ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 18, 2017

ARSENAL YABAMIZWA 3-1 NA WEST BROMWICH, HOFU YATANDA KAMA WATACHOMOZA TOP 4.

 
 Craig Dawson akiwa hewani juu ya Nahodha wa Arsenal, Laurent Koscielny kuifungia West Bromwich Albion bao la kwanza dakika ya 12 katika ushindi wa 3-1 dhidi ya timu ya kocha Mfaransa, Arsene Wenger katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jioni ya leo Uwanja wa The Hawthorns. 

Dawson alifunga mabao mawili na la tatu dakika ya 75, huku la pili la West Bromwich likifungwa na Hal Robson-Kanu dakika ya 55 na la kufutia machozi la Washika Bunduki wa London, likifungwa na Alexis Sanchez dakika ya 15 

 Alexis Sanchez mpachika mabao wa klabu ya Arsenal's akionekana kuchoka mara baada ya timu yake kuelemewa.

Kwa masikitiko akiwa benchi  Alexis Sanchez mkono kichwani akisikitika mara baada ya kutolewa dakika za lala salama huku timu yake ikiwa nyuma ya matokeo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.