ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, September 7, 2017

TANZIA: KAMISHNA MSTAAFU WA OPERESHENI WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI AFARIKI DUNIA MAPEMA LEO JIJINI DAR ES SALAAM.


Kamishna   Jenerali wa Jeshi   la   Zimamoto   na Uokoaji Nchini   – Thobias  Andengenye   anasikitika   kutangaza   kifo   cha   aliyekuwa Kamishna   wa   Operesheni   Mstaafu   wa   Jeshi   la   Zimamoto   na Uokoaji CF (OPS) Rogatius Peter Kipali, kilichotokea mapema leo Semptemba 7, 2017 akiwa nyumbani kwake Mombasa, Ukonga jijini Dar es Salaam.


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji anatoa pole kwa Maafisa, Askari na Watumishi wote wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Nchini, familia ya Marehemu na wale wote walioguswa na msiba huu kwa namna tofauti tofauti.


Jeshi   la   Zimamoto   na   Uokoaji   kwa   kushirikiana   na   familia   ya Marehemu linaendelea kuratibu shughuli za msiba huo na taarifa za Mazishi zitatolewa baadaye baada ya taratibu zote kukamilika.


Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi Amina.


IMEANDALIWA NA KITENGO CHA HABARI NA ELIMU KWA UMMA-JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.