ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 18, 2016

RC MWANZA APOKEA GARI LA WAGONJWA.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella, akizungumza na watumishi kabla yakupokea msaada wa gari la wagonjwa.
Mkuu wa mkoa akikata Utepe kuashiria uzinduzi wa mapokezi ya Gari la Wagonjwa kutoka Rafiki Surgical Mission.
Balozi, Issaya Chialo, alipokuwa akitoa maelezo mafupi juu ya msaada wa gari la wagonjwa walilo likabidhi kwa hospitali ya Mkoa wa Mwanza.
Watumishi katika hospitali ya Mkoa wa Mwanza, wakimasikiliza kwa makini mkuu wa mkoa wa Mwanza hayupo pichani, wakati wa hafla fupi yakukabidhi gari hilo.
Mganga mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Subi, akitoa maelezo ya awali kuhusu huduma za afya katika mkoa wa Mwanza wakati wa hafla hiyo ya makabidhiano.
Wananchi wanao hudumiwa katika hospitali hiyo ya mkoa nao hawakuwa nyuma katika hilo, hapo wakisiliza kwa makini maelezo ya mkuu wa mkoa.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Nyamagana, Bi Maricella, akimkaribisha mkuu wa mkoa wa Mwanza.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella, akikabidhi cheti cha Shukrani kwa Balozi Issaya Chialo, kama sehemu ya shukrani kwa kutambua mchango wa Rafiki Surgical Mission, walio utoa kwa Mkoa huo wa Gari la Wagonjwa.(Habari na picha zote na Afisa habari wa mkoa wa Mwanza)
Hilo ndilo gari lililotolewa na Rafiki Surgical Mission.
Na. Atley Kuni RS Mwanza.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella amepokea gari la Wagonjwa kutoka kwa Sargical Rafiki Mission kwaajili ya kuhudumia wananchi wa mkoa huo ambalo amelikabidhi kwa uongozi wa  hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekouture na kuwataka kuitunza kwa maslahi mapana ya wananchi wa mkoa huo.
Akizungumza kabla yakupokea gari hilo mkuu huyo wamkoa amesema, msaada walio upokea kutoka kwa Rafiki Mission ni masaada wakupigiwa mfano kwakuwa watu wengi wanabarikiwa vitu vingi lakini suala lakutoa misaada wameshindwa.
Mongella amesema kama mkoa ukipata marafiki wa aina ya Rafiki hawana budi kuwa ng’ang’ania wasiondoke kwenye himaya yao. “ Nafahamu hata sisi tunabarikiwa sana lakini hata siku moja hakuna mtu aliwahi kuleta hata mkasi, hivyo lazima tufahamu kutoa ni moyo na sio utajiri.
Katika hatua nyingine mkuu huyo wa mkoa amesema, karibu asilimia tisini ya matatizo ya afya yanayo ikabili jamii ya kitanzania yamejikita katika suala la afya ya mama na mtoto ambayo kama taifa tukifanikiwa kuwekeza katika hili, basi matatizo mengine ya afya yataondoka yenyewe “ Najua suala la mama na mtoto ni tatizo mtambuka kwa taifa, hivyo tukiwekeza zaidi katika afya ya mama na mtoto tutakuwa tumekabili changamoto kubwa ya masuala ya afya na itawawezesha wananchi kujikita katika shughuli za maendeleo”, alisema Mongella
Awali akitoa salama za Rafiki Mission, Balozi Issaya Chialo, alisema wao kama Rafiki Mission, wanatambua matatizo yanayo ikabili jamii ya kitanzania hususan masuala ya afya,  na kwamba wao kama Rafiki Surgical mission, hawana ubaguzi katika utoaji wa misaada kwa jamii nzima ya kitanzania.
“ Mkuu wa mkoa sisi shughuli zetu zipo katika mkoa wa Mtwara tukijikita katika zaidi katika utafutaji wa mafuta na Gesi, lakini hiyo haituzuii sisi kupeleka misaada pembe zingine za nchi na ndio maana leo tupo katika mkoa wako wa  Mwanza” alisema Balozi Chialo nakuongeza kuwa, wanajisikia fahari katika hilo.
Chialo ameutaka uongozi wa Hospitali ya rufaa ya  mkoa wa Mwanza Seko’uture kulitunza gari hilo la wagonjwa lenye thamani ya Mil. 40, ambalo litasaidi katika kuwakimbiza wagonjwa wenye mahitaji maaluma sehemu mbali mbali za mkoa huo na mikoa ya jirani.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dkt. Subi, amesema hivi sasa hospitali ya mkoa huo inakabiliwa na changamoto ya chumba cha kutolea huduma ya upasuaji kwa akina mama, ambapo mkuu wa mkoa amemtaka Mganga huyo wa mkoa kutenga kiasi cha Mil. 5 kutoka katika makusanyo ya ndani ya hospitali ya mkoa huo  na Mkuu wa mkoa kupitia wadau wa maendeleo atahakikisaha kiasi kingine cha fedha kinacho salia  kinapatikana kwaajili ya ukarabati wa chumba hicho ambacho kinahitaji Mil.20 ili kiweze kufanya kazi ya upasuaji kwa akina mama.
Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mwanza  Seko’uture, imekuwa msaada kwa wagonjwa wa mkoa huo na mikoa ya jirani kutokana na huduma zake kuwa nzuri na madaktari mabingwa wanaopatikana katika mkoa huo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.