ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 18, 2016

MAJAMBAZI WAVAMIA DUKA MWANZA, WAMUU MAMA WA KIHINDI KWA RISASI.


WATU wanaosadikia kuwa ni majambazi wakiwa na silaha za moto, wamevamia duka moja lililopo Mtaa wa Nkurumah (Katikati ya jiji la Mwanza) na kumuua kwa kumpiga risasi mama mmoja mwenye asili ya Kihindi kisha kupora kiasi cha pesa ambacho hakijajulikana bado.

Duka hilo linauza bidhaa mchanyanyiko Mini Supermarket pia hutoa huduma za miamala ya kifedha kwa njia ya mitandao ya simu za mkononi..

VIDEO YA TUKIO.
Imeelezwa kuwa wakati majambazi hao wakiwa kwenye harakati hizo, aliingia mama mmoja mwenye asili ya Kihindi kwa ajili ya kununua dawa za kutuliza maumivu, panadol, ndipo majambazi hayo yalipomfyatulia risasi tatu na kusababisha afariki dunia papo hapo kisha yenyewe kutoweka kusipojulikana.
Tukio hili limetokea kwenye duka na matukio ya kuporwa kwa watoa huduma za miamala ya pesa kwa njia ya simu imekuwa sugu kwenye Jiji la Mwanza huku majambazi wakitekeleza uharifu huo kwa hutumia silaha za moto hivyo kuleta hofu na amani kutoweka miongoni mwa wakazi wa Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.