ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 8, 2016

BREAKING NEWS: WENJE APIGWA CHINI KESI YAKE DHIDI YA MABULA.

Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza Mtaturu akimpongeza Mbunge wa Nyamagana Stanslaus Mabula mara baada ya kesi ya kupinga matokeo ya Ubunge iliyofunguliwa na Ezekiel Wenje katika jimbo hilo kufutwa.
Mahakama kuu kanda ya Mwanza imeifuta kesi ya kupinga Matokeo ya Ubunge katika jimbo la Nyamagana iliyokuwa imefunguliwa na mbunge aliyemaliza muda wake Ezekiel Wenje (CHADEMA) baada ya kushindwa kuthibitisha.
Kufutwa kwa Kesi hiyo kumeweza kumpatia ushindi Stanslaus Mabula (CCM) kuwa mbunge halali wa jimbo la Nyamagana jijini Mwanza,ambapo wafuasi wa CCM wanaelezwa kuwapo nje ya Mahakam hiyo huku wakishangilia ushindi wa Mbunge huyo.


Mbunge wa Nyamagana Stanslaus Mabula akifanya mahojiano na waandishi wa habari jijini Mwanza.
Jembe Fm 93.7 kupitia mwandishi wake Mansour Jumanne iliyekuwa eneo la tukio  Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza na kisha baadaye ofisi za CCM wilaya ya Nyamagana anasimulia kilichotokea kupitia kipindi cha KAZI NA NGOMA
BOFYA PLAY KUSIKILIZA KILICHOJIRI.

Mbunge wa Nyamagana Stanslaus Mabula akizungumza na wananchi waliojitokeza kumpongeza mbele ya ofisi za CCM Nyamagana, kulia ni Mkuu wa Wilaya hiyo Baraka Konisaga.
Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Nyamagana pamoja na marafiki wa Mbunge wa Nyamagana Stanslaus Mabula walipita mitaa mbalimbali katikati ya jiji la Mwanza kuelekea ofisi za CCM wilayani humo huku wakiimba kusherehekea.
Selfie za makada wa CCM.
Mabangoz.....!!!

Mwaka jana Octoba 25 Mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stanslaus Mabula alitangazwa mshindi wa mbio za ubunge katika jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza kwa kupata kura 81, 170 dhidi ya Ezekiel Wenje (Chadema) aliyepata kura 79, 280.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.