ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, July 22, 2015

KUELEKEA UCHAGUZI 2015 GHAFLA CHADEMA YASISIMUA MWANZA.

Jiji la Mwanza hii leo limesimama kwa dakika kadhaa kupisha shamrashamra za maandamano zilizoambatana na Mkutano wa CHADEMA uliofanyika jijini hapa ukiwa na lengo la kutambulisha baadhi ya wabunge walio hama CCM na kukimbilia chama hicho (Lembeli na Ester Bulaya) sanjari na watu wakitegemea kusikia jina la mgombea kiti cha urais ambaye awali alitajwa kuwa angetambulishwa kupitia mkutano huo.

Mamia ya wanachama na wafuasi wa chama hicho wamehudhuria mkutano uliofanyika kwenye uwanja wa Magomeni kirumba jijini Mwanza kisha baadaye kwa maandamano wakawasindikiza viongozi wao hadi hoteli walizofikia.

Umati unaoonekana hapo juu 'kideoni' ni kutoka hoteli ya Gold Crest ukiwasindikiza viongozi walio fikia hotelini hapo.
Katibu mkuu wa CHADEMA W. Slaa akihutubia makumi kwa mamia ya wananchi na wanachama waliojitokeza leo kwenye viwanja vya Magomeni \kurumba jijini Mwanza.
Ze nyomi kwa area.
Katibu mkuu wa CHADEMA W. Slaa akihutubia makumi kwa mamia ya wananchi na wanachama waliojitokeza leo kwenye viwanja vya Magomeni \kurumba jijini Mwanza.
Mwenyekiti wa Chama cha maendeleo na Demokrasia nchini (CHADEMA) Mbowe akihutubia makumi kwa mamia ya wananchi na wanachama waliojitokeza leo kwenye viwanja vya Magomeni kurumba jijini Mwanza.
Salum Mwalimu.
Mkutano huo pia uliwatambulisha wabunge walio hama CCM na kukimbilia chama hicho Ester Bulaya na Mbunge wa Kahama Mhe. Lembeli ambao walirudisha kadi zao na kukabidhiwa kadi mpya za CHADEMA.
Ester Bulaya na Lembeli wakikabidhiwa kadi zao.
Haya wamezaliwa upya ndani ya CHADEMA ni Ester Bulaya na Lembeli.
Hata hivyo bado ni kitendawili kuhusu mgombea wa urais kwa kiketi ya UKAWA kupitia muungano wa vyama vya upinzania ambavo ni Chadema, NCCR-Mageuzi, CUF na NLD angetangazwa, lakini hakuna aliyetangazwa. 

Hadi sasa tarehe za kumtangaza mgombea huyo zimerushwa zaidi ya mara mbili huku mvutano ikiendelea ndani ya vyama hivyo. Gumzo lililopo je ni chama gani kitamtoa rais na mgombea mwenza?, Je mgawanyo wa ruzuku mwisho wa siku utakuwa?

UZINDUZI WA KAMPENI YA AWAMU YA PILI YA WAZAZI NIPENDENI WAFANYIKA DAR ES SALAAM LEO

Mkurugenzi wa Kitengo cha Ubora wa Huduma za Afya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Ali Mohamed Ali (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati akitoa tamko kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Donan Mmbando katika uzinduzi wa kampeni ya awamu ya pili ya wazazi nipendeni uliofanyika Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Afya ya Uzazi na Mtoto Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Georgina Msemo na Mshauri wa Kiufundi wa Malaria kutoka  Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID)
 Ofisa Uzazi Salama,  Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Heavengton Mshiu (kulia), akizungumza katika uzinduzi huo.
Mshauri wa Masuala ya Afya ya Uzazi wa Taasisi ya Center for Comminication Programs Johnns HopKins University, Dk,.Rosemarie Madinda (kulia), akizungumza katika uzinduzi huo. Taasisi hiyo ndiyo inayoendesha kampeni hiyo.
Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Afya ya Uzazi na Mtoto Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Georgina Msemo (kulia), akizungumza kwenye uzinduzi huo.
Mwongozaji wa uzinduzi huo akiendelea na kazi.
Wanahabari wakiwa kwenye shughuli hiyo.

Ofisa Uzazi Salama,  Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Heavengton Mshiu (kushoto), akimpongeza  Mkurugenzi wa Kitengo cha Ubora wa Huduma za Afya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Ali Mohamed Ali, baada ya kutoa tamko la Wizara hiyo katika uzinduzi huo.
Mwanamuziki Nyoshi Al-Saadat wa Bendi ya Muziki wa Dansi ya FM Academia "Wana wa Ngwasuma" itakayotoa burudani katika maonyesho mbalimbali yatakayokwenda sanjari na uzinduzi huo yatakayofanyika kuanzia kesho viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es Salaam kuanzia kesho, akizungumza katika uzinduzi huo utakaopambwa na burudani za kumwaga.

Na Dotto Mwaibale

SERIKALI imesema imepiga hatua katika kupunguza vifo vya watoto waliochini ya miaka mitano toka 157 mwaka 1990 hadi kufikia 54 kwa mwaka 2013.

Hayo yalibainishwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ubora wa Huduma za Afya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Ali Mohamed Ali wakati akitoa tamko kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Donan Mmbando katika uzinduzi wa kampeni ya awamu ya pili ya wazazi nipendeni uliofanyika Dar es Salaam leo

Alisema kati yua watoto hai 1,000 wanaozaliwa na kufikia lengo la Melenia (MDG) 4 waliojiwekea kufikia mwisho wa mwaka huu Disemba 2015.

"Pamoja na mafanikio hayo bado hari si shwari kwa upande wa vifo vinavyotokana na uzazi kwani vimepungua kutoka 770 mwaka 1990 na kufikia 410 kwa mwaka 2014 kwa kila vizazi hai 100,000 tofauti na lengo tulilojiwekea kufikia Disema 2015 kuwa vipungue kufikia 193 kwa kila vizazi hai 100,000" alisema Dk.Ali.

Alisema Kampeni ya Wazazi Nipendeni awamu ya kwanza ilitengenezwa na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na msaada toka watu wa Marekani kupitia taasisi ya USAID, Mfuko wa Malaria wa Rais wa Marekani na taasisi ya Kukinga na kuzuia Magonjwa.

Dk. Ali alisema programu hiyo ilihusisha kutuma ujumbe uliolenga kuimarisha afya ya mjamzito na mtoto na kuwa ilizinduliwa hapa nchini jijini Mwanza kwa mara ya kwanza mwezi Novemba, 2012.

Alisema katika kampeni hiyo ya masuala ya afya na ustawi wa jamii vyombo vyote vya habari ni muhimu zaidi kuhabarisha na kuwa ujumbe mfupi wa simu za kiganjani wenye taarifa anwai zitakuwa zinatumwa wakati wowote wa ujauzito mpaka mwaka mmoja baada ya kujifungua.

Aliongeza kuwa ili kujiunga mhusika, ndugu, jirani au rafiki atatuma ujumbe "mtoto" kwenda namba 15001 jambo litakalosaidia kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi, mtoto mchanga na mtoto alie chini ya miaka mitano.

Alisema uzinduzi wa kampeni hiyo unakwenda sanjari na maonyesho mbalimbali, upimaji wa damu, masuala ya huduma ya VVU na Ukimwi yatakayoanza leo asubuhi viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es Salaam.

Dk. Ali alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam na mingine hasa wanaume na wanawake kufika kwenye maonyesho hayo kupata huduma za afya ya uzazi ambayo yataambatana na burudani za muziki kutoka bendi za Wanaume Familia, Ngwasuma, Wanaume Halisi na nyingine nyingi.

ZIARA YA OBAMA NCHINI KENYA NI GUMZO SASA HADI KITAA


If Obama was Kenyan.
Calls Uhunye...
Obama: Man, I need to tell you something
Uhunye: Niaje mzito, Ehe sema...
Obama: And please don't be mad
Uhunye: Weee niambie aki
Obama: I just remembered I have a meeting on Friday
Uhunye: Hauko serious...
Obama: I will still come
Uhunye: Aaaah weee maaani.
Obama: I promise I will pass by.
Uhunye: Utapitia ama Utakam?
Obama: Will Ruto be there?
Uhunye: Ziiiii Ziiii hatakuwa.
Obama: Are you sure?
Uhunye: Eeeeh hatakuwa, double sure, ata nimempea leave saa hii like 5 minutes ago.
Obama: Ok, I really wanted to talk to him
Uhunye: Ako apa mtaongea na yeye?
Obama: On friday, not now
Uhunye: Atakuwa. Utakam saa ngapi?
Obama: 1PM i will be there
Uhunye: Atakuwa from 6AM
Obama: Hopefully i will be there
Uhunye: Weee niambie ama unakuja ama hukuji
Obama: Hey stop the altitude
Uhunye: Ok, ok, Am very sorry, are you coming yes or no
Obama: I will tell you
Uhunye: Sawa, lakini utakam?
Obama: Let me call you back
Uhunye: After how long?
Obama: Evening
Uhunye: Ngai
Obama: I will call you
Uhunye: Ok niseme upikiwe ama usipikiwe friday
Obama: I will tell you
Uhunye: So Wapike?
Obama: I will tell you.
Uhunye: Ok, ama wasipike, ndio tusijiwaste
Obama: Ok, tell them to hold on first
Uhunye: So haukuji?
Obama: I might be late
Uhunye: Meeting itakuwa wapi nikupick?
Obama: Moscow
Uhunye: Uko ni far, Uko sure huezi kam alafu uende meeting?
Obama: Putin says its urgent
Uhunye: Bado mnaongeanga na huyo jamaa, yani. Wee kuja, huyo jamaa hakuwangi mpoa
Obama: I will call you. [Hangs up.]
Uhunye Calls Putin
Uhunye: Sema Bro
Putin: Am Good man
Uhunye: Nikuulize mnameet na Obama Friday ama ananienjoy...
Putin: Zi, kwani amekushow?
Uhunye: Poa. Thanks [Hangs up.]
Uhunye Calls Obama
Obama: Hello
Uhunye: Putin ameniambia hamuna meeting Friday...

CHADEMA WATINGA MWANZA ESTER BULAYA, LEMBELI NDANI

Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa, akipungia mkono wananchi wa jijini Mwanza waliojitokeza hii leo kumlaki tokea airport hadi kwenye mkutano viwanja vya Magomeni Kirumba.
MAELEZO: HISANI YA MWANANCHI
BAADA ya vuta vikuvute ya muda mrefu, hatimaye leo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinatarajia kumtangaza mgombea wake wa urais katika mkutano maalumu utakaofanyika jijini Mwanza.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na viongozi wa chama hicho Kanda ya Ziwa Magharibi na makao makuu zilisema kuwa leo mgombea huyo atatangazwa mkoani hapa huku zikibainisha kuwa anayepewa nafasi kubwa ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa.
Taarifa hizo zimekuja wakati kukiwa na tetesi kuwa chama hicho kilikuwa kinafanya mazungumzo na waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa aliyekuwa anawania urais kupitia CCM na kutemwa katika hatua za awali, huku vyanzo mbalimbali vikisema mazungumzo hayo yanachukua muda mrefu na kuna uwezekano mkubwa wa kutozaa matunda.
Jana, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe pamoja na baadhi ya wabunge walikaririwa wakitoa matamko ya kumkaribisha Lowassa kuingia Chadema lakini kwa sharti la kufuata kanuni na taratibu za chama hicho, lakini Dk Slaa alisita kumzungumzia kiongozi huyo akiahidi kuzungumza mambo yatakapokuwa sawa.
Mratibu wa Operesheni za Chadema Kanda ya Ziwa Magharibi, Tungaraza Njugu alisema mgombea huyo (bila kumtaja jina), atatangazwa katika mkutano wa hadhara utakaofanyika kwenye Viwanja vya Magomeni, Ilemela kuanzia saa nane mchana.
Njugu alisema katika mkutano huo, viongozi wakuu wa Ukawa wanatarajia kuwapo na maandalizi yake yamekamilika.
“Kesho (leo) tutakuwa na mkutano mkubwa kwenye viwanja vya Magomeni,” alisema Njugu na kuongeza: “Mgombea urais kupitia Ukawa atajulikana hapo, kwani tunatarajia viongozi wakuu wa Ukawa watamtangaza.”
Katika mazingira tofauti, akihutubia mkutano wa hadhara mjini Geita juzi, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alidokeza jina la Dk Slaa kama mgombea urais wa chama hicho, kitendo kilichoibua hamasa na umati kumshangilia, lakini akawapoza akisema ulimi umeteleza.
Alipoulizwa kuhusu mkutano huo, Mwenyekiti wa NLD, Dk Emmanuel Makaidi alikiri kuwa leo kulikuwa na mpango wa kumtangaza mgombea wa Ukawa, lakini alidhani ingekuwa Dar es Salaam, hivyo kwa kuwa wameamua iwe Mwanza angefanya utaratibu wa ndege ili aweze kuwahi.
Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia hakupatikana kuzungumzia mkutano huo, lakini Katibu Mkuu wa chama hicho, Mosena Nyambabe alisema hakuwa na taarifa hizo, hasa kwa kuwa vikao vya mwisho vilivyofanyika Jumapili na Jumatatu vilihusisha wenyeviti wa vyama pekee.
Kiwia Ilemela (kushoto) Wenje Nyamagana (kulia) wote kugombea kupitia CHADEMA.
Hata hivyo, alisema ilibidi mgombea huyo atangazwe ama jana au leo. Chama cha CUF kimekwishatangaza kuwa kinasubiri uamuzi wa kikao cha Baraza Kuu la Uongozi litakaloketi Julai 25 kuamua juu ya hatima yake ndani ya Ukawa.
Alipotakiwa kudokeza ni nani atasimama kuwakilisha Ukawa, Njugu alisema jukumu hilo ni la viongozi wa juu na kwamba yeye akiwa kiongozi wa Kanda anatambua mgombea urais wa Ukawa atatangaziwa Mwanza leo.
Lissu arusha watu roho Geita
Akihutubia mkutano wa hadhara juzi, Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki alisema mgombea wa Ukawa anafahamika ndani na nje ya nchi na kinachosubiriwa ni kutangaza jina lake baada ya taratibu kukamilika akisisitiza kwamba chama hicho hakitashindwa kwa goli la mkono.
Aliwaambia wananchi wa Mji wa Geita waliokuwa wamefurika kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Nyankumbu kuwa Ukawa wamechelewa kumtangaza mgombea huyo kutokana na kuchelewa kupatikana mgombea mweza kutoka Zanzibar.
“Ndugu wananchi mgombea wa Ukawa nimtaje, nisimtaje,” aliwauliza wananchi waliofurika kwenye mkutano huo, nao wakaitikia, “mtajeee”
“Tumeshampata mgombea urais wa Ukawa na mnampenda sana na mnamjua sana.

Ni mtu anayefahamika nchi nzima na duniani kote,” alisema Lissu huku akishangiliwa na wananchi.
Huku wananchi wakiwa na shauku ya kujua jina la mgombea, Lissu alisema baada ya taratibu za kumpata mgombea mwenza kukamilika, mgombea huyo atatangazwa.
“Siku tunamtangaza mtajua tu, tutaita vyombo vyote vya habari ili kumtangaza kwa hiyo mtamjua,” alisema Lissu.
Wakati Lissu akitoa ufafanuzi huo, alijikuta akitaja jina la Dk Slaa na kusababisha umati uliokuwa umefurika uwanjani hapo kushangilia.
“Kuna mambo yametuchelewesha, lakini wakati tunashughulika kumtangaza Dk Slaa... Wananchi (wakalipuka kushangilia)..., Lissu akaendelea, “Samahani ulimi hauna mfupa, samahani sana naomba mniwie radhi jamani…jamani, jamani, tulieni.”
Alisema umoja huo bado una presha kubwa kuhusu kutaja jina la mgombea na kuwa wapo baadhi ya viongozi wa Serikali na vyama hasimu ambao wanaombea Ukawa iparaganyike.
“Wapo wanaotuombea mabaya Ukawa na wengine wanapewa fedha ili kuhakikisha Ukawa inavunjika.

Kamwe Ukawa haitavunjika. Ninawahakikishia wananchi kwamba Ukawa iko imara na haitavunjika hata wakituombea mabaya,” alisema Lissu.
Amtaja Dk Magufuli
Akimzungumzia mgombea wa CCM, Dk John Magufuli, Lissu alisema Ukawa haitishiki naye kwa sababu hajawahi kuzungumzia kero zinazowakabiliwa wananchi, yakiwamo mateso yaliyowapata wafugaji baada ya ng’ombe wao kuuawa na wengine kuteswa wakati wa Operesheni Tokomeza.
Alisema tangu kuibuka kwa tuhuma mbalimbali dhidi ya Serikali iliyopo madarakani likiwamo sakata la Richmond na Tegeta Escrow, Dk Magufuli hajawahi kusimama na kuutangazia umma nini msimamo wake kuhusiana na kashfa hizo.
Bulaya atajwa Chadema
Mkutano huo utakaorushwa moja kwa moja katika televisheni, pia unatarajia kumpokea Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya aliyetangaza kukihama chama hicho juzi bila kuweka wazi anakohamia.
Hata hivyo, mbunge huyo ambaye tayari ameweka wazi kupitia ukurasa wake wa Facebook kuwa atawania ubunge katika Jimbo la Bunda Mjini, amekaririwa na gazeti hili akisema hatima yake itakuwa hadharani leo.
Mbunge wa Kahama (CCM), James Lembeli akiwa kwenye msafara ndani ya gari la wazi.
Lembeli rasmi Chadema
Mbunge wa Kahama (CCM), James Lembeli jana alihitimisha uvumi kuwa angehamia Chadema baada ya kutangaza rasmi kujiunga na chama hicho na papo hapo akatangaza kulitetea jimbo hilo kupitia chama hicho cha upinzani.
Lembeli (58), ambaye pia anatarajiwa kutambulishwa rasmi katika mkutano wa Mwanza, aliwaambia wanahabari Dar es Salaam jana kuwa amekihama chama tawala baada ya kushindwa kuvumilia fitna na rushwa.
“Nimekaa, nimetafakari, nimezungumza na mama yangu kwa muda wa zaidi ya saa 10, mke wangu na watoto na kwa kusikia kilio cha wananchi wa jimbo la zamani la Kahama nimeamua yafuatayo; kwanza ni kujiondoa uanachama wangu ndani CCM.
“Sikupenda ila nimelazimika kuchukua uamuzi huu, najua umewauma wengi na kuwakera wengi lakini nawaomba nao waangalie hali ya viongozi wa wilaya wa Kahama waliosababisha hayo… ni uamuzi mgumu sikupenda iwe hivyo na pili, kuanzia leo najiunga na Chadema,” alisema Lembeli aliyeambatana na binti yake ambaye pia alijiunga nacho.
Mbunge huyo aliyeitumikia CCM katika nafasi hiyo kwa miaka 10, aliwataka wananchi wa Jimbo jipya la Ushetu alikozaliwa kutovunjika moyo na kuunga mkono safari yake mpya akiahidi kuwa atakuwa nao bega kwa bega kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Alipoulizwa kwa nini aliamua kuhamia Chadema na siyo vyama vingine vya upinzani, Lembeli alisema ni chama cha pili kwa nguvu na kina mtandao nchini, hivyo asingependa kuhamia chama ambacho angeanza upya safari yake ya kisiasa.
“Mimi nimeonyesha nia kutoka rohoni ya kuhamia Chadema, nitapitia mchakato wote wa kumtafuta mgombea ili nipate ridhaa ya kupererusha bendera ya chama hicho na nina uhakika kwa Kahama kwa asilimia 100 nitapita… iwapo nitafeli mimi sina mpango mbadala na nimeshajiunga Chadema mpaka mwisho,” alisema.
Si mtandao wa Lowassa
Huku akizungumza kwa umakini, Lembeli alisema Watanzania wanapaswa kufahamu kuwa yeye si miongoni mwa makada wanaoihama CCM kutokana na kukatwa kwa Lowassa, bali kutokana na rushwa iliyokithiri, hivyo hatua hiyo (ya kukimbia rushwa), itamsaidia kukwepa fedheha.








Tuesday, July 21, 2015

SLAA Vs LOWASSA CHADEMA...??

YAFUATAYO NI MAZUNGUMZO YA WANA WA JUKWAA LA WANA MABADILIKO WANAVYOJADILI:-

MSEMAJI NO. 1
Kunazidi kucha huko kwa wahafidhina....magazeti ya leo yanafunua kile ambacho tumekuwa tunasema....Slaa bado peke yake anakataa ujio wa Lowassa chadema.....ametishia kurudisha kadi ya chadema iwapo mpango wa chama kumpokea Lowassa na kumpa ugombea urais utaendelea.......
 Ngona tuone hii itaishia wapi?...


MSEMAJI NO. 2
Amini amini nawaambieni, kuna ukweli mkubwa tu kwenye hili na wala halikuanza leo. lilianza muda mrefu tu sasa linafukuta. Hamna awezaye kulipinga hapa kwa wale wandani ya chama.  Slaa km kweli ni mpambanaji likitokea na arudishe kadi maana hamna jinsi nyingine, mtu timamu huwezi
kula matapishi.


MSEMAJI NO. 3
Hivi wa TZ tukoje?
Kwa nini tusingoje kupewa ukweli na wahusika, tunabaki na hisia tu, tukiamini habai za magazeti? 


CCM ni chama kimoja, lakini tumeona changamoto zinazowakumba, itakuwa vyama vinne? Magazeti mengi yamekuwa yanajiandikia tu; mara hili linaandika hiki, lile linakanusha; mnawezaje kuamini maandishi haya? 
 

Kwa nini tusisubiri, maana liwalo liwe, ukweli utajitokeza tu! Hivyo hakuna sababu ya ku-speculate!

MSEMAJI NO. 4
Hakuna kitu hatari kama ku corrupt media na kuwa na watu kama Ludo katika jamii wanaotutesa sasa hivi muda si mrefu watasikia kutoka kwetu.

Kichwa cha wendawazimu, kila kinyozi anataka aonyeshe staili yake. Wale wanajifunza na wale ambao ni hawajui kabisa!!!

MSEMAJI NO. 5
Kama sababu ya mtu au kikundi cha watu kuhama chama kimoja cha siasa kwenda chama kingine ni kutafuta kupata cheo peke yake, na siyo kushinikiza mabadiliko yenye tija kwa watanzania wote, uchaguzi utakuwa  hauna manufaa makubwa kwa nchi.

AIRTEL WAKABIDHI JEZI KWA TIMU ZITAKAZOSHIRIKI MICHUANO YA AIRTEL RISING Stars.

Mwenyekiti kamati ya soka la vijana katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),Ayubu Njenza (kushoto) akimkabidhi vifaa vya michezo katibu wa chama cha mpira wa miguu Wilaya ya Kinondoni,Isaac Mazwile kwaajili ya mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars, inayoanza tarehe 24 Julai mkoani Mbeya. katikati ni Afisa Uhusiano Airtel,Jane Matinde. Makabidhiano hayo yalifanyika leo jijini Dar-es-Salaam.
Mwenyekiti kamati ya soka la vijana katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),Ayubu Njenza (kushoto) akimkabidhi vifaa vya michezo katibu wa chama cha mpira wa miguu Wilaya ya Ilala Kanuti Daudi kwaajili ya mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars katikati ni Afisa Uhusiano Airtel Jane Matinde. Makabidhiano hayo yalifanyika leo jijini Dar-es-Salaam.
Mwenyekiti kamati ya soka la vijana katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),Ayubu Nyenza akiongea wakati kupokea vifaa vya michezo ya Airtel Rising Stars kutoka kwa kampuni ya simu za mikononi ya Airtel , Kulia Afisa Uhusiano Airtel,Jane Matinde kushoto ni Afisa Maendeleo wa TFF bwana Jemadari.
Mwenyekiti kamati ya soka la vijana katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),Ayubu (katikati kushoto), Afisa Uhusiano Airtel, Jane Matinde, katibu wa chama cha mpira wa miguu Wilaya ya Kinondoni,Isaac Mazwile kulia na Afisa Maendeleo wa TFF bwana Jemadari kwa pamoja wakionyesha vifaa vya michezo vitakavyotumika wakati wa michuano ya Airtel Rising Stars.
AIRTEL  jana ilikabithi vifaa kwa timu zote zitakazoshiriki michuano ya Airtel Rising Stars kwa mwaka huu. IMG 3184 Afisa Uhusiano Airtel, Jane Matinde akimkabithi vifaa vya michezo Mwenyekiti kamati ya soka la vijana katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ayubu Nyenza kwaajili ya mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars, inayotegemea kutimu vumbi kuanzia Ijumaa, Julai 24, 2015 mkoani Mbeya. 

Airtel wakabidhi jezi kwa timu za U-17 Dar es Salaam, Jumatatu Julai 20 2015….Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imekabidhi jezi kwa timu za wasichana na wavulana za U-17 zinazoshiriki michuano ya Airtel Rising Stars ambayo inatarajiwa kuanza katika ngazi ya mkoa Ijumaa, Julai 24. 

Mkoa wa Dar es Salam unajumuisha mikoa ya kisoka ya Ilala, Kinondoni na Temeke huku timu nyingine zikitoka mikoa ya Morogoro, Mbeya, Arusha na Mwanza. 

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa makabidhiano hayo yaliyofanyika katika uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya soka la Vijana ya TFF Ayoub Nyenzi alisema kwamba maandalizi yote kwa ajili ya michuano hiyo ngazi za mikoa yamekamilika.
 “Ni matarajio yetu kuwa tutashuhudia mechi zilizojaa ushindani na mvuto na vilevile ningependa kuona mamlaka zinazohusika na usimamizi wa michuano hiyo ngazi ya mkoa zikichagua wachezaji bora ambao wataunda timu za kombaini za mikoa tayari kwa kushiriki fainali hizo ngazi ya taifa zitazofanyika jijini Dar es Salaam baadaye mwezi Septemba”,alisema. 

Mkoa wa Mbeya utakuwa wa kwanza kuzindua mashindano yake Julai 24, ikifuatiwa na mkoa wa Dar es Salaam Julai 27, Morogoro Agusti 1 na Arusha Agusti 9, huku Mwanza wakitarajia kufanya uzinduzi wao mnamo Agusti 15. 

Wageni rasmi katika hafla za uzinduzi wa mikoa wanatarajiwa kuwa wakuu wa mikoa husika. Mikoa yote shiriki inatarajiwa kuwa na timu za wavulana na wasichana isipokuwa mkoa wa Arusha ambao unatoa timu ya wasichana pekee na Morogoro inayoshirikisha wavulana tu. 

Huu ni mwaka wa tano mfululizo ambao michuano hii imekuwa ikifanyika nchini, huku ikichangia kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa vipaji vyenye manufaa kwa Taifa. Ofisa Uhusiano wa Airtel Tanzania Jane Matinde, ameelezea nia ya dhati ya kampuni yake kuendelea kudhamini programu za vijana huku akiomba sapoti kutoka kwa TFF, Wizara inayoshughulikia masuala ya michezo pamoja na wadau wengine wa mchezo wa soka. 

Alisema Airtel Rising Stars mwaka huu inaenda bega kwa bega na kampeni mpya ya ‘It’s Now’ huku nahodha wa Ivory Coast ambaye pia ni kiungo wa Manchester City Yaya Toure akiongoza kampeni hiyo. 

Kampeni hii inalenga kulea na kukuza vipaji barani Afrika kupitia nyanja mbalimbali kama vile michezo, mtindo wa maisha na mziki lakini vilevile kuwapa mbinu zitazaowawezesha kupata ufumbuzi wa masuala ya kiteknolojia na kuona fursa zinazowazunguka. 

Airtel Rising Stars ni program ambayo ipo bara zima la Afrika maalum kwa ajili kuwapa vijana fursa ya kuonesha vipaji vyao na kuwarahisishia makocha kupata vijana ambao watawaendeleza vipaji vyao kwa manufaa ya baadaye.

BREEKING NEWS: MBUNGE WA KAHAMA, JAMES DAVID LEMBELI AONDOKA CCM NA KUJIUNGA RASMI NA CHADEMA


Aliyekuwa Mbunge wa Kahama kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), James David Lembeli (kushoto) akiingia ukumbi wa Hoteli ya Blue Pearl Ubungo Dar es Salaam leo asubuhi akiwa ameongozana na mtoto wake, Wizilya Lembeli wakati akienda kutangaza kuondoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kahama mkoani Shinyanga, James David Lembeli, akizungumza na waandishi wa habari Hoteli ya Blue Pearl Ubungo Dar es Salaam leo asubuhi wakati akitangaza kuondoka katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Pamoja na kutangaza nia ya kugombea ubunge kupitia chama hicho.
Lembeli akizungumza na wanahabari.
Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.
 Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.
Wanahabari wakimsikiliza Lembeli. Suleiman Msuya

Na Mwandishi Wetu

ALIYEKUWA Mbunge wa Kahama James Lembeli, amehamia rasmi Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), akitokea Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Tukio hilo la kuhama lilifanyika jijini Dar es Salaam leo asubuhi katika Hoteli ya Blue Pearl, Ubungo Plaza ambapo aliambatana na mwanae ambaye alijitambulisha kwa jina Wizilya James.

Akizungumzia uamuzi wake huo Lembeli alisema amekuwa ndani ya CCM kwa miaka yake yote lakini kutokana na vitendo vinavyofanyika ndani ya chama hicho ameaona akae pembeni.

Lembeli alisema, ndani ya CCM ili ufanikiwe kupita michakato yote sahihi ni lazima utoe rushwa au kuiba kura jambo ambalo yeye analipiga vita hivyo kutofautiana na viongozi wa chama ngazi ya Wilaya.

"Ndani ya CCM rushwa imekuwa ibada inasumu kali kuliko ukimwi hivyo nimeshindwa kuvumilia naona Chadema wana viashiria vinavyofanana na mimi ngoja tukafanye kazi," alisema Lembeli.

Alisema katika harakati za kupata wagombea katika jimbo la Kahama kila mwaka ni lazima rushwa itumike lakini chama kimekuwa kimya na kuwabeba wale watoa rushwa.

Mbunge huyo alisema ushahidi wa watu kutoa rushwa hasa katika kipindi hiki umeonekana lakini wahusika wameendelea na hatua zingine bila kukemewa.

"Mimi mwaka 2010 nilikuwa nimekatwa lakini huruma ya Rais Jakaya Kikwete nilirejeshwa sasa nimeona hakuna sababu ya kuendelea kulazimisha kama viongozi hawakutaki," alisema.

Alisema iwapo angechukua fomu CCM mkakati ambao ulikuwepo ni kumkata kwa kile ambacho wanaamini kuwa amekuwa akisimamia misimamo ambayo ina madhara kwa Serikali.

Lembele alisema kutokana na dhana hiyo ni vema aende katika chama ambacho kinaonekana kuwa wabunge wake wanauchungu na nchi yao na sio kubebana kusiko na sababu.

"Kufanya kosa sio kosa lakini kurudia kosa ni kosa kubwa sana hivyo siwezi kurudia kosa la 2010 hivyo huku Chadema ndiko sahihi," alisema.

Alisema ukiona mwenzako ananyolewa ni vema kujiandaa kwa kutia maji nywele jambo ambalo ameliona na ameamua kufanya hivyo.

"Siwezi kutoa rushwa kwa sababu sijafunzwa hivyo na hata wananchi wa Kahama wanajua kuwa mimi sio mtoa rushwa hivyo ukiwa hutoi rushwa CCM ni ngumu kukubalika jambo ambalo linafanya kuwa rushwa iwe mbaya kuliko ukimwi," aliongezea.

Akizungumzia kugombea ubunge kupitia Chadema, alisema atafanya hivyo kwani ukweli ni kuwa anakubalika kwa wananchi wote kutokana na misingi yake ya utumishi.

Alisema mpaka anafanya uamuzi huo ameshafanya utafiti ambapo anaamini kuwa atashinda tena kwa kishindo kwani wananchi wa jimbo hilo wanamkubali.

Lembeli alisema kimsingi jimbo la Kahama wapinzani wapo tangu yeye akiwa Mbunge, hivyo anaamini kuwa iwapo atafanikiwa kushinda hatapata wakati mgumu kufanya kazi.

"CCM imefanya mambo mengi ambayo kimsingi hayana afya ndani ya chama ukiwa wa kwanza kwa kura ndani ya CCM unakuwa wa mwisho hali ambayo inakatisha tamaa na hilo lilitokea 2010 na Chadema wakapata ushindi," alisema

Pia alisema amepokea simu na meseji nyingi ambazo kutoka kwa wananchi zinamtaka agombee kupitia chama Chadema hivyo pamoja na ukweli kuwa ni uamuzi mgumu ila hawezi kula matapishi.

Alisema ilimchukua masaa 10 kumuelezea mama yake juu ya uamuzi huo lakini baadae alielewa hivyo kwa sasa ana baraka zote za mama na familia kwa ujumla.

Kuhusu uhusiano na 4U Movement

Akizungumzia kuhusu uamuzi huo kuhusishwa na kundi la 4u Movement, alisema kimsingi kundi hilo analiona kupitia mitandoa ya kijamii ila hana uhusiano nalo na hahitaji kuwa katika hao.

Lembeli alisema wananchi wa Kahama ni watu makini wanajua nini cha kufanya hivyo uamuzi ambao watafanya utakuwa ni kwa uelewa wao na sio kwa msukumo wa kundi hilo linalotajwa kuwa ni wafuasi wa Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa.

Kuhusu Katiba iliyopendekezwa Lembeli alisema yeye ni muumini wa Serikali tatu na alionesha hilo katika vikoa vyote vya bunge lile ambapo alikuwa katika kamati namba moja.

Alisema kutokana na ukweli huo ni dhahiri kuwa ameenda chama ambacho wanafanana kifra kwani bila Serikali tatu hatma ya Tanzania itakuwa mashakani.

"Kwa hili siwezi kubadilika mimi msimamo wangu hadi leo ni Serikali tatu ambapo pia ni msimamo wa Chadema hivyo wengi ndio walishinda lakini mimi sio mmojawapo," alisema.

Aidha Lembeli alitumia muda huo kufafanua ni kwanini alitoa hoja ya kutaka Lowassa na wengine ambao wamekutana na majanga ndani ya bunge wasafishwe ambapo alisema haki haikutendeka kusafisha watu baadhi na wengine kuachwa.

Lembeli alisema katika taarifa ya Operasheni Tokomeza haikusema mawaziri fulani wanamakosa ila iliweka bayana kuwa kulinga na nafasi zao wanapaswa kuwajibika kisiasa.

Alisema mfumo wa kusafisha watu fulani na wengine kuwaacha sio mzuri kwani hauendani na misingi ya haki za binadamu ni ubaguzi.


Kwa upande wa mtoto wake wa pili Wizilya James Lembeli alisema wanamuunga mkono baba yao kwa uamuzi huo na kuwa wako nyuma yake.

Alisema uamuzi ambao amechukua baba yake ni mgumu hasa ukilinganisha na kipindi husika lakini hakuwa na njia nyingine kwani ni mtu wa siasa.

Akizungumzia ujio huo Ofisa Habari wa Chadema ambaye ndiye alimpokea Lembeli alisema kimsingi mwanachama huyo mpya alikiwa ni mpinzani kiroho hivyo hawana shaka naye.

Makene alisema wanaamini kuwa wamepata mtu ambaye anapenda mabadiliko kwani alionekana ndani ya bunge na nje kwa kusimamia rasilimali za nchi bila uoga.

Alisema Chadema itaendelea kupokea wanachama wapya kutoa CCM na vyama vingine hadi Julai 25 kwani lengo lao ni kuhakikisha kuwa nchi inafikia kwenye mabadiliko chanya.

Lembeli amekuwa Mbunge wa jimbo la Kahama, tangu mwaka 2005 hadi 2015 ambapo awali alikuwa  mwandishi na mtumishi katika shirika la Hifashi ya Taifa (Tanapa).

WATUMISHI WA UMMA WAASWA KUWA WAADILIFU

Kaimu Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Jasper Mero (Mbele) akiingia katika ukumbi wa Kings way kufungua mafunzo ya awali (Induction course) kwa waajiriwa wapya wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi yanayofanyika katika Hoteli ya Kings Way Mkoani Morogoro.
Mkurugenzi Msadizi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Bibi Eliaika Manyanga (Kulia) akizungumza na waajiriwa wapya wa Ofisi hiyo katika mafunzo ya awali (Induction course) yanayofanyika katika Hoteli ya Kings Way Mkoani Morogoro.
Baadhi ya waajiriwa wapya wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wakiwa katika mafunzo ya awali (Induction course) yanayofanyika katika Hoteli ya Kingsway Mkoani Morogoro.
Baadhi ya waajiriwa wapya wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wakiwa katika mafunzo ya awali (Induction course) yanayofanyika katika Hoteli ya Kingsway Mkoani Morogoro.
Baadhi ya waajiriwa wapya wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wakiwa katika mafunzo ya awali (Induction course) yanayofanyika katika Hoteli ya Kingsway Mkoani Morogoro.
Mkurugenzi  wa Utawala na Rasilimali Watu wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Bw. Gerald Mwanilwa akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya awali ya waajiriwa wapya wa Ofisi hiyo jana Mjini Morogoro.
Kaimu Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Jasper Mero (Kulia) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya awali kwa waajiriwa wapya wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi yanayofanyika katika Hoteli ya Kingsway Mkoani Morogoro.
Baadhi ya waajiriwa wapya wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wakimsikiliza kwa umakini Kaimu Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Jasper Mero (hayupo pichani).
Kaimu Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Jasper Mero (Kushoto) akisisitiza jambo wakati akijibu maswali mbalimbali ya waajiriwa wapya wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi.



Kaimu Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Jasper Mero (Katikati waliokaa) na baadhi ya viongozi waandamizi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waajiriwa wapya wa Ofisi hiyo.
Na Saidi Mkabakuli
WATUMISHI wa umma nchini wameaswa kuwa waadilifu na kuzingatia ubora wa kazi wakati wanatoa huduma kwa wananchi.

Wito huo umetolewa na Kaimu Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Bw. Jasper Mero wakati akifungua mafunzo ya awali ya wiki moja kwa waajiriwa wapya 130  wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi yanayofanyika katika Hoteli ya Kingsway mkoani Morogoro.

Bw. Mero amesema kuwa udilifu na ubora kwa watumishi wa umma ni kinga dhidi ya matumizi mabaya ya ofisi za umma na ni moja kati ya njia zinazowawezesha watumishi wa umma kuwa wachapakazi hodari.

“Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi inaamini katika “Ubora”kwa kila inachokifanya ukianzia ubora wa taarifa za ukaguzi zinazotolewa, huduma bora kwa wadau wake, ubora wa watumumishi kwa maana ya taaluma, maadili, weledi,” alisema Bw. Mero.

Ameongeza kuwa Falsafa hii ya ubora ndiyo iliyoifanya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi kupata umaarufu mkubwa kikanda na Kimataifa.   

“Kiwango cha juu cha Ubora wa kazi zetu na utendaji wa kazi unaozingatia weledi vitaweza tu kufikiwa kwa kuajiri watumishi wenye sifa stahiki, maadili, na bidii ya kuchapa kazi na wanaoweza kwenda sambamba na kasi kubwa ya mageuzi katika Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi,” aliongeza Bw. Mero. 

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Ofisi hiyo, Bw. Gerald Mwanilwa alisema kuwa mafunzo elekezi ni matakwa ya Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma za mwaka 2003, hususani Kanuni Na.103 (1-6) pamoja na Kanuni za kudumu za Utumishi Serikalini za 2009 Kifungu G.3 (a na b).

“Mafunzo haya ni kwa mujibu wa matakwa ya kisheria na yanalenga kutoa uelewa mahususi kwa waajiriwa wapya kulingana na kada zao,’ alisema. 

Kwa mujibu wa Bw. Mwanilwa, kupitia mafunzo hayo, washiriki wataweza kuelewa namna ya kutekeleza majukumu yao kama Watumishi wa Umma pamoja na kupata fursa ya kujifunza Miongozo na Nyaraka mbalimbali watakazozitumia kama watumishi wa umma na wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali. 

Pia, kupitia mafunzo hayo watapata fursa ya kujifunza na kuelewa utamaduni wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi unaosisitiza kufanya kazi kwa uweledi, uadilifu na kwa kuzingatia ubora na viwango vya kitaifa na kimataifa ambapo ofisi yetu ni Mwanachama (Intosai Afrosai na Afrosai-E).

“Mafunzo haya ni ya wiki moja yatatoa fursa kwenu kujua maana ya kuwa mtumishi na kazi za mkaguzi na miiko au maadili yake. Pia mtaelezwa kwa kifupi na kupewa utangulizi kuhusu Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, sheria mbali mbali, Kanuni na taratibu ili kuwawezesha kuelewa na kufanyakazi kama watumishi wa umma,” aliongeza Bw. Mwanilwa.