ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 3, 2017

'CHAKUWA' YABAINISHA CHANGAMOTO ZILIZOPO KWA WASAFIRI NA SEKTA YA USAFIRI MWANZA.

Familia ya Bi. Ashura Mohamed wa kwanza kulia mwenye tiketi akionyeshoa tiketi ya awali waliyopewa na kukatazwa kupanda basi kwaajili ya safari yake mara baada ya Polisi kwa kushirikiana na Chama Cha Kutetea haki za Wasafiri (CHAKUWA) na kituo cha radio Jembe Fm kumsaidia kupata haki zake na sasa ataweza kusafiri kuelekea jijini Dar es salaam.
Licha ya mizigo yao kuondoka na Basi walilopaswa kusafiria wasijue usalama wake huko mbele ya safari au hata ikifika jijini Dar es salaam, Familia ya Bi. Ashura Mohamed alishindwa kusafiri na kuishi maisha ya kuungaunga kutokana na kuzuiwa na wahusika wa basi la Princess Shabaha wakimweleza kuwa amezidisha mtoto mmoja. 
 MAMA huyo ambaye tangu juzi tarehe 1 mwezi Februari alipaswa kusafiri yeye, watoto wawili na bibi mmoja kutoka Mwanza kuelekea jijini Dar es salaam lakini mpaka leo tarehe 3 alikwama kusafiri, lakini Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Chama Cha Kutetea Haki za Wasafiri (CHAKUWA) wamefanikisha safari yake leo asubuhi na mama huyo kulipwa stahiki zake za usumbufu alioupata.  BOFYA PLAY KUSIKILIZA ALICHOSEMA SIKU YA KWANZA

Mapema leo alfajiri Gsengo BLOG ilifika kituo cha mabasi yaendayo mikoani kwenye eneo la Nyegezi na kushuhudia mama huyo akiwa unafuu mara baada ya kupata stahiki zake ikiwa ni pamoja na kupata tiketi za kusafiri yeye na familia yake kuelekea mkoani Dar es salaam.
Elimu kwa madereva kutoka CHAKUWA.
CHAMA CHA KUTETEA HAKI ZA WASAFIRI TANZANIA WAISHANGAA MWANZA KUTOKUWA NA UTARATIBU WA KUTOA TIKETI.
Mkurugenzi wa CHAKUWA Kanda ya Mashariki Wilson Sylvester amesema kuwa moja kati ya changamoto walizokuja kuzibainisha kwa wananchi kupitiaelimu wanayoitoa ni pamoja na abiria kujua wajibu wao pale panapotokea upandishwaji holela wa nauli, namba za simu na TIN namba kutokuwepo kwenye tiketi za abiria na pale ajali inapotokea nini haki za abiria.   BOFYA PLAY KUSIKILIZA.
Moja ya mabasi mkoani Mwanza na siti ya dereva.
Mazingira ya mbele kwa dereva.
Ndani.
Uchakavu wa viti vya basi na mzingira.
Air Jordan


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.