeshi wa Israel ni Ramadan Mohammad Faisal Thawabta, aliyekuwa na miezi minane tu, ambaye alifariki dunia Oktoba 30, 2015 baada ya kuvuta gesi ya kutoa machozi iliyofyatuliwa na wanajeshi Wazayuni katika maandamano yaliyofanyika mjini Beitul Fajjar, kusini mwa Beitul Lahm.
Watoto wa Kipalestina katika jela za Israel.
Kadhalika ripoti hiyo ya Wizara ya Habari ya Palestina imebainisha kuwa, watoto zaidi ya 12 elfu wa Kipalestina wametekwa nyara na askari wa Israel na kuzuiliwa chini ya mazingira magumu, katika kipindi cha miaka 17 iliyopita.
Kwa mujibu wa shirika la kutetea haki za wafungwa wa Palestina la Addameer, wanajeshi katili wa Israel wamewahukumu vifungo jela watoto 300 wa Kipalestina tangu mwezi Aprili mwaka huu hadi sasa, vikiwemo vifungo vya hadi miaka 20 jela.