ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 7, 2015

SPORTS LADY ZAINABU 'IKOTA' MHAMILA SASA KWENDA SEKONDARI


SPORTS LADY ZAINABU 'IKOTA' MHAMILA.
Zainabu Ikota Mhamila akipokea zawadi kutoka kwa dada yake Sada Swedy wakati wa mahafari ya 22 ya shule ya msingi msimbazi mseto dar es salaam katikati ni shangazi yake Azania Athumani Mtopa na baba yake Rajabu Mhamila ;super d

Asha Kamnyanga 'mama Ikota' kushoto akimpatias zawadi bint yake Zainabu Mhamila ' Ikota' wakati wa mahafari ya 22 ya shule ya msingi msimbazi mseto Dar es salaam katikasti ni shangazi yake Azania Athumani Mtopa

Asha Kamnyanga 'mama Ikota' kushoto akimpatias zawadi bint yake Zainabu Mhamila ' Ikota' wakati wa mahafari ya 22 ya shule ya msingi msimbazi mseto Dar es salaam katikasti ni shangazi yake Azania Athumani Mtopa
Zainabu Mhamila 'Ikota' akimlisha keki Mama yake Asha Kamnyanga 'Mama Ikota' wakati wa Mahafali ya 22 ya shule ya msingi msimbazi mseto Dar es salaam anaeshudia katikati ni dada yake Sada Swedy.
Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akiwa na bint yake Zainabu Mhamila 'Ikota' wakati wa mahafali ya 22 ya shule ya msingi msimbazi mseto Dar es salaam.
Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu mhamila wa pili kushoto akiwa na baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi msimbazi mseto Dar es salaam wakati wa mahafali ya 22 ya shele hiyo
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi msimbazi mseto wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mahafari ya 22 ya shele hiyo

LOWASSA AIPA UKAWA WABUNGE 116

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu, Damian Lubuva  akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana kuhusiana na uteuzi wa wabunge wa viti maalumu. Picha na Anthony Siame 
By Tumaini Msowoya, Mwananchi
Dar es Salaam. Aliyekuwa mgombea urais wa Chadema aliyeungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa ameupa umoja huo ushindi wa viti 116 vya wabunge katika Bunge la kumi na moja litakaloanza Novemba 17, Mjini Dodoma.
Idadi hiyo ya wabunge ndiyo kubwa kuwahi kufikiwa na upinzani tangu kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 na tangu kufanyika kwa uchaguzi wa kwanza wa ushindani wa vyama mwaka 1995.
Idadi ya wabunge wa Ukawa imeongezeka baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) jana kukamilisha kazi ya kuwateua wabunge wa viti maalumu ambao orodha yake itawasilishwa kwenye vyama husika.
Katika uchaguzi wa mwaka huu uliohusisha majimbo 258 kati ya 262, CCM imeshinda ubunge katika majimbo 188, CUF 35, Chadema 34, NCCR–Mageuzi kiti kimoja. NLD haikupata kiti wakati ACT – Wazalendo ilipata kiti kimoja.
Idadi wa wabunge wa Ukawa inatokana na jumla ya wabunge wa vyama vinavyounda umoja huo ambavyo ni Chadema, CUF na NCCR.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva alisema CCM imepata viti maalumu 64, Chadema 36 na CUF 10.
“Vyama vingine havijapata wabunge wa viti maalumu kwa sababu havikufikisha asilimia tano ya kura za wabunge kwenye majimbo, kwa mujibu wa Katiba,” alisema Jaji Lubuva.
Kwa hesabu hiyo, Chadema imefikisha wabunge 70  kutoka 48 wa mwaka 2010, CUF ina wabunge 45 kutoka 36 wa mwaka 2010 wakati NCCR-Mageuzi imeshuka kutoka wabunge wanne wa 2010 hadi mmoja na kufanya idadi ya wabunge wa Ukawa kuwa jumla 116. CCM imefikisha wabunge 252.
Lubuva alisema jumla ya wabunge wa viti maalumu waliopatikana kwenye vyama vyote ni 110 kati ya 113 wanaotakiwa na watatu wanaosalia watapatikana baada ya kufanyika uchaguzi ambao uliahirishwa kwenye majimbo manane kutokana na sababu za vifo vya wagombea sita na kasoro mbalimbali katika majimbo mawili.
Majimbo ambayo wagombea walifariki dunia ni Masasi, Ludewa, Lushoto, Ulanga Mashariki, Arusha Mjini na Handeni Mjini wakati majimbo yenye kasoro ni Lulindi na Kijitoupele.
Jaji Lubuva alisema CCM imepata idadi hiyo ya wabunge wa viti maalumu baada ya kupata jumla kura 8,333,955 za wabunge, Chadema kura 4,627,923 za wabunge na CUF kura 1,257,955.
Kwa matokeo hayo, vyama 19 kati ya 22 vimeambulia patupu baada ya kupata kura zisizozidi asilimia tano ya kura zote halali za wabunge.
Jaji Lubuva alisema: “Tumetoa matokeo ya wabunge wa viti maalumu baada ya kupewa mamlaka kikatiba ya kutangaza wabunge wa viti maalumu vya wabunge wanawake visivyopungua asilimia 30 ya wabunge wote.”
Alisema kwa mujibu wa uamuzi wa Serikali wa mwaka 2010, idadi ya wabunge wanawake wa viti maalumu iliongezwa na kufikia asilimia 40, ambayo pia imetumika katika uteuzi wa mwaka huu.
“Haya yote ni kwa mujibu wa Ibara ya 66 Kifungu cha (1) na (b) na Ibara ya 78 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ya mwaka 1977, ikisomwa kwa pamoja na Kifungu 86A cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura 343,” alisema Jaji Lubuva.
Kauli za vyama
Akizungumzia matokeo hayo, Kiongozi wa ACT - Wazalendo, Zitto Kabwe alisema chama chake kimefikisha asilimia 4 tu ya kura za wabunge, hivyo hakikutimiza vigezo vya kupata wabunge wa viti maalumu.
“Napenda kupongeza vyama vyote vilivyotimiza takwa la kisheria na hivyo kupata viti vya ubunge. Kwa namna yoyote, ile demokrasia ya Bunge imeimarika kwa idadi ya wabunge wa upinzani kuongezeka,” alisema na kuongeza:
“Sisi ACT – Wazalendo tumepata tunachostahili na kazi iliyo mbele yetu sasa ni kujenga chama kama taasisi imara na kufanya siasa za masuala. Tutatumia kiti kimoja tulichopata na madiwani 50 tuliopata nchi nzima na Manispaa ya Kigoma tutakayoongoza kuhakikisha tunaonyesha tofauti yetu na vyama vingine.”
Kauli ya Chadema
Mkuu wa Mawasiliano wa Chadema, Tumaini Makene alielezwa kushangazwa kwake na NEC kukwepa jukumu la kufanya uteuzi na kutaja majina ya wabunge wateule wa viti maalumu na badala yake kuvisukumia vyama vya siasa kufanya hivyo. Alisema hadi jana jioni, bado majina ya wabunge wa viti hivyo yalikuwa hayajawasilishwa kwenye chama chao.
“Kwa nini NEC wamekwepa jukumu la kufanya uteuzi na kutaja majina ya wabunge wateule wa viti maalumu kisha wanatupia mpira kwa vyama,?” alihoji Makene.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), Magdalena Sakaya alisema ongezeko la wabunge wa Ukawa bungeni litasaidia kuwapo kwa mijadala mizito, kwa ajili ya maendeleo ya Taifa. “Ongezeko la wabunge wa Ukawa litaongeza meno na kuwa na mijadala mizito, kwa sababu wabunge wengi wanao uwezo wa kujenga hoja, kufanya utafiti na wanajua kwa nini wamepewa nafasi hiyo,” alisema. CHANZO MWANANCHI.

Friday, November 6, 2015

RAIS DR. MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA WIZARA YA FEDHA.

 Raisi Dk.Magufuli avamia wizara ya fedha na kukuta baadhi ya wafanyakazi hawapo kazini.
Ifuatayo ni VIDEO ya tukio zima.


PRESS RELEASE: KUAMMY RELEASES MUSIC VIDEO OF “CONDO” FEAT. ICE PRINCE

The afro hip hop artist Kuammy (Afolabi kolade Kuam) repping Kwara State and Lagos releases the music video of his second single “Condo”, featuring Chocolate city’s top artist Ice Prince Zamani. Following the success of his debut single "Show me Your Style"; “Condo” is a bonafide hip hop banger and Kuammy’s strong entrant into the African entertainment scene. Signed to FMV Magic Sound Entertainment Kuammysays, “Condo will take people away from their worries.” The song is a stress reliever and all about partying and having a good time. 

Featuring Ice Prince on his debut release, Kuammy says he relates to Ice’s target market, plus “Ice has conquered Africa and I want to conquer Africa too. What better way than to have someone who has Africa in his pocket already on my song? He killed it though,” Kuammy asserts of the song produced by Kuammy’s Label Producer Illblacki.

HOW TO GET “CONDO”

Watch CONDO on YouTube: http://bit.ly/1kyx3JO
SoundCloud: http://bit.ly/1iHxP65
Condo Custom Download URL: http://bit.ly/1Q8k92m

Kindly find attached “Condo” single and artwork. Share as much as possible within your networks.  

HALMASHAURI YA USHETU KUGAWA PEMBEJEO KWA WAKULIMA

Na Emmanuel Mlelekwa
Novemba 6,2015.
KAHAMA

Kuelekea msimu mpya wa kilimo Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga imewataka wakulima kutumia Pembejeo zinazosambazwa na Mawakala waliothibitishwa na Serikali badala ya kununua  mtaani.

Akizungumza na Jembe Fm Kaimu Afisa Kilimo wa Halmashauri hiyo Mshana Wilson amesema kuwa Serikali imepanga kuboresha kilimo cha Wakulima kwa kuleta Pembejeo bora ambazo zitakuwa na tija kwa wakulima.

Mshana amesema kuwa Wakulima wanatakiwa kutumia Pembejeo  zinazosambazwa na serikali kwa mfumo wa Vocha na tayari usambazwaji wake umeanza kwa utaratibu maalum  kupitia ofisi za kata.

Ameongeza kuwa Halmashauri hiyo  imepata Vocha ya Pembejeo za  Mahindi na Mpunga kwa upande wa mazao ya Chakula, Pamba na Tumbaku kwa upande wa  Biashara pamoja na Mbolea na Madawa ambazo zitagawiwa kwa wakulima.

Hata hivyo takwimu sahihi ya idadi ya wakulima watakaopatiwa Pembejeo hizo bado haijafahamika sanjari na gharama ya vocha ya Pembejeo hhizo kutokana na Mawakala wa usambazaji kutowasilisha nakala  hadi sasa kwa Mkurugenzi.

ENEO LA LEBANON KATIKA SOKO LA KIMATAIFA LA SAMAKI LA FERI JIJINI DAR ES SALAAM NI HATARI KWA UCHUMI, IKULU

Mama Lishe wa soko hilo, Taus Barnabas, akichangia neno katika mkutano huo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Soko la Samaki la Kimataifa la Feri, Ali Kibwana, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi wanaotembelea masoko mbalimbali ya Manispaa ya Ilala kuona jinsi gani vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia umepungua katika soko hilo baada ya Shirika la Equality for Growth (EfG) kutoa mafunzo ya kupinga ukatili katika masoko hayo. Kushoto ni Mwezeshaji wa Sheria katika soko hilo, Bakari Said.
Mwezeshaji wa Sheria katika Soko la Kimataifa la Samaki la Feri, Asha Malenda (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wanaotembelea masoko mbalimbali ya Manispaa ya Ilala kuona jinsi gani vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia umepungua katika soko hilo baada ya Shirika la Equality for Growth (EfG) kutoa mafunzo ya kupinga ukatili katika masoko yaliyopo Manispaa ya Ilala. Kulia ni Mama Lishe wa soko hilo, Taus Barnabas na Fatuma Saijali.
Ofisa Ufuatiliaji na Tathmini wa EfG, Shaban Rulimbiye (kulia), akizungumzia kuhusu mradi huo wa miaka mitatu wa Mpe Riziki si Matusi.

Mwonekano wa sehemu ya soko la Samaki la Feri

Na Dotto Mwaibale

ENEO la Lebanon katika Soko la Kimataifa la Samaki la Feri ambalo lipo jirani na Ikulu jijini Dar es Salaam limedaiwa kuwa ni hatari kwa wafanyabiashara wa soko hilo na kuwa linadhohofisha uchumi kutokana na kukithiri kwa watu wasio rasmi.

Hayo yamebainishwa na Mwezeshaji wa Sheria wa soko hilo, Asha Malenda wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi wanaotembelea masoko mbalimbali ya Manispaa ya Ilala kuona jinsi gani vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia umepungua katika soko hilo baada ya Shirika la Equality for Growth (EfG) kutoa mafunzo ya kupinga ukatili katika masoko hayo.

"Tunachangamoto kubwa sana katika soko letu la Feri tunayoipata kutoka eneo la Lebanon lenye mwingiliano wa watu wasio rasmi kutoka nje ya soko ambao ni kama wamejianzishia soko lao na wamekuwa na maamuzi yao lakini viongozi wa soko la Feri wanashindwa kuwachukulia hatua hali ambayo inatudhalilisha sisi wafanyabiashara hasa mama lishe na kuharibu uchumi wa soko letu" alisema Malenda.

Alisema wengi wa watu waliopo katika eneo hilo lisilo rasmi wamekuwa wakifanya biashara kiholela huku wakipika vyakula katika maeneo yanayoweza kuhatarisha afya ya mlaji wakati katika soko hilo kuna eneo maalumu la mama lishe na wengi wa watu hao wakienda kula eneo hilo rasmi wamekuwa hawalipi fedha na wakibanwa kulipa wanadiliki kutoa visu na silaha za jadi kuwatishia wanaodai.

"Eneo hilo la Lebanon ni hatari na kinachoshangaza linatizamana na Ikulu lakini hakuna hatua yoyote ya makusudi inayochukuliwa na viongozi wetu na linapopelekwa kwa viongozi wa kisiasa wanadai waachwe kwani ndio wapiga kura wao" alisema Mwezeshaji wa Sheria katika soko hilo, Bakari Said.

Said alisema katika soko hilo kuna changoto nyingi za udhalilishaji wanawake kwa kushikwa katika maungo yao lakini kupitia EfG wamejitahidi kupunguza changamoto hizo kwani wasaidizi wa sheria waliopatiwa mafunzo na shirika hilo wanajitahidi kuupenyeza ujuzi waliopata kuifikishia jamii ambayo imeanza kuelewa kuhusu vitendo hivyo.

Aliongeza kuwa uvaaji wa nguo za kubana na kuacha vifua wazi kwa upande wa wanawake pia ulikuwa ukichochea kukithiri kwa vitendo vya udhalilishaji uliokuwa ukifanywa na vijana wasio rasmi katika eneo hilo la Feri ambao hawana makazi na maisha yao yapo Feri lakini baada ya kufikiwa na mafunzo ya EfG hali hiyo imepungua kwa asilimia 80.

Mwezeshaji Fatuma Saijali alisema changamoto kubwa iliyopo hivi sasa katika soko hilo ni kuzuiliwa kupika chakula katika eneo hilo la Feri lakini wakati huo huo kuna kundi la wanawake wamekuwa wakiingiza chakula kutoka majumbano kwao na kukiuza hivyo kuharibu soko lao la chakula.

Mwenyekiti wa Kamati ya Soko hilo, Ali Kibwana alisema mafunzo waliyopata kupitia EfG yamesaidia sana kupunguza vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia katika soko hilo na kila mtu anayebainika kujihusisha na vitendo hivyo amekuwa akiitwa na kukanywa na kama akiendelea kuwa mkaidi anachukuliwa hatua nyingine kwa kufuata kanuni na sheria.

Kamanda wa Ulinzi na Mazingira wa Soko hilo, Nurdin Hassan amesema hali katika soko hilo ni nzuri kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na EfG ya kufanya semina na matamasha ya uhamasishaji hivyo kuifanyajamii kuelewa kuhusu vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia.

Ofisa Ufuatiliaji na Tathmini wa EfG, Shaban Rulimbiye alisema Shirika hilo linaendesha mradi wa miaka mitatu wa Mpe Riziki si Matusi wenye lengo la kutoa elimu ya kupinga ukatili wa vitendo vya ukatili wa kijinsia na udhalilishaji na nia zaidi mradi huo ni kuusambaza hadi katika maeneo mengine ya nchi.

TNRF WAMTAKA MAGUFULI ADHIBITI UPOTEVU WA MALIASILI NCHINI

 Mwenyekiti wa Jumuiko la Maliasili nchini (TNRF) ,Dr.Suma Kaare akizungumza katika mkutano wa 7 wa jumuiko hilo uliofanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na mashirika binafsi pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya maliasili.Picha na Gadiola Emmanuel
  Mkurugenzi wa Shirika la Haki kazi Catalyst Alais Moridant akifafanua jambo  katika mkutano wa 7 wa jumuiko hilo uliofanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na mashirika binafsi pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya maliasili.Picha na Gadiola Emmanuel
  Mkurugenzi wa Shirika la AWF ,John Salehe  akifafanua jambo  katika mkutano wa 7 wa jumuiko hilo uliofanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na mashirika binafsi pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya maliasili.Picha na Gadiola Emmanuel
  Washiriki wa  mkutano wa 7 wa jumuiko la maliasili  uliofanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na mashirika binafsi pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya maliasili.Picha na Gadiola Emmanuel
  Viongozi mbalimbali wa jumuiko la maliasili wakiwa katika mkutano wa 7 wa jumuiko hilo uliofanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na mashirika binafsi pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya maliasili.Picha na Gadiola Emmanuel
 Washiriki wa  mkutano wa 7 wa jumuiko la maliasili  uliofanyika jijini Arusha wakiwa katika picha ya pamoja, ,mkutano huo ulihudhuriwa na mashirika binafsi pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya maliasili.Picha na Gadiola Emmanuel
Washiriki wa  mkutano wa 7 wa jumuiko la maliasili  uliofanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na mashirika binafsi pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya maliasili.Picha na Gadiola Emmanuel 
Washiriki wa  mkutano wa 7 wa jumuiko la maliasili  uliofanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na mashirika binafsi pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya maliasili.Picha na Gadiola Emmanuel 
Mwakilishi wa Shirika la WWF ,Sware Semesi  akizungumza katika  mkutano wa 7 wa jumuiko la maliasili  uliofanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na mashirika binafsi pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya maliasili.Picha na Gadiola Emmanuel 
 Washiriki wa  mkutano wa 7 wa jumuiko la maliasili  uliofanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na mashirika binafsi pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya maliasili.Picha na Gadiola Emmanuel
Wasemaji Wakuu wa   mkutano wa 7 wa jumuiko la maliasili  uliofanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na mashirika binafsi pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya maliasili.Picha na Gadiola Emmanuel 

Na Ferdinand Shayo wa Wazalendo 25 Blog ,Arusha.



Mwenyekiti wa Jumuiko la Maliasili nchini Dr.Suma Kaare amemtaka Raisi John Pombe Magufuli adhibiti upotevu wa mali asili za wanyama pori na misitu uliokithiri katika maeneo mengi nchini ili kunusuru uhai wa maliasili.



Suma Kaare amesema  hayo katika mkutano wa 7 wa jumuiko la maliasili  unaoendelea jijini Arusha,Kaare amesema kuwa jukwaa hilo litashirikiana na Rais huyo katika  kuhakikisha kuwa maliasili zinalindwa na kuwanufaisha Watanzania kwa kiwango stahiki.



“Tunajua Rais wetu mpya ana kazi  kubwa  ya kulinda maliasili za nchi hii kama ilivyo kauli mbiu yake ya “kazi tu” tunaamini atazuia upotevu mkubwa wa rasilimali unaofanywa na watendaji wasio waaminifu” Alisema Kaare



Mratibu wa Masuala ya misitu katika shirika la uhifadhi wa maliasili na Mazingira (wwf) ,Isaac Malungu amesema kuwa asilimia 90% ya nishati inayotumika nchini inatokana na kuni pamoja na mkaa hali ambayo inaathiri misitu na kutishia uhai wa maliasili nchini hivyo ameitaka serikali ihimize matumizi ya nishati mbadala ili kunusuru mazingira yanaoharibiwa kila kukicha.



Malungu alisema kuwa kilimo cha kuhama hama pamoja na ukataji miti ovyo umekua ukisababisha uharibifu wa mazingira na hata kupelekea hecta laki 4 za misitu kupotea kila mwaka kutokana na shughuli hizo.



Mkurugenzi wa  Shirika la AWF,John Salehe Alisema kuwa mabadiliko ya tabia ya nchi yamesababisha hali ya ukame inayowaathiri wanyama pamoja na mimea hivyo kuathiri uhifadhi kwa ujumla .



Salehe alisema kuwa juhudi zaidi zinapaswa kuchukuliwa ikiwemo upandaji wa miti pamoja na kutunza misitu ili kurejesha uoto wa asili uliopotea.

RAIS DKT.MAGUFULI AMWAPISHA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI, IKULU DAR LEO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akisalimina na Makamu wake, Mama Samia Suluhu Hassan, wakati aliwapowasili kwenye Ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam,leo asubuhi Okt. 6, 2015 kwa ajili ya kumwapisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, aliyemteua jana Okt 5, 2015 mara tu baada ya kuapishwa rasmi. Kushoto ni Jaji Mkuu wa Tanzania, Othman Chande. Picha na OMR
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akimwapisha George Masaju, kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali,wakati wa hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo asubuhi Okt. 6, 2015. Picha na OMR
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli (wa tatu kushoto) akiwa na Makamu wake, Mama Samia Suluhu Hassan (wa pili kushoto) Spika wa Bunge Mstaafu, Anne Makinda (kushoto) Jaji Mkuu wa Serikali, Othman Chande (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, baada ya kuapishwa leo wakati wa hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Picha na OMR
Baadhi ya ndigu jamaa na marafiki na watumishi wa Serikali waliohudhuria hafla hiyo ya kuapishwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Picha na OMR
makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan,(kushoto) akizungumza jambo na Jaji Mkuu wa Serikali, Othman Chande (katikati)  wakati wa hafla fupi ya kumwapisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliyofanyika leo Ikulu jijini Dar es Salaam. Picha na OMR