ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, October 28, 2016

EXCLUSIVE DJ KFLIP AITEMA LAKE FM ARUDI JEMBE.

Katika picha ya pamoja ni Deejay K-Flip (katikati) baada ya kusaini mkataba mpya na Jembe Fm 93.7 mapema leo baada ya kurejea akitokea redio Lake Fm, wengine katika picha Kushoto ni Meneja wa Vipindi Jembe Fm Mbaba Vc na Eddie Jembe (kulia). 
NA. MWANDISHI WETU.
Dj machachari mwenye maskani yake Kanda ya ziwa toka jiji la miamba Mwanza Deejay K-flip hatimaye leo ijumaa ya tarehe 29 October 2016 ameikacha rasmi redio aliyokimbilia miezi mitatu iliyopita Lake Fm na kusaini mkataba mnono wa kuitumikia redio yake ya awali Jembe Fm.

Huu ni mrejeo wa kushitua sana na inatajwa kuwa ni kama fimbo kali ya maumivu itakayoigharimu radio aliyoikacha kwani baada ya Dj huyo kujiunga nayo miezi kadhaa iliyopita alikuwa ni mmoja wa wachoraji ramani wa redio hiyo kuhusu nini kinatakiwa kwenye soko la ushindani wa sasa.

"Najua hili ni pigo kwao, lakini nawasihi watulie kwani maisha lazima yaendelee, kupanga ni kuchagua nami nimechagua kurudi nilikotoka nyumbani kwetu" alisema K-Flip 


K-Flip na Dj Scopion.
Akizungumzia kuhusu sababu zilizo mfanya kurejea Jembe Fm K-Flip amesema kuwa ndani ya wiki mbili tu za mwanzo baada ya kujiunga na Lake Fm aliona  mzigo mkubwa aliojitwisha, kwani ilimlazimu kujifunza kwa haraka utamaduni mpya wa utengenezaji na uendeshaji vipindi na akawa na wakati mgumu kwani ilimlazimu kugeuka kuwa mwalimu kuwafundisha watangazaji wa kituo hicho mfumo utakao uza redio kwa raia.

"Nakumbuka jinsi nilivyokuwa na wakati mgumu kukipitia kila kipindi na kukisahihisha kwa kuwasilishia maoni yake na marekebisho, ni kazi kweli kwani ilinipasa kuamka mapema kusikiliza kila kipindi na contents zake, kazi ambayo ili nimaliza akili" alisema 


K-Flip na producer Oxy.



"Hapa Jembe Fm watangazaji na Ma-Dj wote wanajua majukumu yao, kila kipindi kimeshiba, ubunifu kila kunapokucha na matirio mpya kila siku, Dj unafanya kazi yako umerelux kiasi kwamba unaweza kwenda hata likizo ukaacha mambo yanaendelea bila wasiwasi, thanx God nimerudi nyumbani najisikia niko mahali sahihi na salama" 

"Pamoja na kwamba niliondoka na kwakuwa sikuondoka kwa ubaya bado nilikuwa nakutana na watu wangu wa nyumbani ambao tuliendelea kula pamoja, kunywa pamoja na kushea burudani mbalimbali pamoja lakini nilikuwa nahisi kuna kitu kama kinapungua hivi, kweli niliteseka na mwisho wa siku nikaamua kuutua mzigo" kisha akaongeza.

"Naomba samahani kwa wale watakao nifikiria vibaya lakini haya ni maisha yangu"

Uamuzi huo umepokelewa kwa shangwe na memba wa redio hiyo


K-Flip na Chriss The Dj.
K-Flip na mtangazi Johari Ngassa.


K-Flip na Bob White Pamba.
Head of Djz wa Jembe DjZ wakuitwa Dj Mike beatz (kushoto) akimkabidhi vitendea kazi Dj K-Flip.
Mengi yalisikika kwenye kipindi cha Hotzone.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.