ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 11, 2017

*MASHABIKI WA SIMBA WASHUTUMIWA KWA UHARIBIFU UWANJA WA CCM KIRUMBA MECHI DHIDI YA MBAO FC TAREHE 10.04.2017*

*TAARIFA YA UHARIBIFU WA UWANJA WA CCM KIRUMBA KWENYE MECHI YA MBAO FC VS SIMBA SC TAREHE 10.04.2017*

Uongozi wa Uwanja wa CCM Kirumba, kupitia Meneja wa Uwanja Ndg *Steven E. Shija* unapenda kutoa taarifa za uharibifu wa Uwanja.

Mechi iliyochezwa Tarehe 10.04.2017, kwenye Uwanja wa CCM Kirumba kati ya Mbao Fc Vs Simba Sc umesababisha uharibifu Mkubwa kwenye Maeneo ya kuingilia Wachezaji, Waamuzi na Geti Namba 4 ambapo walikuwa wamekaa Mashabiki wa Simba

Uharibifu huo umetokana na Mashabiki wa Timu ya Simba Sc kupanda Juu ya maeneo ya Kivuli yaliyojengwa kwenye maeneo yaliyotajwa ( Vyumba vya Kubadirishia Nguo kwa wachezaji, Waamuzi na Geti namba Nne), uharibifu huo umepelekea kushindwa kufunga Milango ya Mbele ambapo ni hatari kwa usalama wa maeneo hayo muhimu

Hivyo uongozi wa Uwanja umeishazitaarifu Mamlaka husika ili zichukue hatua kwa Wanaohusika ili kuhakikisha eneo hilo linatengenezwa mapema kabla ya Mechi ya Toto African Vs Simba Sc Tarehe 15.04.2017


*Imetolewa:-*
*Uongozi wa Uwanja wa CCM Kirumba - Mwanza*
*11.04.2017*

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.