ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 16, 2015

ZAIDI YA WASANII 260 WAJITOKEZA KUWANIA NAFASI KUTUMBUIZA JUKWAA LA JEMBEKA FESTIVAL MWANZA

Kuelekea Show ya Uzinduzi wa Jembe Fm Radio ya Jijini Mwanza unaotarajia kufanyika May 23 mwaka huu katika Uwanja wa CCM Kirumba, zaidi ya Wasanii 260 ambao wanafanya style tofauti tofauti za muziki wamejitokeza hii leo katika Usaili kwa ajili ya Kuwania nafasi ya Kupanda jukwaani kutumbuiza katika Uzinduzi huo. Pichani majiaji wakiwa kazini kweye usaili uliofayika jioni hii Jemba Beach jijini Mwaza.
Mshiriki upande wa ku-Rap Yasinta.
Sura hii imetinga fainali upade wa kuimba hivyo itamenyana na wenzake tarehe 23 Mei 2015 uwanja wa CCM Kirumba Jembeka Festival.
Scorpion wamesonga mbele hivyo kuchuana faiali CCM Kirumba Mwanza.
Angle.
Makopa nao fainali ileeeeee.......Tukutae CCM Kirumba Mwanza tarehe 23 Mei 2015.
Another Crew.
Chop Chop.
Mashuhuda.
Majaji wakichekecha \UbongO.
Tukutane fainali....tarehe 23 Mei 2015 CCM Kirumba kwa kiingilio cha shilingi 5000/= uazama ndani.
Miongoni Mwa wasanii watakaotumbuiza katika Tamasha la Burudani la Jembeka Festival ni pamoja na Young D, Pam D, Izzo Busness, Yamoto Band, JJ Band, Dogo Janja, Chege, Mr.Blue,Juma Nature, Mo Music, Baraka Da Prince, Diamond Platnumz, H.Baba, Director Shahibu, pamoja wasanii Wengine wengi ambapo Kiingilio itakuwa ni shiling 5,000 na Milango itakuwa wazi kuanzia saa Sita Mchana hadi Majogoo.

MTU KWAO: HAYA NDIYO MAPOKEZI YA MBUNGE WA JIMBO LA KWIMBA.

Mbunge wa Kwimba Mansoor amepata mapokezi makubwa jimboni kwake.
Akiwa ameambatana na Katibu wa mkoa wa Mwanza Bw. Miraji Mtaturu, Mbunge huyo amekabidhi kadi 1600, mifuko ya saruji 600 yenye thamani ya shilingi milioni 12 na kuviwezesha vikundi mbalimbali zaidi ya shilingi milioni 5.
Mbunge wa Kwimba Mansoor akihutubia watu wa jimbo lake ambapo kubwa zaidi alizungumzia suala la kuboresha elimu na nini mikakati ya baadaye kuhusu kukamilisha miradi ya maji..
Kusanyikoni.
Katibu wa mkoa wa Mwanza Bw. Miraji Mtaturu naye alipata fursa ya kuzungumza na waanci wa Jimbo la Kwimba akatia msisitizo.
Wanachama wapya.
Kusanyiko.PICHA ZOTE NA ZEPHANIA MANDIA


MBUNGE MANSOOR, JIMBO LA KWIMBA LIMEBADILIKA NA KUPIGA HATUA YA MAENDELEO KWA VITENDO.

NA PETER FABIAN, KWIMBA.
MBUNGE wa Jimbo la Kwimba, Shanif Mansoor,ametamba kuwa wananchi wa jimboni humo wajivune kwa kushirikiana nae kuleta maendeleo kwa vitendo na kulibadilisha badala ya kusikiliza uzushi wa baadhi ya wapinzani wake kisiasa wanaoendekeza ukabila.

Pia amekuwa akichangia miradi ya maendeleo ambapo metoa kiasi cha shilingi milioni 17 za kutekeleza ahadi zake za maendeleo na Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa vitendo katika Jimbo lake.

Mansoor alikabidhi saruji mifuko 600 katika Kata za Mhande, Fukalo, Ngudu na Bupamwa kwa ajili ya kusaidia ujenzi kwenye shule za msingi, zahanati na sekondari pamoja na kuchangia fedha na vifaa vya Kompute kwenye baadhi ya sekondari    na Chuo cha Afya cha Ngudu mjini.

Mbunge Mansoor akizungumza na mamia ya wananchi waliofurika kwenye mkutano wa hadhara juzi uliofanyika katika viwanja vya stendi mjini Ngudu, alisema kwamba saruji hiyo aliyoitoa katika Kata ya Bupamwa kwenye vijiji vya Dodoma, Kiliwi na itegamatwi kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa shule za msingi.

Katika Kata ya Fukalo alitoa saruji katika vijiji vya Sanga, Msongwa, Chibuji kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za msingi, Kata ya Mhande ni kijiji cha Gurumwa kwa ajili ya kusaidia pia ujenzi wa shule ya msingi na milioni tatu kwa maabara ya sekondari na Kata ya Ngudu mjini alitoa fedha kiasi cha shilingi milioni mbili sekondari ya Bujiku Sakila na shilingi milioni moja Ngudu mjini.

Maeneo mengine aliyochangia ni Chuo cha Afya Ngudu mjini shilingi milioni 2 kwa ajili ya ujenzi wa choo na kutoa Komputa tatu(sh. 1.8 mil), kuchangia saruji mifuko 50 kanisa la Romani (RC) na mifuko 50 kanisa la Afrika Iniland Charch Tanzania (AICT) katika kijiji cha Kilyaboya na kikundi cha ujasilimali Ngudu mjini kilipata shilingi laki tano.

Mansoor aliwaeleza wananchi kuwa katika fedha hizo za kuchangia maendeleo hazihusiani na Mfuko wa Jimbo la Kwimba bali kutokana na nguvu yake kwa lengo la kuwasaidia wananchi ili kupiga hatua ya maendeleo, ambapo al katika Kata ya Ngudu mjini alichangia saruji pia vijiji vya Gudula (shule) na Chamela (jengo la Kiliniki).

“Thamani ya saruji ambayo leo nimeitoa kusaidia wananchi katika vijiji hivyo ni shilingi milioni 12 na jumla ya fedha zilizokabidhiwa ni shilingi milioni tano tasilimu hivyo hapa misaada yote imegharimu kiasi shilingi milioni 17 jambo ambalo ni la kujivunia kwa wananchi kwa kuwa na Mbunge anayetambua maendeleo,”alisema.

Mansoro alitamba kuwa kwa kipindi chake cha uwakilishi kwa wananchi amefanya mambo makubwa kusimamia ikiwemo, usambazaji umeme vijijini katika Kata, kupigania maji safi kutoka chanzo cha Ziwa Victoria cha Ihelele, Shinyanga- Kahama ambayo huduma imefika na barabara ya Hungumalwa, Ngudu-Magu kwa kiwango cha lami ambayo tayari upembuzi yakinifu utaanza hivi karibuni.

Mbunge    huyo alitoa wito kwa wananchi wa Jimbo la Kwimba kumpatia ushirikiano kutekeleza yale aliyoahidi kwao na kutekeleza Ilani ya CCM kwa vitendo na kuwapuuza baadhi ya wanasiasa wachache walioanza kupitapita huku wakimchafua na kuanza kuhamasisha ukabila jambo ambalo alisema wananchi wanapashwa kutafakari na kuwataka wapinzani wake waeleze sela na hoja zitakazowashawishi kuwachagua.

UKUMBI MPYA WA MIKUTANO WA KIMATAIFA UNAOJENGWA NA CCM MJINI DODOMA

 Muonekano wa ndani wa ukumbi mpya wa mikutano uliojengwa na CCM mjini Dodoma ambao uko katika hatua za mwisho kukamilika kabla ya kuanza kutumika.Ukumbi huu upo karibu na jengo la  Benki Kuu, njia ya kuelekea Chuo Kikuu cha Dodoma - UDOM.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua ujenzi wa Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Dodoma unaojengwa na  CCM.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua ujenzi wa Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Dodoma unaojengwa na  CCM. Kulia ni makamu mwenyekiti wa CCM Bara Philip Mangula.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na makandarasi wanaojenga ukumbi wa kimataifa wa Mikutano wa Dodoma unaojengwa na  CCM, leo.Ukumbi huu upo karibu na Benki Kuu, njia ya kuelekea Chuo Kikuu cha Dodoma.

Muonekano wa ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Dodoma. Picha na Freddy Maro.

Friday, May 15, 2015

KUANZIA SASA TUTAVAA JEANS TOKA BONGO

Meneja wa Utekelezaji na Maendeleo wa Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji nchini (EPZA), Mhandisi Keneth Haule (Kulia) akiukaribisha ugeni kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipokwenda kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Mamlaka, Mabibo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Kiongozi wa Msafara huo, Bibi Florence Mwanri. Wengine pichani ni Bw. Abel Shirima (Kushoto), Bw. Aloyce Andrea (Wapili Kushoto), na Bw. Omary Abdallah (Wapili Kulia).
Kiongozi wa Msafara kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) akizungumza na Mkurugenzi wa Mipango wa EPZA, Bw. Lamau Mpolo (Katikati) wakati walipotembelea kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam. Anayewasikilizia ni Meneja wa Utekelezaji na Maendeleo wa Mamlaka, Mhandisi Keneth Haule (Kulia).
Mkurugenzi wa Mipango wa EPZA, Bw. Lamau Mpolo (Katikati) akizungumza na Kiongozi wa Msafara kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) wakati Bibi Mwanri na ugeni wake walipotembelea Ofisi za Mamlaka kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Mamlaka, Mabibo jijini Dar es Salaam. Anayewasikilizia ni Meneja wa Utekelezaji na Maendeleo wa Mamlaka, Mhandisi Keneth Haule (Kulia).
Bibi Lilian Kalengo (Kulia), muwakilishi wa Kiwanda cha Tooku Garments akiwaonesha suruali ya jeans wageni kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipokwenda kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa eneo la Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji nchini (EPZA), Mabibo jijini Dar es Salaam. Kiwanda hicho ni moja ya viwanda 12 vilivyoanza uzalishaji katika Ukanda wa huo.
Kiongozi wa Msafara kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) akiangalia moja ya suruali zinazotengezwa na kiwanda cha Tooku Garments kilichopo katika eneo la Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji nchini (EPZA), Mabibo jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa mabinti wa Kitanzania walioajiriwa na Tooku Garments akiwa kazini.
Wakina dada wakiendelea na kazi ya utengenezaji wa suruali za jeans zinazotengenezwa na kiwanda cha Tooku Garments kilichopo katika eneo la Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji nchini (EPZA), Mabibo jijini Dar es Salaam.
Mandhari ya kuvutia ya Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji nchini (EPZA) yaliyopo Mabibo, jijini Dar es Salaam.
Mandhari ya kuvutia ya Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji nchini (EPZA) yaliyopo Mabibo, jijini Dar es Salaam.
Mandhari ya kuvutia ya Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji nchini (EPZA) yaliyopo Mabibo, jijini Dar es Salaam.

PICHA NA SAIDI MKABAKULI

DJ K FLIP SIMPLE SCRATCHES @ JEMBE FM 93.7 MWANZA


Ni ijumaa mazee na kama unataka kula ngoma za kijanja ile kisawasawa + Live Band basi tukutane Jembe Beach Malimbe Mwanza nchini Tanzania, ikiwa ni njia moja kuelekea siku ya kutengeneza historia katika tasnia ya kubongesha kwa hewa tarehe 23/05/2015 ndani ya uwanja wa CCM Kirumba.... Jembe ni Jembe Watu wana maswali mengiiiii. 

FAINALI YA KOMBE LA NG'OMBE ARUSHA NI ZAMZAM V/S NYOTA

kombe 3
Mfadhili wa michuano ya kombe la Ng'ombe  ambaye pia mkurugenzi wa kampuni ya  East Link Tanzania Ltd,Kim Fute wapili kutoka kushoto akibadilishana mawazo na baadhi ya vijana waliofika kushuhudia michuano hiyo ,michuano hiyo itahitimishwa mapema siku ya jumapili wiki hiii katika uwanja wa shule ya msingi Sinoni ambapo Timu ya Zamzam na Nyota watachuana(Habari picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)

kombe na view meru mlimaTaswira ya muonekano wa mlima Meru unavyoonekana pichani,hii ilikuwa juzi katika uwanja wa shule ya msingi Sinoni jijini Arusha


kombe 2
Baadhi ya wachezaji wa klabu ya Zamzam FC wakimwangalia mlinda mlango wao ,Seleman Casillas mara baada ya kuanguka na kulalamika kuua mguuni juzi katika mechi baina yao na Parrot katika kombe la Ng"ombe iliyochezwa katika uwanja wa shule ya msingi Sinoni jijini Arusha,klabu ya Zamzam ilifanikiwa kutinga fainali katika mchezo huo ambapo itakutana na Nyota siku ya jumapili

SOKA  ni mchezo wa ajabu embu sikia hii mlango wa klabu ya Parot FC,Sacrifice Adam juzi  alijikuta akiangua kilio uwanjani mara baada ya kushuhudiwa timu yake ikitolewa katika michuano ya kombe la ng’ombe linaloendelea  kuwaka moto katika uwanja wa shule ya msingi Sinoni jijini Arusha.

Adam,aliangua kilio wakati alipokuwa akishuhudia timu  yake ikiondolewa na klabu ya Zamzam FC juzi katika viwanja hivyo katika hatua ya matuta baada ya timu yake kuchapwa kwa jumla ya penati 5 kwa 4.

Hatahivyo,hapo awali Adam alifanikiwa kuokoa mipira mingi ya hatari iliyokuwa ikipigwa na washambuliaji wa klabu ya Zamzam hususani wakati timu hizom zinakkwenda kumalizia kipindi cha pili.

Kwa hatua hiyo klabu ya Zamzam sasa imefanikiwa kukata tiketi ya kuingia katika hatua ya fainali ambapo itakutana na Nyota siku ya kesho (jumapili) katika viwanja hivyo ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mdau wa michezo jijini Arusha na  mkurugenzi wa kampuni ya  East Link Tanzania Ltd,Kim Fute.

Hatahivyo,jambo la kuvutia katika mechi hiyo ni pale paliposhuhudiwa watu wa kada zote wanafunzi,wanawake,wazee pamoja na watoto wadogo walipokusanyika kwa pamoja kushuhudia mchezo huo jambo lililoashiria kwamba mchezo wa soka bado unachukua nafasi ya kupendwa kwa kiasi kikubwa kupendwa tofauti na michezo mingine.

SHIRIKA LA UMEME TANESCO PWANI LATOA TAHADHARI KWA WANANACHI WANAOFANYA BIASHARA CHINI YA NGUZO ZA UMEME.

NA VICTOR MASANGU, PWANI 
 
SHIRIKA la ugavi wa umeme Tanesco Mkoa wa Pwani  limewataka wananchi na wafanyabiashara ambao kwa sasa wanaoendeshea shughuli zao mbali mbali chini ya nguzo   za umeme kuondoka mara moja kutokana na kuwepo kwa hali ya hewa ya mvua kubwa ambayo inaweza kuhatarisha maisha yao.
 
 Hayo yamebainshwa na Afisa usalama wa Tanesco Mkoa wa Pwani Hery Byarugaba wakati wa zoezi la kufanya ukaguzi  wa miundombinu ya umeme ya shirika hilo  ikiwemo mita, nyaya,  transfoma, nguzo pamoja na mingineyo ili kuweza kuifanyia matengenezo.
 
 Afisa huyo alibanisha  kwamba kwa sasa wananchi wanatakiwa kuwa makini kutokana na kuharibika kwa miundombinu ya umeme kutokana na mvua ambayo inaendelea kunyesha katika maeneo mbali mbali.
 
Byarugaba alisema kwamba kutokana na kuwepo kwa mvua hizo sambamba na upepo mkali umesababisha kuwepo kwa uharibifu mkubwa wa miundombinu ya umeme ikiwemo kudondoka kwa nguzo zaidi ya nane hivi karibuni hali ambayo inaweza kuleta madhara makubwa kwa wananchi hivyo wanatakiwa wasiwe chini ya nyaya za umeme.
 
“Kwa sasa kitu kikubwa tunachokifanya kama tanesco ni kuhakikisha tunafanua jitihada za hali na  mali katika kukagua miundombinu yetu ya umeme ili kama kuna tattizo lolote la kiufundi tuweze kuikarabatiharaka iwezekanavyo na kuweza kuwapatia huduma wateja wetu ambayo inasatili,”alisema Byarugaba.
 
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Enarist Ndikilo amewaomba wazazi na walezi katika Mkoa wa Pwani kuwa makini na watoto wao na kuachana na kuwatuma katika maeneo ya mbali huku wakiwa peke yao na badala yake wawalinde kwani wanaweza kusombwa na maji.
 
“Nadhani mamlaka husika ya hali ya hewa tayari imeshatoa taadhari kuwa mvua bado inaendelea kunyesha katika maeneo mbali mbali ya Mkoa wa Pwani na maeneo mengine hivyo kitu kikubwa ninachowaomba wazazi na walezi kuwa makini na watoto wao, kwani wanaweza kupoteza maisha kutokana na mvua hizi,”alisema Ndikilo.
 
Aidha Injia Ndikilo amewataka wavuzi katika maeneo ambayo yapo kando kando ya  bahari ya hindi kutoendelea na shughuli zao za ufuaji wa samaki kwani kwa sasa bahari imechafuka hivyo lolote linaweza likajitokeza kutokana na kuwepo kwa mvua kubwa kunyesha ambazo zinaambatana na upepo mkali ambozo zinaweza kuleta madhara makubwa.

TUME YA MIPANGO YATEMBELEA BANDARI YA DAR ES SALAAM

Meneja wa Mipango na Mikakati wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Bw. Ntandu Mathayo (Kulia) akiukaribisha ugeni kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipokwenda kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Bandari ya Dar es Salaam. Kushoto ni Kiongozi wa Msafara huo, Bibi Florence Mwanri. Wengine pichani ni Bw. Aloyce Andrea (Wapili Kushoto), Bw. Robert Senya (Katikati) na Bw. Abel Shirima. 
Meneja wa Mipango na Mikakati wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Bw. Ntandu Mathayo (Wapili Kushoto) akizungumza wakati ugeni kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipokwenda kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Bandari ya Dar es Salaam. Wanaomsikiliza ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Bibi Lucy Kazibure (Kushoto) na wageni kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango.
Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Bibi Lucy Kazibure (Kushoto) akizungumza na ugeni kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipokwenda kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Bandari ya Dar es Salaam. Ugeni huo uliongozwa na Naibu Katibu Mtendaji (Huduma za Jamii na Masuala ya Idadi ya Watu) Bibi Florence Mwanri (Wapili Kushoto).
Kiongozi wa Msafara kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) akikaribishwa na Mkuu wa Sehemu ya Kushushia Mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam, Kapteni P. R. Paul (Kulia) wakati walipotembelea kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Bandari ya Dar es Salaam.
Mkuu wa Sehemu ya Kushushia Mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam, Kapteni P. R. Paul (Kulia) akitoa maelezo kuhusu hali ya upakuaji wa mafuta kwa ugeni kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipokwenda kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Bandari ya Dar es Salaam.
Kiongozi wa Msafara kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) akizungumza wakati walipokwenda kujionea maendeleo ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Bandari ya Dar es Salaam. a
Pichani meli ikipakua shehena ya mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam.
Pichani meli ikipakua shehena ya mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam.
PICHA NA SAIDI MKABAKULI.

MBUNGE JAMES MBATIA APENDEKEZA SHULE BINAFSI ZIPEWE RUZUKU TOKA SERIKALINI

Wanafunzi wanaohitimu kidato cha sita katika shule ya sekondari ya Maua Seminary wakiimba wimbo wa taifa wakati wa mahafali ya kuhitimu kidato cha sita yaliyofanyika shuleni hapo.
Wahitimu wa kidato cha sita shule ya sekondari Maua Seminari.
Mkuu wa shule ya sekondari Maua seminari ,Erastus Tesha akizungumza katika mahafali ya 33 kwa wahitimu wa kidato cha sita yaliyofanyika shuleni hapo.
Mgeni rasmi katika mahafali hayo ,mbunge wa kuteuliwa na rais ,Mh James Mbatia akizungumza na wanafunzi wa shule hiyo pamoja na wageni waalikwa .
Baadhi ya wageni waliofika shuleni hapo kwa ajili ya mahafali ya ndugu zao wanaotarajia kuhitimu kidato cha sita katika shule ya sekondary ya Maua.
Mbunge Mbatia akieleza mapungufu aliyoyaona katika kitabu cha sera ya elimu kilichozinduliwa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete.
Mbatia akimkabidhi mkuu wa shule ya sekondari Maua Seminary kitabu cha sera ya elimu.
Mkuu wa shule ya sekondari ya Maua Seminari akimkabidhi Mbatia zawadi kutokana na kazi anayoifanya ya kutetea elimu ya Tanzania.
Mgeni rasmi katika sherehe hiyo ,Mbunge Mbatia akitoa zawadi ya keki kwa wanafunzi wanaohitimu kidato cha sita katika shule ya sekondary Maua Seminary.
Mgeni rasmi katika mahafali ya 33 ya kidato cha sita katika shule ya sekondari ya Maua,James Mbatia akiwa katika picha ya pamoja na walimu pamoja na wahitimu.
Mbunge Mbatia akiongozwa na mkuu wa shule ya sekondari ya Maua Seminary,Erastus Tesha kutembelea maeneo mbalimbali ya shule hiyo.
Baadhi ya majengo yaliyopo katika shule ya sekondary Maua Seminary.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Knada ya Kaskazini.