ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, June 30, 2016

BILA KUBORESHA SHERIKA YA USIMAMIZI WA MAZINGIRA VITA DHIDI YA UCHAFUZI WA MAZINGIRA NI NDOTO.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Utawala Bora na Demokrasia nchini (ADLG), Mr. Jimmy Luhende,  akitoa darasa katika Mjadala wa Mwezi June uliofanyika hii leo Jijini Mwanza, na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali toka Taasisi, mashirika na vikundi vya ujasiliamali Kanda ya Ziwa.
 Jamal Baruti ambae ni Mratibu wa Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC, Kanda ya Ziwa, akiwasilisha mada juu ya tathmini ya athari za mazingira zitokanazo na shughuli za uchimbaji wa madini.
Taasisi ya ADLG huendesha mijadala tofauti tofauti kila mwisho wa mwezi ambapo wadau mbalimbali hukutana na kujadili mada husika. Mjada wa mwezi june umeangazia Fursa, changamoto na athari za kimazingira zitokanazo na shughuli za migodini. 

 Katika mjada ulio wasilishwa, wadau wameishauri serikali kupia Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEC, kuboresha sheria ya usimamizi wa mazingira ili kuweza kuwafanyia tathmini za uchafunzi wa mazingira wachimbaji wadogo kwa kuwa baadhi yao wamekuwa wakichangia uchafunzi wa mazingira nchini. 
Kwa umakini na kumbukumbu daftarini, wadau wa mazingira wakichukuwa pointi.
Kwa mujibu wa wachangiaji, Tathimini ya uchafuzi wa mazingira imekuwa ikifanyika kwa wachimbaji wakubwa wa madini kabla na baada ya uchimbaji lakini wachimbaji wadogo wamekuwa hawaguswi na tathmini hiyo kutokana na kutojumuishwa katika tathimini hiyo kwa mjibu wa sheria ya mazingira.Ni vyema sasa wachimbaji wadogo wadogo wakashirikishwa ipasavyo ili kuondokana na uchafuzi wa mazingira katika shughuli zao.
Kasi ya maendeleo katika nchi zinazoendelea inaweza kurudi nyuma miaka mitano ijayo,iwapo hatua thabiti hazitachukuliwa kupunguza kasi ya uharibifu wa mazingira.
Ripoti ya 2011 kuhusu uendelevu na usawa ilieleza kuwa, uendelevu wa mazingira unaweza kufikiwa kwa njia ya haki na yenye matokeo mema iwapo masuala ya afya, elimu, kipato, na tofauti za jinsia kuchukuliwa hatua za kimataifa kuhusu uzalishaji wa nishati na utunzaji wa mazingira.

Uharibifu wa mazingira unatishia uhai wa viumbe duniani kwa kiasi kikubwa kutokana na shughuli mbalimbali za wanadamu ikiwemo ukataji miti na uchomaji moto misitu ya asili.

Msisitizo mkubwa umekuwa ukifanywa na wadau wa mazingira kwa kuhakikisha mikataba na sheria zinawekwa ili kulinda, mazingira na viumbe adimu wasitoweke.
Tanzania ni moja ya nchi duniani zilizobarikiwa kuwa na misitu ya asili na mito mikubwa isiyokauka maji kwa kipindi cha mwaka mzima.

Mbali na vivutio hivyo,kumekuwa na uelewa mdogo wa masuala ya uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji miongoni mwa jamii.

Ukosefu wa elimu kwa jamii ya Watanzania umesababisha wananchi kushindwa kutambua umuhimu wa kuhifadhi mazingira na vyanzo vya maji vilivyowazunguka katika maeneo yao.
Wadau wa habari ambao vile vile ni Bloggers wa Mwanza, kutoka kushoto Gsengo, Atley Kuni na Kijukuu cha Bibi.
Mchanganuo toka katika jedwali la Makampuni na kuanzishwa kwake ikiwa ni pamoja na mapitio ya sheria ya mazingira.
Wadau wa mazingira wamekusanyika hapa 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.