ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, January 13, 2016

AKAMATWA NA MENO YA TEMBO KILO 50 YENYE THAMANI YA TSH MIL 120 MKOANI KATAVI

Meno ya Tembo vipande 8 vyenye uzito wa kilo 50 ya thamani  ya milioni  120  ambayo ni sawa na Tembo hai wane aliyokamatwa nayo hivi karibuni mtuhumiwa  Nzuri Ndizu Mkazi wa Kijiji cha Mbede Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi
 
 Mtuhumiwa  Nzuri  Ndizu  Mkazi wa Kijiji  cha Mbende Wilaya ya Mlele akiwa katika  ofisi ya Kamanda  wa Polisi wa Mkoa wa Katavi  baada ya kukamatwa na meno ya Tembo  vipande  nane   yenye thamani ya shilingi  milioni  120  hapo juzi
Kamanda wa  Polisi  wa Mkoa Katavi  Dhahiri Kidavashari akiwa ameshika meno ya Tembo  aliyokamatwa nayo mtuhumiwa  Nzuri Ndizu  mkazi wa Kijiji cha Mbede Wilaya ya Mlele   Mkoa wa Katavi ambae alikamatwa juzi akiwa na vipande 8 yenye thamani  ya milioni 120
Picha  na  Walter Mguluchuma Katavi yetu blog.

Mtu mmoja aliyefahamika  kwa jina la  Nzuri  Ndizu (44) Mkazi wa Kijiji cha Mbede  Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi  amekamatwa akiwa  na meno  ya Tembo  nane  yenye uzito wa kilogramu 50 yakiwa na thamani ya shilingi milioni 120 ambapo ni sawa na Tembo wanne waliuwawa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia waandishi wa Habari   kuwa  mtuhumiwa huyo alikamatwa   mida ya saa tatu  na nusu .
Kidavashari alisema mtuhumiwa  Ndizu  alikamatwa  kufuatia   misako  na  uparesheni mbalimbali zinazoendelea kufanywa  na Jeshi la Polisi  ikiwa ni kuhakikisha  wahalifu  wa makosa mbalimbali wakimemo  wawindaji  haramu  wa wanyama pori  wanakamatwa.
Siku hiyo ya tukio  jeshi la polisi  lilipata taarifa  toka kwa Raia  wema  kuwa katika  pori  la akiba  la Lwafe  kuna watu  wanajihusisha na biashara haramu ya meno ya Tembo .
Kidavashari aliendelea kuwaambia waandishi wa Habari  baada ya taarifa hizo kupokelewa  ufuatiliaji  ulifanyika  kwa polisi kufika  kwenye eneo hilo  na kuweka  mtego .
Na walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo  Nzuri Ndizu  akiwa  na meno ya Tembo  vipande nane  akiwa ameyaficha kwenye  pori kwa ajiri ya kusubilia wateja .
Kamanda Kidavashari alisema mtuhumiwa   anaendelea  kushikiliwa  na  jeshi la Polisi  kwa hatua za  upelelezi  zaidi  ilikuendelea  kubaini  mitandao  yote inayojihusisha  na biashara  hiyo haramu  ya meno ya Tembo na kufikishwa Mahakamani  baada ya upelelezi  kukamilika .
Hivi karibuni watu watatu walikamatwa katika mtaa wa Aiter Mjini hapa  wakiwa na vipande  kumi na mbili vya meno ya Tembo yenye thamani ya shilingi milioni 120 hari hiyo inaonyesha kuwa kuna kasi kubwa ya biashara haramu ya meno ya Tembo Mkoani Katavi 
Na Katavi yetu blog/Blogs za Mikoa

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.