ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 23, 2016

GAZETI LA MTANZANIA LAPEWA SIKU 3 KUKANUSHA TAARIFA ZA TAMVU KUMWOMBA MAGUFULI KUMFUKUZA KAZI MKUU WA MKOA WA MWANZA.

Muungano wa wapiga kura Tanzania TAMVU umekanusha taarifa zilizoandikwa na gazeti ka Mtanzania juu ya ombi la kufukuzwa kazi mkuu wa mkoa wa Mwanza.

Rais wa muungano huo Milton Rutabana akizungumza na Jembe Fm amesema taarifa hizo si za kweli na kuwa hakutoa taarifa yoyote ya kwamba Rais amfukuze kazi mkuu huyo.

Kufuatia hali hiyo Bwana Milton amesema tayari amekwisha tuma barua kwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti hilo kukanusha taarifa hizo. BOFYA PLAY KUSIKILIZA


Bwana Lutabana ametoa siku 3 kwa gazeti hilo kuomba radhi kupitia kurasa zake za mbele za gazeti sanjari na kukanusha taarifa hiyo vinginevyo atalichukulia hatua za kisheria.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari iliyoandikwa na Muungano huo inasema Gazeti la Mtanzania lilichapisha taarifa tarehe 19 January 2015 ikisema Muungano huo umemwomba Rais Magufuli kumfukuza kazi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa mulongo kutokana na kukosa sifa za kuongoza mkoa huo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.