ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 17, 2017

WATU 3 WAUAWA, POLISI KENYA WAKIZUIA MSAFARA WA KUMPOKEA RAILA ODINGA UWANJA WA JOMO KENYATTA AKITOKEA NJE YA NCHII.


Polisi wa Kenya wakifyatua risasi dhidi ya wapinzani wa serikali;

 

Gladys Wanga amewapa ruksa polisi kumfyatulia risasi, iwe isiwe atasonga kuingia uwanjani kumpokea Raila.

Jeshi Kenya laua waandamanaji watatu, magari kadhaa yachomwa, Raila arejea nchini

Watu watatu wameuawa hii leo wakati jeshi la polisi la Kenya lilipojaribu kutawanya waandamanaji waliokusanyika kupokea msafara wa kiongozi wa upinzani, Raila Odinga aliyerejea nchini mapema leo akitokea nje ya nchi.


Polisi ya Kenya imetumia gesi ya kutoa machozi na kufyatua risasi angani dhidi ya wafuasi wa Odinga waliokuwa katika barabara inayotoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta wakielekea mjini kati jijini Nairobi.


Waandamanaji wawili wameuawa katika mapigano yaliyotokea baina yao na polisi waliokuwa wakitaka kuzua waandamanaji hao kuingia katika maeneo ya kibiashara mjini Nairobi. 

Ripo zinasema magari kadhaa yameteketezwa kwa moto katika ghasia na machafuko hayo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.