ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 24, 2017

LIVE: Hafla ya Kuapishwa kwa Mawaziri Wapya, Dk Mwakyembe na Kabudi

Rais Magufuli, leo anawaapisha mawaziri wawili aliowateua siku chache zilizopita. Rais Magufuli amefanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mawaziri na kumteua waziri mpya wa habari na michezo. Dkt. Magufuli amemteua Dkt. Harrison George Mwakyembe kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Nape Moses Nnauye ndiye aliyekuwa anashikilia wadhifa huo.

Aidha, Dkt Magufuli amemteua Prof Palamagamba Aidan John Mwaluko Kabudi kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.


Mawaziri hao wanaapishwa Ikulu ya Magogoni, jijini Dar es Salaam
Bw Nauye amevuliwa majukumu yake siku moja baada yake kupokea ripoti ya kamati ya uchunguzi kuhusu uvamizi uliotekelezwa na mtu anayedaiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda katika studio za kituo cha habari cha kibinafsi cha Clouds mwishoni mwa wiki.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.