ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 23, 2016

KOCHA Arsene Wenger awapa jeuri mashabiki wake.


Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ameweka mkazo kwamba yupo tayari kutumia pesa kusajili mchezaji sahihi ambaye ni anaweza kufiti kwenye mfumo wake.
Mpaka sasa, Arsenal wamefanikiwa kutumia kitita kikubwa kumsajili Granit Xhaka na baadaye kuwachukua Mjapani Takumo Asano na Rob Holding
Wenger amekuwa akikosolewa kwa kushindwa kwake kusajili wachezaji wenye majina makubwa hasa kwenye nafasi ya beki wa kati na ushambuliaji licha ya wapinzani wake wengi kufanya hivyo.
Hata hivyo Wenger amesema kwamba bado hajamaliza kusajili ila anaangalia mtu sahihi wa kumleta kwenye timu yake.
“Tuna mwamko mkubwa. Kama tunapata mchezaji sahihi basi hatuwezi kusita kutumia pesa kumsajili,” Wenger aliimbia tovuti ya klabu baada ya sare ya bao 1-1 kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Lens.
“Mpaka sasa tayari tumetumia pesa nyingi. Kwa ujumla tayari tumeimarisha kikosi chetu kwa kiasi kikubwa lakini hata hivyo bado yuko macho kwenye dirisha la usajili.
“Nisingeoenda kuangalia zaidi majina, kwasababu kama hujawapata, watu watakuuliza kwanini. Tuko makini, tena makini sana kila siku na hatujamaliza zoezi la usajili. Ndiyo kwanza tarehe 22 leo (jana) na dirisha la usajili linafungwa Agosti 31. Na unafahamu fika kwamba mambo mengi hutokea wiki ya mwisho. Hivyo bado kuna safari ndefu. Lakini tupo makini na tunalifanyia kazi suala hilo.
Mpaka leo hakuna aliumiapesa nyingi kutuzidi katika usajili nchini hapa. Hata kama [Paul] Pogba anataraji kuja hapa kutokea Italy, sijui….

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.