ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 27, 2017

MSUMENO WA KICHUYA WAI-CHANACHANA MBAO


Makali ya msumeno wa Shiza Kichuya jioni ya leo ndiyo yamefanikiwa 'kuzichana chana' mbao za Mbao FC toka Mwanza na hata kuipa Simba ubingwa wa Azam Federation Cuf katika dimba la Jamhuri mjini Dodoma.

Wakati timu hizo zikiwa sare ya 1-1 hadi dakika ya 118, Simba ikapata penati baada ya beki mmoja wa Mbao Fc kuunawa mpira katika harakati za kuokoa mpira usitinge nyavuni.

Kichuya alipiga penati hiyo kiufundi akimwacha mlinda mlango wa Mbao Fc akienda kushoto naye akiutupia kulia.

Kiungo wa Simba, James Kotei amekuwa mchezaji bora wa mechi ya fainali ya Kombe la Shirikisho. Katika mechi hiyo, Simba imeshinda kwa mabao 2-1 na kubeba ubingwa. Kotei alicheza namba nne na kuonyesha kiwango cha juu kabisa katika mchezo huo.

Friday, May 26, 2017

BREAKING NEWS:- MZEE CHIFUPA AFARIKI DUNIA.

Mzee Chifupa ambaye ni baba  wa marehemu Amina Chifupa wa Mpakanjia amefariki dunia muda mfupi uliopita......Taarifa zaidi tutawapenyezea hapa kupitia Blogu hii. RIP

• MWANAMUME AMUUA MKEWE KWA KUMPIGA RISASI NA YEYE MWENYEWE KUJIUA KWA KUJIPIGA RISASI WILAYANI NYAMAGANA.

MAUAJI MWANZA: Mume adaiwa kumuua mke wake kwa kumpiga risasi na yeye kujiua kwa risasi usiku wa kuamkia leo huko Mahina jijini Mwanza, polisi yathibitisha. 

Tayari Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na hii hapa taarifa kamili. BOFYA VIDEO KUIPATA TAARIFA KAMILI.

Mwanza. Mkazi wa Mahina, jijini Mwanza, aliyefahamika kwa jina moja la Max, anadaiwa kumuua mke wake, Teddy Malulu kwa kumpiga risasi usiku wa kuamkia leo. 

Baada ya kufanya mauaji hayo, Max naye anadaiwa kujiua kwa kujipiga risasi. Mpaka sasa chanzo cha mauaji hayo hakijajulikana. 

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amethibitisha tukio hilo na kusema kuwa mwanamke anayedaiwa kuuawa na mume wake ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wavuvi Tanzania (Tafu) . 

Kamanda Msangi amesema uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea. Taarifa kamili na #video nimeiweka

FID Q, SNURA, MADEE KUTUMBUIZA TAMASHA LA TAIFA MOJA JUMAMOSI HII.

Wasanii wa kizazi kipya Fid Q, Snura, Madee, Dogo Njaja, Stamina na Navy Konzo wanatarajia kutoa burundani katika matamasha ya Taifa Moja ambayo yatafanyika kesho (Jumamosi) kwenye mikoa mine tofauti hapa nchi. 
Burandani hio itaenda sambasamba na kutoa elimu kwa Wananchi wa mikoa husika juu ya uhuru wa kutuma pesa bila mipaka ambayo ni ushirikiano wa makampuni matatu ya simu za mkononi kupitiia huduma zao Tigo Pesa, Airtel Money na Ezy Pesa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Liginiku Milinga ambaye ni Mkurugenzi wa kampuni ya Fern Tanzania ambao ndio waratibu na waandaaji wa matamasha hayo alisema wasanii wote washathibitisha kushiriki kwao kwenye matamasha hayo na kwamba maandalizi yote yamekamilika huku akiwaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi kupata burundani toka kwa wasanii wakali hapa nchini na pia kupata elimu juu ya kutuma na kupokea pesa kwenda mtandao wowote hapa Tanzania kwa gharama ile ile.

Wasanii Stamina na Fid Q watambuiza kwenye tamasha litakalofanyika kwenye uwanja wa Mwembetongwa mjini Iringa wakati Dogo janja na Baba Levo wakifanya ya kwao kwenye uwanja wa Community Center grounds uliopo mjini Kigoma huku Snura na Madee wakiwashika vilivyo wakazi wa mji wa Tanga kwenye uwanja wa Tangamano. Navy Kenzo huku akitamba na wimbo wake wa kamati ya chini, atakuwa kwenye uwanja wa shule ya msingi ya Sabasaba iliyopo mjini Morogoro.

Tangu tuanze kampeni yetu ya Taifa Moja tumekuwa tukitumia wasanii wetu kutoa elimu kwe Wananchi kupitia burudani na tumetapata mafanikio makubwa sana ya kufikisha ujumbe wetu wa uhuru wa kutuma pesa bila mipaka kupitia burudani kwa Watanzani. Naomba nitoe wito wangu kuwaomba Watanzania wajitokeze kwa wingi kesho kushuhudia wasanii wetu ambao wamehaidi kutoa burundani ya uhakika.

Bali na kupata burundani, Watanzania wataweza kufahamu jinsi ya kujikwamua kiuchumi kwani kwa njia ya kutuma pesa kwenda mtandao wowote ule kwa gharama ile ile imetoa urahisi kwa kuongeza watumiaji wengi wa huduma ya kutuma pesa na hivyo kuwa rahisi Wananchi kupata huduma za kifedha.


Taifa Moja ni kampeini ambayo imedhaminiwa na taasisi za Financial Sector Deepening Trust of Tanzania (FSDT) pamoja na Bill & Melinda Gates Foundation huku ikiratibiwa na International Finance Corporation (IFC) chini ya muungano ya makampuni matatu ya simu za mkononi za Airtel Tanzania, Tigo Tanzania na Zantel kupitia huduma zao za Airtel Money, Tigo Pesa na Ezy Pesa.

MZEE YUSUPH ANAKUTAKA UFUTE NYIMBO ZAKE KWENYE SIMU YAKO.

Aliyekuwa mfalme wa muziki wa taarab nchini, Mzee Yusuph amefunguka na kueleza kuwa watu wote walio na nyimbo zake kwenye simu zao wafute na kuacha kusikiliza ili kuepuka dhambi.

Katika mahojihano na kipindi cha Mitikisiko ya Pwani cha Times Fm, Mzee Yusuph ameelezea maisha yake ya ndoa, kidini na kiuchmi yalivyo kwa sasa ukilinganisha na hapo awali.

“Mimi nikikubali watu wacheze nyimbo zangu ina maana nimeruhusu dhambi tena ni bora nirudi kuimba muziki tena hivyo, watu wote waliokuwa na nyimbo zangu kwenye simu zao wafute na kuacha kusikiliza kuepuka dhambi,” amesema Mzee Yussufu.

Mzee Yussufu amesema yeye hayupo kwenye kundi lake la ‘Jahazi Modern Taarab’ kama baadhi ya watu wanavyodhani na wala hafuatilii kabisa kundi hilo.

“Nilitaka kulivunja Kundi la Jahazi lakini sheria za nchi haziruhusu nikaliacha na haya niliambiwa na Basata wenyewe. Vyombo vya bendi ya Jahazi havikuwa vya kwangu tulikuwa tunasaidiana na mabosi,” amesema.

Katika hatua nyingine Mzee Yusuph amesema maisha ya kiuchumi kwa sasa ni toufauti na kipindi alichokuwa anafanya muziki kwani hapo awali kwa wiki alikuwa anaweza kutengeneza milioni moja na nusu mpaka mbili ila sasa kushika laki tano au milioni inaweza kumchukua miezi miwili.

Ameongeza kuwa wake zake wanne bado anaendelea kuishi nao kama kawaida, na kuwa na wake ni jambo ambalo amehimizwa na sio amri, na kwa sasa wanamjua ni mtu wa namna gani na mambo yote yanaenda sawa hakuna hata mmoja anayefanya sivyo.

Thursday, May 25, 2017

TETEMEKO LAUWA ASKARI MMOJA MKOANI MWANZA NA WAWILI KUPOTEZA FAHAMU

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi,


Tetemeko laua Mwanza
May 25, 2017

Tetemeko la ardhi lililotokea leo majira ya saa 6 na dakika 55 mchana mkoani Mwanza na kudumu kwa sekunde kama 30 hivi linadaiwa kusababisha kifo cha askari polisi kilichotokea wilayani Misungwi mkoani Mwanza. 

Akithiibisha kifo hicho Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amesema askari huyo amepatwa  na mkasa huo wakati akifanya mahojiano na mahabusu.
BOFYA PLAY KUMSIKILIZA KAMANDA.

Marehemu askari Joyce  Mwalingo.
Aidha Kamanda Msangi amesema askari mwingine na mahabusu walipoteza fahamu na kupelekwa hospitali baada ya kupata taarifa za kufariki dunia kwa askari Joyce  Mwalingo.


Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi anawataka wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya mabadiliko ya hali ya hewa pamoja na hali yeyote ya dharura itakayojitokeza. BOFYA PLAY KUSIKILIZA MASHUHUDA WA MAENEO MENGINE JIJINI MWANZA.


Hili ni tetemeko la tatu kutokea mkoani Mwanza  katika kipindi kisichozidi mwaka mmoja ambapo, Tetemeko la kwanza lilitokea septemba 5 mwaka jana likiwa na ukubwa wa 5.7. na tetemeko la pili lilitokea Aprili 30 mwaka huu.

WACHIMBAJI WADOGO WA4 WAFA HUKU WA3 WAKIJERUHIWA GEITA.

Geita.Wachimbaji wadogo wanne wamekufa baada ya kufukiwa na kifusi katika machimbo madogo ya nyamalimbe yaliyopo wilayani Geita mkoani hapa.

Watu saba walifukiwa ambapo kati yao watatu wameokolewa na wamelazwa katika Kituo cha Afya Katoro.

Tukio hilo limetokea  saa mbili asubuhi. Mkuu wa Wilaya ya Geita Herman Kapufi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

HIVI NDIVYO WALIVYOPOKELEWA SERENGETI BOYS.


















SERENGETI BOYS YAPOKELEWA NA WAZIRI MWAKYEMBE
Na Abog. JEMBE FM
Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 imetua leo nchini baada ya kuondolewa kwenye michuano ya AFCON U17 nchini Gabon na kupokelewa na waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Harrison Mwakyembe kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es salaam.

Msafara wa timu hiyo ulikuwa chini ya mjumbe wa kamati ya Utendaji ya TFF Ayoub Nyenzi pamoja na benchi lote la ufundi likiongozwa na kocha mkuu Bakari Shime maarufu Mchawi Mweusi.

Gsengo Blog ilifika uwanjani hapo na kukukusanyia picha za matukio yote katika mapokezi hayo kama zinavyoonekana hapo chini.

MAAMUZI MAKUBWA, MATOKEO MAKUBWA



Napenda kuungana na mamilioni ya Watanzania kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Joseph Magufuli kwa uzalendo na mapenzi ya dhati anayoonyesha kivitendo kwa Wananchi na Taifa kwa ujumla kwa kuhakikisha analinda rasilimali, Mali, haki na maslahi.

Hivi karibuni Rais Magufuli alizuia makontena 277 yenye mchanga wa madini kusafirishwa kwenda nje ya nchi na kuunda kamati kuchunguza hasara au faida tuliyokuwa tukiipata Watanzania kutokana na kusafirisha mchanga huo ambapo kamati imewasilisha taarifa ya awali imeonyesha thamani ya makontena hayo 277 ni Tsh. Bilioni 112.1 kumbe thamani halisi ni Tsh. Trilioni 1.44. Taarifa hiyo imeonyesha hayo makontena tu tulikuwa tumepoteza zaidi ya Tsh. Bilioni 829.4 ambapo kwa mwaka mmoja tu tulikuwa tukipoteza Trilioni 25 ambayo Serikali ilikuwa haipati hata senti moja.  

Kupitia mchanga huo tu tulikuwa tukiibiwa hivyo kwa takribani miaka 18 huku tukipoteza Tsh. Trilioni 829.4 sawa na bajeti ya miaka 26 ya Tsh  Trilioni 32 kwa kila mwaka.

Tunapoteza pesa hizo huku tukiangalia mahospitali hayana madawa, miundombinu mibovu, mishahara haikidhi, tunakopa kukamilisha bajeti ya nchi maumivu ambayo hatukustahili kabisa kuyapata sisi Watanzania.

Ahsante sana Rais Magufuli kwa kuonyesha uzalendo wa kuzuia unyonyaji na uhujumu uchumi huu wa kikatili uliokuwa ukiendelea nchini. Ni viongozi wachache sana Afrika waliosalia wenye kariba ya uzalendo kama alionao Rais Magufuli.

Huu ni mwendelezo wa uzalendo wa kivitendo unaoonyesha na Rais Magufuli. Tukumbuke ni Rais Magufuli huyu huyu anasimamia vyema upotevu wa mapato bandarini, kuzuia matumizi ya ovyo Serikalini ya kodi za Wananchi kwa kufuta safari za nje, kulipana posho zisizo na tija na kupunguza matumizi ya kawaida kwa kuongeza fedha zaidi kwenye matumizi ya kimaendeleo.

Kiukweli ninaiona Tanzania mpya ikijengwa na uzalendo alionao Rais Magufuli kwa Watanzania na Taifa kwa ujumla. Watendaji, viongozi na Wananchi yatupasa tuige Uzalendo wa Rais wetu mpendwa Dk. John Pombe Magufuli kwa kuungana nae kupambana na wahujumu uchumi wa nchi yetu.

Rais Magufuli fanya uliyotumwa na wanyonge usiogope wanaojiita wachambuzi ambao kila kitu hukuchambua kinyume, hao ni changamoto ya wewe kusonga mbele!

Tunakuombea Rais Magufuli ulinzi, Baraka, hekima na busara zaidi toka kwa Mwenyezi Mungu.

Mungu Ibariki Tanzania
Mungu mbariki Rais wetu Dk. Magufuli.

Na Emmanuel J. Shilatu
25/05/2017
0767488622

PICHA TUZO ZA VPL 2016/17

















ZIMBWE JR, MSUVA KICHUYA NA MEXIME WANG’AA TUZO ZA VPL 16/17.
Na Abog JEMBE FM.
Usiku wa kuamkia leo zimetolewa tuzo na zawadi kwa washindi wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara VPL katika sherehe zilizofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City.

Katika tuzo hizo, mlinzi wa kushoto wa Simba Mohamed Hussein maarufu Zimbwe Jr ameibuka mchezaji bora wa ligi kuu msimu wa 2016/17. Mabingwa wa ligi klabu ya Yanga wamekabidhiwa zawadi yao ambayo ni Tsh. Milioni 84, huku washindi wa pili,tatu na nne wakipewa zawadi zao ambao ni Simba, Azam na Kagera Sugar.

Simon Msuva na Abdulrahman Mussa pia wamekabidhiwa zawadi yao ya ufungaji bora. Tuzo ya kocha bora imechukuliwa na kocha wa Kagera Sugar Meck Mexime huku mshambuliaji wa klabu hiyo Mbaraka Yusuph akiibuka mchezaji bora chipukizi.

Golikipa bora ni Aishi Manula wa Azam huku Shiza Kichuya akitwaa tuzo ya goli bora alilofunga dhidi ya Yanga kwenye mechi ya mzunguko wa kwanza. Tuzo nyingine ni ile ya mchezaji bora wa kigeni ambayo imetua kwa kiungo wa Yanga Haruna Niyonzima, huku tuzo ya heshima ikitua kwa Kitwana Manara.