ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 17, 2017

SIKU YA MTOTO WA AFRICA JIJINI MWANZA.

Na Zephania Mandia tarehe 16.06.2017
Jamii imetakiwa kujifunza kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kutokomeza vitendo vya ukatili dhidi ya watoto ili kuhakikisha haki za watoto zinalindwa. 


Wito huo umetolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishana wa Polisi Ahmed Msangi katika maadhimisho ya mtoto wa afrika mkoani Mwz.


Kutengana kwa wanandoa na ukatili dhidi ya watoto kunatajwa kuwa chanzo kikubwa cha watoto kutoroka majumbani na hatimaye kushia mitaani na wengine kuathirika kisaikolojia na hivyo kusababisha kushuka kwa taaluma.


Watoto wanaokulia mtaani wanatajwa kuwa wathirika wakubwa wa vitendo vya kikatili ikiwemo ubakaji na ulawiti. Mwenyekiti wa madereva kanda ya ziwa DEDE PETRO ni miongoni mwa watu waliokulia katika mazingira ya mtaani.


Jeshi la polisi limewataka wananchi kutumia madawati ya jinsia yaliyopo  kwenye vituo vya polisi kukomesha vitendo vya kikatili dhidi ya watoto.


Utumikishaji watoto, Mimba za utotoni,ubakaji na ulawiti kwa watoto imeelezwa kuwa miongoni mwa changamoto zinazoikabili jamii kutokana na  kutotoa ushirikiano kwa jeshi la polisi na wananchi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.