ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 24, 2016

MKUU WA MKOA WA MWANZA ALIPOPATA FURSA KUKARIBISHA WAGENI WALIOHUDHURIA MKUTANO MKUBWA WA INJILI WA REINHARD BONNKE LIKIHUBIRIWA NA DANIEL KOLENDA

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongela Alhamisi ya tarehe 23 mwezi juni katika uwanja wa Furahisha Kirumba jijini Mwanza amewakaribisha wageni wote na wenyeji kuzitumia vyema fursa zipatikanazo ndani ya mkoa wake, huku akiwahimiza wananchi hao kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa ili kuilinda amani ya familia na nchi kwa ujumla.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongela akizungumza na kusanyiko la Mkutano wa Injili la Reinhard Bonnke linaloratibiwa na Umoja wa Makanisa Mwanza na kuhubiriwa na mhubiri wa Kimataifa toka nchini Ujerumani Daniel Kolenda.
Ummati uliofurika katika viwanja vya Furahisha kirumba jijini Hapa kwaajili ya kulishwa neno.
Kamati ya maandalizi iliyoundwa na wachungaji na maaskofu kutoka Umoja wa Makanisa mkoa wa Mwanza ikiwa jukwaa kuu na Muhubiri wa Kimataifa Daniel Kolenda wa tano kutoka kushoto.
Sehemu waliyoketi waratibu wa mkutano.
Kusanyiko katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongela akipongezwa na mtumishi wa Mungu mara baada ya kuzindua kusanyiko.
Kuna salamu iliyoendelea toka jukwaa kuu ambayo iliwavutia wengi...ambayo iliambatana na kushangaa juu ya ukuu wa Mungu, ni Muhubiri Daniel Kolenda na Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongela!!
Kusanyiko lilipunga mkono kuashiria kushangilia.
Kona na kona viwanja vya Furahisha kusanyiko la Mkutano mkubwa wa Injili wa Reinhard Bonnke unaohubiriwa na Daniel Kolenda kutoka nchini Ujerumani.
Amen
Usikivu ni kwa asilimia 100.
Injili inapenya ndani ya kusanyiko hili litakalodumu kwa uda wa siku tatu mfululizo kiliele kikiwa siku ya jumapili ya tarehe 26 June 2016.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.