ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 25, 2016

GESI NYINGINE YAGUNDULIKA BONDE LA MTO RUVU INA UKUBWA WA UJAZO FUTI TRILIONI 2.17

Tanzania  imedhihirisha kuwa ni tajiri mkubwa wa rasilimali ya gesi asilia baada ya kugundulika kwa gesi nyingine katika bonde la mto Ruvu yenye ukubwa wa ujazo wa futi trilioni 2.17.

Ugunduzi huo wa gesi asilia umefanywa na Kampuni ya Dodsal Hydrocarbons and Power Tanzania Limited ambayo imekuwa inafanya shughuli za utafutaji wa gesi na mafuta katika Mkoa wa Pwani.

Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Pilavullathil Surendran alisema jana katika mkutano wa wawekezaji wa gesi na mafuta ulioandaliwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kuwa, thamani ya gesi iliyoko katika eneo hilo inafikia Dola za Marekani bilioni sita sawa na Sh trilioni 12.

Ugunduzi huo mpya unafanya hadi sasa Tanzania kuwa na amana ya gesi yenye ukubwa wa futi za ujazo trilioni 57.27.

Kwa upande wake, Profesa Muhongo alithibitisha kugundulika kwa gesi hiyo tangu Julai mwaka jana, lakini akaeleza kuwa Serikali imechelewa kutangaza ugunduzi huo kama inavyoagizwa na Sheria ya Mafuta ya Mwaka 2015 kutokana na shughuli za uchaguzi.

“Sheria mpya inatutaka kabla ya waziri mwenye dhamana ya gesi kutangaza ugunduzi mpya wa gesi na mafuta ni lazima athibitishiwe na mamlaka ya udhibiti wa bidhaa za Petroli na Gesi (PURA).

“Wizara yangu itawasiliana na mwanasheria mkuu wa serikali ili kupata ushauri wa kisheria kuhusu jambo hilo na bahati nzuri tayari PURA imeshaanza kushughulikia jambo hilo na naamini kuwa nitatangaza ugunduzi huo mpya hivi karibuni,” alifafanua Profesa Muhongo.

Licha ya ugunduzi huo mpya tayari gesi imegundulika katika maeneo ya kisiwa cha Songo Songo mkoani Lindi na eneo la Mnazi Bay huko Mtwara na katika Wilaya ya Mkuranga, Pwani pia kumegundulika kiasi kikubwa cha gesi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.