ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 12, 2016

UPDATES: MSIBA WA MTOTO WA ANKAL ISSA MICHUZI

Assalaam aleikum,

Familia ya Ankal Issa Michuzi iliyopatwa na msiba wa kuondokewa na Mtoto wa Ankal, Maggid Muhidin aliefariki Jumapili Mei 8, 2016 huko Durban, Afrika Kusini.

 Taarifa ya sasa ni kwamba, Ndugu zetu kule Durban wanakamilisha taratibu za kusafirisha mwili, hivyo sote tupo standby kwa hilo na naomba tufanye subira kwani hiki ni kipindi kigumu kwetu sote, na mwili ukiwasili ratiba rasmi ya mazishi itatolewa.

Msiba uko Tegeta Wazo Hill, Nyumbani kwa Mama Mzazi wa Marehemu (likiwa ni ombi maalum la Mama), na taratibu zote zinafanyika huko.

NAMNA YA KUFIKA MSIBANI
Ukitokea Tegeta Kibaoni kama unaelekea Kiwanda cha Cement Wazo, mbele mkono wako wa kulia utaona Kanisa la KKKT na ukienda mbele tena kidogo, utaona uzio wenye rangi ya njano umeandikwa Twiga Cement, unakatisha hapo upande huo huo wa kulia. ukikatisha tu utaona kuna mtaa mwingine unaingia upande wa kulia, uache na usogee mbele, utaona mtaa mwingine unaingia kulia, ingia nao huo na utakuwa umefika msibani.



Innalillah wa inna ilayhi raajiun
-AMIN.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.