ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, June 15, 2016

JEMBE FM YAMSAKA SURA MBAYA NA MKALI WA DANADANA.

Mc wa mpango mzima wa kumsaka Sura mbaya na Mkali wa danadana, ambaye ni Mtangazaji wa Jembe Fm kipindi cha Hit Zone, Babajuti akiongoza mchakato wa kusaka vipaji kwa kutaja vigezo na masharti kwenye uwanja wa Stendi ya Igoma ulioko Nyamagana jijini Mwanza.
Ufundi wa kucheza na mpira kwa kutumia miguu yote ni moja ya vigezo vya kufaulu kuwakilisha kituo kwenye fainali zitakazopigwa tarehe tarehe 25 Juni 2016 pale Rock City Mall. Hewani ni mshindi toka Igoma Owasi Tiger akionesha maufundi katika kinyang'anyiro cha kumsaka Mkali wa danadana chini ya udhamini wa Tigo, StarTimes, na pikipiki za GSM.
Igoma kumekucha
Msemaji kutoka GSM akizungumza na wana Igoma kuhusu huduma wanazozitoa kupitia pikipiki zao mpya zenye ubora uliofanyiwa tafiti kulingana na soko na mazingira ya watumia barabara nchini Tanzania.
Muamko wa wana Igoma.
Ushindani katika Mkali wa Danadana ulikuwa mkubwa.
Maufundi hadi ndala zinakatika......balaaaaaaaa!!!
Ufundi na mautundu.
Alaaaaa......maufundi zaidi.
Ze area.
Mshiriki wa shindano la Sura Mbaya Igoma katika pozi la kucheka.
Wadau wa Igoma.
Pia mashabiki waliojitokeza viwanjani hapo walichomoka na zawadi mbalimbali kutoka kwa wadhamini hapa jamaa anaondoka na Tishirt ya StarTimes baada ya kujibu swali.
Mshindi mwingine katika maswali ya papo kwa hapo..
Kijana huyo aliigiza moja kati ya sauti za matangazo ya Jembe Fm ambapo alimuigiza Mhe. Magufuli na kujinyakulia kalamu toka kwa moja wa wadhamini wetu StarTimes.
Ze area.
Pozi la kushangaa mshiriki toka Igoma.
Kucheka jeh!!.
Washiriki wawili Stamin Chankaga (kushoto) na Elisha Ezekiel (kulia) ndiyo wawakilishi kwenye kinyang'anyiro cha kumsaka Sura Mbaya, wakiwakilisha kituo cha Igoma kwenye fainali itakayopigwa tarehe 25 Juni 2016 pale Rock City Mall ambapo mshindi atachomoka na zawadi ya pikipiki toka Kampuni ya GSM pamoja na zawadi nyingine kibao toka kwa wadhamini wa mchakato mzima ambao ni Tigo, StarTimes na Jembe Fm.
Wawakilishi wa shindano la Sura Mbaya kutoka Igoma katika picha na wadhamini.
Wawakilishi wa kumsaka mkali wa danadana igoma Owasi Tiger (wapili kutoka kulia) na Chuse Juma (wapili kutoka kushoto) wakiwa wamewekwa kati na wadhamini kwenye picha ya pamoja.
Maufundi ya Jembe Djz na Deejay Jacko.
Mzigo wa mshindi toka GSM.
Me inade area.
Next ni Pasiansi wilayani Ilemela jijini Mwanza

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.