ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 19, 2017

WIKI YA ELIMU SENGEREMA 19/5/2017



Maadhimisho ya wiki ya  Elimu yamefanika katika halmashauri ya wilaya ya sengerema ikiwa na kauli mbiu ya (UWAJIBIKAJI KWA ELIMU BORA NA JUMUISHA )
Maadhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya Nyatukala Jeshini ikiwa na lengo la kuhamasisha wananchi katika maendeleo ya elimu .

Akizungumza na waadishi wa habari mratibu wa elimu kata ya Nyatukala mwalimu Jesca Manyanga  amesema wananchi wanatakiwa kushiriki katika swala la maendeleo ya elimu ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa na kuacha kuitegemea Serikali. 

Kwaupande wa waalimu wamesema mzazi anatakiwa kutoa ushirikiano kwa kufatilia maendeleo ya mwanafunzi. Nao wanafunzi wamesema mzazi anatakiwa kumpeleka mtoto shule ili kumpa msingi bora kwa maisha ya baadae. BOFYA PLAY KUSIKILIZA.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.