ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 25, 2017

UN YAANZISHA KAMPENI MPYA YA KUTOKOMEZA POLIO AFRIKA.


Kampeni hiyo ambayo itafanywa kwa wakati mmoja na wahudumu wa kujitolea 190,000 kwa kutembea kwa miguu, baiskeli na njia zingine zozote, ni katika harakati za kuutokomeza kabisa ugonjwa huo katika nchi zilizobakiwa na waathirika wa ugonjwa huo ambao WHO inasema bado ni tishio kubwa kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka mitano.
Mashirika hayo yamesema mapigano katika jimbo la Borno nchini Nigeria yalisababisha watoto wanne kupooza mwaka 2016 kutokana na ukosefu wa chanjo, eneo pekee ambalo kirusi cha Polio bado kinatishia maisha, na iwapo hakitashughulikiwa haraka, eneo hilo na maeneo yaliyo jirani yatakuwa hatarini kuambukizwa. Jimbo la Borno ni ngome ya kundi la kigaidi la magaidi wakufurishaji wa Boko Haram.

Mtoto aliyepooza kutokana na polio
Ili kufanikisha kampeni hiyo, mashirika hayo yamesema ushirikiano wa serikali kuu hadi za mashinani unahitajika ili kuweza kumfikia kila mtoto.
Nchi hizo 13 ni Benin, Cameroon, Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, Chad, Côte d'Ivoire, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Guinea, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Nigeria na Sierra Leone.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.