ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 30, 2016

CHID BENZ AYARUDIA MADAWA.

Leo nimeona picha ya kushoto na nyinginezo kadhaa zikimuonesha alivyo hivi sasa zikisambaa mitandaoni katika hali ya wengi kusikitishwa na hali hiyo iliyomkumba kijana mwenzetu, Msanii wa bongofleva aliyekuwa na uwezo mkubwa wa kughani jukwaani kwa madaha na stail ya aina yake iliyowavutia wengi.

Chid Benzii hali yake kwa sasa inasikitisha sana anahitaji msaada mkubwa kwa namna yoyote ile, Shime watanzania naamini tunaweza kumrudisha na kumjenga Chid Benz na kurejea katika hali yake,ingaawaje inaweza kuchukua muda sana, lakini si haba kijana mwenzetu akaendelea na maisha yake maZuri aliokuwa nayo hapo mwanzo.

Wasanii popote pale mlipo mkae mkijua athari ya Madawa ya Kulevya ni mbaya,mbaya sana, ni vema mkajiepusha na janga hilo kungali mapema,kama ulikuwa unatumia, unataka kuanza kutumia unaendelea kutumia, Tafadhali achana nayo ni hatari kwa afya na maisha yako.
!!!CHUNGA SANA!!!

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.