ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 27, 2017

MAAFISA WA NGAZI ZA JUU WA WIZARA YA MAMBO YA NJE YA MAREKANI WAJIUZULU, HAWATAKI KUFANYA KAZI NA TRUMP.


Maafisa wote wa ngazi za juu wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani waliofanya kazi katika kipindi cha uongozi wa rais mstaafu wa nchi hiyo, Barack Obama wamejiuzulu kwa pamoja.
Gazeti la Washington Post limeandika kuwa, kujiuzulu kwa wakurugenzi na maafisa wote wa ngazi za juu wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani ni sehemu ya mwenendo wa kuachia ngazi maafisa wa ngazi za juu wa serikali ya Washington ambao hawataki kufanya kazi katika serikali ya Rais Donald Trump wa nchi hiyo. 
Kujiuzulu kwa kwa pamoja maafisa wote wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani kunatatiza kazi ya Rais Trump katika sekta ya masuala ya kigeni. 

Wamarekani wakiandamana kupinga uongozi wa Donald Trump.

Mkurugenzi wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani, Patrick Kennedy ambaye amekuwa na nafasi kubwa katika mchakato wa kuhamisha madaraka na ilidhaniwa kuwa ataendelea kufanya kazi katika kipindi cha uongozi wa Trump, naye alijizulu Jumatano iliyopita katika hatua iliyowashangaza wachambuzi wengi wa masuala ya Marekani. Wakurugenzi wengine wakuu waliojiuzulu nyadhifa zao katika wizara hiyo ni pamoja na Gregory Starr, Michele Bond na Tom Countryman.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.