ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 9, 2017

WASHUKIWA WALIOJIUNGA NA BOKO HARAM WACHUNGUZWA.

Jeshi la Nigeria linawachunguza watu wanaoshukiwa kujiunga na kundi la kigaidi la Boko Haram nchini humo. 

Lucky Irabor, Kamanda wa oparesheni iliyopewa jina la "Lafiya Dole" huko kaskazini mashariki mwa Nigeria amesema kuwa, baadhi ya wafungwa wanaoshukiwa kuwa wanachama wa kundi la kigaidi la Boko Haram hivi karibuni watafikishwa mahakamani. Irabor ameongeza kuwa, aghalabu ya waliotiwa mbaroni katika upekuzi uliofanywa na jeshi la Nigeria wamekiri kushiriki katika mashambulizi ya kundi la kigaidi la Boko Haram.

Lucky Ilabor, Kamanda wa Oparesheni dhidi ya Boko Haram kwa jina la Lafiya Dole.
 
Hadi kufikia sasa watu wasiopungua elfu 20 wameuliwa na wengine zaidi ya milioni mbili na laki sita wamekimbia makazi yao tangu kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram lianzishe mashambulizi na ukatili wake huko kaskazini mashariki mwa Nigeria mwaka 2009. Aidha mashambulizi ya kundi hilo la kitakifiri yameenea huko Chad, Niger na Cameroon kuanzia mwaka 2015.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.