ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 23, 2016

HATIMAYE MWENYEKITI MPYA WA CCM APATIKANA HII HAPA KAULI YAKE YA KWANZA.

Hotuba ya mwenyekiti mpya wa CCM, Mhe. John Magufuli akizungumza mara baada ya kutangazwa kuwa mwenyekiti mpya wa CCM.


Mwenyekiti mpya wa CCM, Rais John Magufuli amezungumzia mambo manne atakayoshughulikia katika chama hicho, hasa kufanya mabadiliko makubwa ili chama kiweze kwenda na wakati.
Pia, Rais Magufuli amewaomba wana-CCM kumuombea ili awe na uvumilivu kama wa mtangulizi wake, Jakaya Kikwete katika kukabiliana na utovu wa nidhamu kwenye chama.
Hayo ni sehemu ya hotuba yake ya shukrani baada ya kupata kura zote 2,398, katika uchaguzi uliokuwa wa mgombea mmoja wa nafasi ya mwenyekiti wa CCM uliofanyika jana kwenye ukumbi wa mikutano wa chama hicho uliopo mjini hapa.
Mwenyekiti huyo mpya alisema utendaji kazi ni suala muhimu, hivyo atajenga chama madhubuti ili kiweze kuisimamia Serikali.

















Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.