ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 4, 2017

MISA TANZANIA YAWAKUTANISHA WABUNGE NA WANAHABARI KUJADILI NAMNA NZURI YA KUSHIRIKIANA

“Tunapongeza kitendo hicho cha viongozi wetu kufikia hatua ya kuyataja hadharani majina ya wauzaji wa dawa za kulevya kwasababu jambo hili siyo rahisi na haikuwezekana huko nyuma kwahiyo kutokana na hili ni vyema wakuu wa  mikoa mingine waanze kuchukua tahadhari ya kupambana na watu watakaohamia mikoani baada ya kutangaziwa vita jijini Dar es Salaam, kwahiyo Mwanza, Tanga, Arusha nao wajipange kupambana na wafanyabiashara hawa,” alisema.

Akizungumzia kuhusu hali ya dawa za kulevya nchini, Soko alisema hali siyo nzuri kwani kuna ongezeko kubwa la matumizi ya dawa za hizo na kuitaka jamii kushiriki kwa kuwaumbua wauzaji na wasambazaji kwasababu wanaishi katika jamii na siyo suala hilo kuiachia serikali pekee.

“Matumizi ya Bangi yameongezeka kwa asilimia 6.5  kwa mwaka 2015/16  ambapo watumiaji 247 walishikiliwa kwa tuhuma hizo na matumizi ya dawa za viwandani aina ya Heroine na Cocaine nayo yameongezeka,” alisema.

 OJADACT wanasisitiza kwamba ni muhimu haki itendeke katika kuwashughulikia  watakaopatikana  na hatia katika sakata hilo na biashara ya dawa za kulevya kiujumla kadri  sheria  ya kuthibiti   dawa za kulevya  ya mwaka 2015 inavyosema.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.