ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 3, 2016

BANC ABC YAANZISHA HUDUMA YA KUKUZA BIASHARA AFRIKA.

 Mkurugenzi Mtendaji wa BancABC Tanzania Bwana. Dana Botha (wa pili kulia), akibadilishana mawazo na baadhi ya wateja wa benki hiyo katika hafla waliyowaandalia  wateja wao kuwajulisha mikakati ya benki hiyo katika kuhakikisha wanatoa huduma bora za kibenki chini ya kundi la atlasmara. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi. Wanaomsikiliza kutoka kushoto ni, John Kazimoto, Jones Mwalemba, naJohn Du Toit.
 Mkurugenzi Mtendaji wa BancABC Tanzania Bwana. Dana Botha ( kulia), akizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo katika hafla waliyowaandalia  wateja wao kuwajulisha mikakati ya benki hiyo katika kuhakikisha wanatoa huduma bora za kibenki chini ya kundi la atlasmara. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi. Wanaomsikiliza kutoka kushoto ni, John Kazimoto na Jones Mwalemba.
Mkuu wa Idara ya Uwekezaji wa Kibenki ya Makampuni wa Kundi la BancABC, Dk. Mabouba Diagne (wa pili kulia), akibadikishana mawazo na baadhi ya wateja wa benki hiyo katika hafla waliyowaandalia  wateja wao kuwajulisha mikakati ya benki hiyo katika kuhakikisha wanatoa huduma bora za kibenki chini ya kundi la atlasmara. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.
Mkuu wa Idara ya Uwekezaji wa Kibenki ya Makampuni wa Kundi la BancABC, Dk. Mabouba Diagne (wa pili kulia), akimsikiliza mmoja wa wateja wa benki hiyo, John Du Toit katika hafla waliyowaandalia  wateja wao kuwajulisha mikakati ya benki hiyo katika kuhakikisha wanatoa huduma bora za kibenki chini ya kundi la atlasmara. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.

Mkuu wa Idara ya Uwekezaji wa Kibenki ya Makampuni  BancABC Tanzania, Khalifa Zidadu (kulia), akizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo katika hafla waliyowaandalia  wateja wao kuwajulisha mikakati ya benki hiyo katika kuhakikisha wanatoa huduma bora za kibenki chini ya kundi la atlasmara. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Ofisa Fedha Mkuu wa Superdoll, Sateesh Babu Desu na Prasanthar Govinder pia wa Superdoll.

 Mkurugenzi Mtendaji wa BancABC Tanzania Bwana. Dana Botha ( kulia), akizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo (hawapo pichani) katika hafla waliyowaandalia  wateja wao kuwajulisha mikakati ya benki hiyo katika kuhakikisha wanatoa huduma bora za kibenki chini ya kundi la atlasmara. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi. Wanaomsikiliza kutoka kushoto ni, John Kazimoto na Jones Mwalemba.
Mkuu wa Idara ya Uwekezaji wa Kibenki ya Makampuni wa Kundi la BancABC, Dk. Mabouba Diagne (wa pili kulia), akifafanua jambo mbele ya baadhi ya wateja wa benki hiyo (hawapo pichani), katika hafla waliyowaandalia  wateja wao kuwajulisha mikakati ya benki hiyo katika kuhakikisha wanatoa huduma bora za kibenki chini ya kundi la atlasmara. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.

Bank ABC imeanzisha huduma mpya kwa wafanyabishara wakubwa kuhamisha and kuingiza mitaji yao ndani na nje ya nchi kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya elektroniki.Akizungumza katika hafla iliyofanyika Jumatano hii, Mkuu wa kundi la Benki hiyo katika ukanda wa Afrika, Dk. Mabouba Diagne alisema wametenga Dola za Kimarekani milioni 20 (zaidi ya Sh billion 40) kwa ajili ya mpango huo unaolenga kuimarisha biashara miungoni mwa nchi za Afrika.

“Tumeanzisha huduma hii mpya kwa ajili ya kurahisisha na kukuza biashara miungoni mwa wafanyabishara wakubwa barani Afrika. Tunataka wafanyabiashara waweze kufungua milango yenye fursa nyingi za kibishara barani Afrika,” Dk. Diagne alisema.Alisema Banc ABC imezimia kuwawezesha Watanzania kutumia teknolojia mpya ya kuhamisha mitaji na fedha nyingi si ndani ya nchi tu bali nje ambako kuna fursa nyingi za biashara zisizotumika.

“Mara nyingi wafanyabishara wengi wa hapa nchini wanaofanyabishara nan chi jirani wamekuwa wakilalamika kukosekana kwa huduma bora za kuhamisha fedha kwa wingi. Sasa jawabu limepatikana kwa Banc ABC kuanzisha huduma za kisasa za kuhamisha mitaji,” alisema.

Alisema watu wanaweza kuhamisha mitaji hata fedha nyingi nchi za nje kwa kutumia simu za mkononi bila kuathiri biashara.“Tumeanzisha huduma hii kwa sababu biashara baina ya nchi za Afrika ni jambo muhimu la kuwezesha nchi na wafanyabishara waweze kutumia fursa nyingi zilizomo barani Afrika kutokana na bara hili kuwa na rasilimali nyingi asilia,” alisema kiongozi huyo msomi mwenye shahada ya juu ya uzamili ya hisabati.

Alisema suala la kubadilishana na kuhamisha mitaji ni biashara kubwa duniani kwa sababu mitaji ni bidhaa muhimu kwa maendeleo ya nchi na watu.Mapema mkurugenzi wa Banc ABC Tanzania, Bw Dana Botha alisema tayari benki hiyo imeanzisha mtandao wa matawi 100 hapa nchini na kuwa miungoni mwa benki imara.Naye Mtendaji Mkuu wa kundi la benki hiyo Dk. Blessings Mudavanhu alisema kuwa benki hiyo ambayo imesajiliwa katika soko la fedha la London, ilizindua aina ya bidhaa yake mpya na kujitanua kimataifa baada ya kuungana na Atlas Mara.

“Tutatumia jamvia la teknolojia ya habari na mawasiliano. Tunataka watu waanchane na kuandika cheki nyingi na kutumia gharama kubwa za miamala ya katatazi badala yake watumie simu za mkononi,” alisema Dk Madavanhu.Alisema benki hiyo ambayo inaendesha biashara katika nchi za Tanzania, Nigeria, Afrika kusini, Botswana Zimbabwe, Rwanda, Burundi na Zambia imedhamiria kuwa benk kubwa inayokuza biashara miungoni mwa nchi za Afrika.

Katika hafla hiyo kampuni kadhaa kubwa zilishiriki na kuvutiwa na huduma hiyo mpya itakayotolewa na benki hiyo ya kimataifa. Kampuni hizo ni; Statoil, Mount Meru (T) Ltd, Lake Oil. Superdoll na Puma Energy.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.