ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 10, 2017

ETHIOPIA KUISHIWA NA CHAKULA CHA MISAADA.

Serikali ya Ethiopia na makundi ya misaada ya kibinadamu yametangaza kuwa, nchi hiyo itaishiwa na chakula cha misaada kwa ajili ya watu milioni 7.8 walioathiriwa na ukame mkubwa hadi kufikia mwishoni mwa mwezi huu.
 
Wahisani, mashirika ya kimataifa ya misaada ya kibinadamu na serikali ya Ethiopia wanasema kuwa, chakula cha msaada cha zaidi ya watu milioni 7.8 wanaosumbuliwa na ukame kitamalizika kufikia mwishoni mwa mwezi huu huku nchi hiyo ikiendelea kusumbuliwa na uhaba wa misaada ya kifedha.
Uhaba wa mvua na mabadiliko ya hali ya hewa vimesababisha ukame mkubwa nchini Ethiopia na katika nchi nyingine kadhaa za Pembe ya Afrika. Nchini Ethiopia pekee inakadiriwa kuwa, idadi ya watu walioathiriwa na njaa na uhaba wa chakula itaongezeka kwa watu milioni mbili kufikia mwezi ujao.
Ukame umeathiri sehemu kubwa ya Pembe ya Afrika
Mwezi Machi mwaka huu Umoja wa Mataifa ulitangaza kuwa, njaa iliyoyakumba maeneo ya kaskazini mashariki mwa Nigeria, Sudan Kusini, Yemen na Somalia imesababisha mgogoro mkubwa zaidi wa kibinadamu kuwahi kutokea duniani tangu mwaka 1945.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.