ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 18, 2017

WAKAZI WA MBAGALA WAVUTIWA NA TAMASHA LA TAIFA MOJA CONCERT.




Msanii wa Bongo Fleva Harmonize akitumbuiza wakati wa tamasha la Taifa Moja lililofanyika Jumapili ya Pasaka kwenye viwanja wa Mbagala Zakhem Jijini Dar es Salaam. Tamasha la Taifa Moja lina lengo ya kutoa elimu kwa wananchi juu ya fursa ya uhuru wa kutuma pesa bila mipaka.
Msanii wa Bongo Fleva Rich Mavoko akitumbuiza wakati wa tamasha la Taifa Moja lililofanyika Jumapili ya Pasaka kwenye viwanja wa Mbagala Zakhem Jijini Dar es Salaam. Tamasha la Taifa Moja lina lengo ya kutoa elimu kwa wananchi juu ya fursa ya uhuru wa kutuma pesa bila mipaka.
Msanii wa Hip Hop Young Killer akitumbuiza wakati wa tamasha la Taifa Moja lililofanyika Jumapili ya Pasaka kwenye viwanja wa Mbagala Zakhem Jijini Dar es Salaam. Tamasha la Taifa Moja lina lengo ya kutoa elimu kwa wananchi juu ya fursa ya uhuru wa kutuma pesa bila mipaka.


Wakazi wa maeneo ya Mbagala na viunga vyake jana jumapili walipata burundani ya aina yake iliyoongozwa na wasanii kutoka kundi la Wasafi Classic Harmonize pamoja na mwenzake Rich Mavoko. Tamasha hilo lilikuwa ni maalum kwa kutoa elimu kwa wananchi juu uhuru wa kutuma pesa bila mipaka ambao ni muungano wa makampuni matatu ya simu za mikononi kupitia huduma za Airtel Money, Togo Pesa na Ezypesa.

Mbali na wasanii hao kutoka Wasafi Classic, Young Killer ambaye ni msanii wa hip hop pia alikonga nyoyo za mashabiki wake pale aliponda jukwaani akiwa ni msanii wa mwisho katika tamasha hilo.

Akiwa na kibao chake cha matatizo, msanii Harmonize alikuwa akilalizimiki kurudia kila wimbo alikuwa akiimba kwa mara tatu kutokana na maombi ya mashabiki ambao walikuwa wamejikoteza kwa wingi.

Akiongea kwenye tamasha hilo Liginiku Milinga ambaye ni Mkurugenzi wa kampuni ya Fern Tanzania ambao ndio walikuwa waratibu na waandaaji wa tamasha hilo alisema kutokana na wingi wa mashabiki waliojitokeza, elimu ya uhuru wa kutuma pesa bila mpaka kupitia kampeini ya Taifa Moja limefanikiwa.

‘Nia ya kuandaa tamasha hili ilikuwa ni kufika Watanzania wengi. Kama mnavyoona hapa kwa siku ya leo mtakubali kuwa elimu ya uhuru wa kutuma pesa bila mipaka imefanikiwa, alisema Milinga’.

Watanzania wengi wanapenda burundani, natoa shukrani za dhati kwa wakazi wote wa Dar es Salaam na sana sana Mbagala na viunga vyake kwa kujitokeza kwa wingi na kuja kushuhudia burundani hii licha ya kuwa na hali ya mvua, aliongeza Milinga.

Milinga aliongeza kuwa kampeini ya Taifa Moja itaendelea nchi nzima kwa matamasha mbali mbali hili kuwafikia Watanzania na kuweza kujikomboa kiuchumi kwa kutumia vyema fursa ya uhuru wa kutuma pesa bila mipaka tofauti na hapo zamani ambapo kulikuwa na changamoto nyingi pale mtumiaji wa mtandao mmoja alikuwa anatuma pesa kwenda kwenye mtandao tofauti.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.