ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 9, 2017

SHAMRASHAMRA ZA UZINDUZI WA TAMASHA LA SAUTI ZA BUSARA ZANZIBAR

Mwenyekiti wa Tamasha la Busara Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akiwa na Mabalozi wa Norway na Uswisi kulia kwa Mhe Simai ni Balozi wa Uswisi Tanzania Balozi Florence Tinguely na Balozi wa Norway Tanzania Balozi Hanne Marie wakiangalia wakiangalia vikundi vya Utamaduni wakati wa Uzinduzi wa Tamasha la Sauti za Busara katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Kisongo leo wakiangalia burudani hizo.
Wasanii wa Kikundi cha Utamaduni kutoka Nchini Burundi wakitowa burudani kwa Wananchi wa Zanzibar katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Zanzibar kabla ya kuaza kwa maandamano ya Uzinduzi huo yalioazia katika viwanja hivyo hadi katika viwanja vya bustani ya forodhani.
Wasanii kutoka burundi wakionesha umahiri wao wa kupiga ngoma za utamaduni wa Kwao. 


Wananchi waliofika katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani wakifuatilia burudani za wasanii mbalimbali kabla ya kuaza kwa maandamano ya ufunguzi wa Tamasha la Busara Zanzibar.
Mwenyekiti wa Tamasha la Sauti za Busara Zanzibar akitowa maelezo kwa Mabalozi wa Uswisi na Norway walipokuwa katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu wakipata maelezo ya Mnara huo

Kikundi cha Six Unity wakionesha umahiri wao wa kujenza Dance wakati wa uzinduzi huo katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani.
Wasanii wakitowa Burudani katika Viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Kisonge.
Wanafunzi wa Skuli ya Maandalizi Jangombe wakicheza ngoma ya Bomo katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu kabla ya kuaza kwa maandamano ya Uzinduzi wa Tamasha la Busara Zanzibar.


Wananchi wakifuatilia burudani zilikuwa zikitolewa  na Vikundi mbalimbali vya Utamaduni vinavyoshiriki Tamasha la Busara Zanzibar.
Imeandaliwa na OthmanMapara.
Zanzinews.com.
othmanmaulid@gmail.com.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.