ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 2, 2015

GUMZO MTAANI - WAJANJA WA MWANZA TUTAKUWA JEMBE BEACH

Japo tayari ni tajiri ,Mayweather ambae jina lake la utani ni Money, inatarajiwa atapokea zaidi ya dolla millioni $150m na Pacquiao kama millioni $100m.
Pacquiao yeye ametoka jamii ya kimaskini huko Ufilipino na kuna wakati katika maisha yake ya utotoni ambapo hata angelala njaa.
Sasa wa kuangalia kwenye TV kando, wengi wa mashabiki wa huko Marekani wangependa kuona makonde yakirushwa 'LIVE' kwa hivyo wamekubali kutoa ada ya hadi $100 kwa kichwa kushuhudia wakiwa 'LIVE' nje ya ulingo.
Wenye uchu wa kushuhudia pambano hilo 'LIVE' lakini hawajapata tiketi wako tayari kuzipata kwa walionanazo huku dau likiwa limepandishwa kwa kiwango atakacho muuzaji huyo mchuuzi.

Wafilipino kumshangilia Pacquiao

Wakati huo huo wito umetolewa kwa wakaazi wa kisiwa kimoja cha Philippines kwamba watumie kawi kwa kipimo kidogo ili kuihifadhi ndio waitumie kumwangalia katika runinga zao hapo Jumapili shujaa wao m-Filipino mwenzao , Manny Pacquiao (36) atakapokuwa akipambana na Mmarekani Floyd Mayweather (38) kwenye ulingo wa shindano la ndondi linalotajwa kuwa kubwa zaidi mnamo siku za hivi karibuni.
Wakaazi hao wameshauriwa na kampuni ya umeme nchini humo Palawan kuzima vifaa vya matumizi mengine ya nyumbani kama friji, kutotumia mashine za kufua nguo, wala kutopiga pasi ili kuhifadhi kawi hiyo siku hiyo itumike tu kuwashia Runinga zao.
Ushauri huo umetolewa kwani kisiwa hicho hukumbwa na upungufu wa umeme mara kwa mara, hivyo ni sharti wafuate maagizo hayo ili wasikose kushuhudia na kumshangilia kinara huyo wao ataeshiriki pambano hilo litakalo fanyika huko Las Vegas Jumamosi usiku saa za Marekani.
Ndilo pambano lililovutia fedha zaidi kuwahi kutokea.

Friday, May 1, 2015

RAIS Dkt. KIKWETE "NISINGEKUWA RAIS NINGEKUWA MSANII MKALI WA BONGO FLEVA"

























 RAIS Dkt. Jakaya Kikwete, ametamba kuwa angekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya basi angelikuwa wa “BongoFleva” kutokana na kuwa na sauti nzuri yenye kumudu kuimba nyimbo kwa ufasaha zaidi.

Kauli hiyo ameitoa leo jijini Mwanza kwenye uwanja wa michezo wa CCM Kirumba wakati wa maadhimisho ya kilele cha sherehe za Mei mosi zilizofanyika Kitaifa jijini Mwanza kwa mwaka huu wa mwisho wa utawala wake.

Dkt. Kikwete akiimba wimbo wa Bendi ya OSS (Ochestra Safari Sound) wenye mashairi yasemayo "mimi msafiri bado niko njiani sijui lini nitafika... naulizia watu kule ninakokwenda....”  na kukonga nyoyo za mashabiki wa muziki wa dansi waliomshangilia ambapo alijigamba kuwa na sauti ya mauzo.

“Mmesikia sauti yangu si mbaya sana,  hakika nisingekuwa Rais wa Nchi hii basi nigekuwa msanii wa bongo fleva kama akina Ali Kiba, Diamond na wasanii wengine wakali nikiuza album zangu kwani ninge kuwa tishio kwa kuimba lakini sikujaliwa kuwa masanii lakini najua kwa kiasi flani kuziimba nyimbo za baadhi ya bendi zilizokuwa maarufu hapa nchini,” alisema.

Rais pia alimpongeza msanii maarufu nchini wa kizazi kipya mwenye mashairi na misamiati ya maneno magumu, Mrisho Mpoto, kwa kumtaka kujibu bango la walimu lililokuwa na ujumbe uliosomeka “Shemeji Unatuachaje??” ambapo alijibu kwa kusema kuwa kuoa mwalimu nitabu kweli kweli haya nimesikia.

Aliwapongeza viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) nchini kwa kumwalika Mpoto “Mjomba” mara nyingi amekuwa akitoa ujumbe mzito kupitia fani yake ya muziki na mashairi lakini yakifikisha ujumbe bara bara kwa wananchi katika sherehe mbalimbali za kitaifa na makongamano .

EXCLUSIVE: IDRIS NA WEMA MWANZA

Yakiwa yamebakia masaa machache tu ile party iliokua ikisubiriwa kwa hamu Zari All White party kufanyika jijini Dar. 

Pati ambayo imeandaliwa na Zari aka Mrs Chibu Dangote pamoja na mpenzi wa zamani wa Wema Sepetu bwana Diamond Platnumz aka Chibu Dangote… 

Madam Wema Sepetu nae akaona alipize kisasi kwa kwenda kufaya party yake jijini Mwanza kesho May 2nd, Jembe ni Jembe Club,  akiwa na Mshindi wa Big Brother 2014 Idris Sultan. Kukiwa na fununu kwamba kwa sasa kishkwambi kipya cha Milionea mtoto huyo ni Wema Sepetu.. Je tutegemee drama jipya mjini?

WFANYAKAZI WAHIMIZWA KUJITOKEA KUJIANDIKISHA KATIKA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

Tume ya Taifa ya Uchaguzi inaendelea kuwahamasisha wananchi wote kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wapiga Kura ili kuweza kupiga kura ya maoni na kuchagua viongozi katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 2015.
Hayo yamedhihirika leo wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani Mei 1, 2015 zilizofanyika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambapo wizara mbali mbali ikiwemo taasisi binafsi zilibeba mabango yenye ujumbe kuhamasisha wafanyakazi.
Mpaka sasa zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura linaendelea vizuri katika Mikoa ya Ruvuma, Lindi na Mtwara.
 Wafanyakazi wa Tume ya Uchaguzi (NEC) wakiwa katika maandamano kusherekea siku ya Wafanyakazi Duniani MEI MOSI huku wakiwa na bango lenye ujumbe wao mahususi kuwahamasisha wananchi kushiriki kujiandikisha na wapige kura kuchagua kiongozi bora.
 Wafanyakazi wa Mamlaka  ya anga nao  hawakuwa nyuma na mabango yao.
 Wafanyakazi wa Ofsi ya Rais - Ikulu...
 Wafanyakazi wa Shirika la Ndege ya Air Tanzania...
Mabango mbalimbali yamebeba kaulimbiu juu ya kuhamasisha wafanyakazi kujiandikisha katika Daftari la Wapiga Kura km. Nikiripoti toka Uwanja wa Taifa wa Zamani (Picha na Christina Njovu).

MRATIBU WA ASASI YA BETTER LIVING AID ATOA WIT KWA WAFANYABIASHARA WA VIFAA VYA UJENZI

Watangazaji Hamisa Mussa Lubilo na Deogratius Yagomba wa VOT fm 89.0 wakimuuliza maswali mratibu wa asasi ya Better Living Aid walipomualika leo asubuhi katika kipindi cha Meza huru!
Mratibu wa asasi ya kiraia ya Better Living Aid Bw Mkala Fundikira leo akiwa amavalia fulana ya mkakati wa Imetosha unaopinga mauaji dhidi ya watu wenye ualbino ambao yeye ni mjumbe wa kamati kuu, ametoa wito kwa wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi mjini Tabora waiunge mkono asasi yake inayodhamiria kujenga vyoo na zahanati katika kijiji  cha Amani kilichopo Ipuli Tabora, kijiji chenye wakazi wazee na wasiojiweza na waishio na gonjwa sugu la ukoma. Alitoa wito huo akiongea katika kipindi cha meza huru cha Vot fm89.0 alisema "nawaomba wenye maduka ya vifaa vya ujenzi watuunge mkono kwa kuchangia hata mifuko mitano ya simenti, bati mbili au hata kifaa chochote cha ujenzi ambacho kitataumika katika ujenzi wa vyoo na zahanati katika kijiji hicho alimradi tunahitaji michango ya aina yeyote ile" 
Mkala Fundikira akijibu moja ya maswali yaliyoulizwa na watangazaji wa kipindi cha Meza huru, kipindi kinachoruka ktk kituo cha redio cha VOT fm 89.0 ya Tabora leo asubuhi.
Pamoja na kueleza kuwa asasi yao inayoundwa na marafiki toka mitandao ya jamii kama Facebook  na Viber pia alieleza kuwa tangu waanze kusadia kijiji hicho washapeleka vyakula, vyandarua na masweta kwa nyakati tofauti, pia ikiwemo kulipia upulizwaji wa dawa za kuuwa wadudu pamoja na kunguni ambao walikuwa wakisumbua wakazi wa kijiji cha Amani. 
Mkala akiwa amevalia fulana yenye ujumbe wenye kupinga mauaji kwa watu wenye ualbino ya mkakati wa Imetosha.
Alipoulizwa dhamira ya asasa yao ni kusaidia Tabora tu au na mikoa mingine? Mratibu huyo alijibu "Hapana, Better Living Aid itasaidia na kwingineko pia, kwa mfano tunatafuta wahisani ili tukajenge zahanati kijijini Masweya wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, Masweya hakuna zahanati pamoja na kuwa pana wakazi zaidi ya 7000, nafikiri wa Tanzania tuwe wahalisia kuwa serikali yetu haitoweza kukidhi mahitaji ya wa Tanzania wote kwa wakati mmoja hivyo basi ni wakati muafaka wa sisi kama jamii kuanza kujitolea na kuwezesha asasi kama yetu kupeleka huduma za afya sehemu kama Masweya"

Fundikira pia alimshukuru Mh Munde Tambwe Abdallah kwa kutoa ahadi ya Mifuko 50 ya simenti, lori 10 za mchanga pamoja na tano za mawe na kokoto , alisema "Tena kabla sijasahau nimpongeze na kumshukuru sasa sana sana Mh Munde Tambwe kwa kutupa msaada ambao ni msingi, kwa maana ya kuwa ahadi yake ndiyo itaanzisha ujenzi wa majengo hayo ya vyoo na zahanati, hivyo basi na wengine wajitolee ili tusonge mbele" 
Hoteli ambamo chakula cha usiku cha uchangishaji fedha kwa ujenzi wa vyoo na zahanati utafanyika baadae mwezi huu jijini Dar es Salaam iliyopo maeneo ya Ocean road.
Aidha asasi hiyo ina mpango wa kuandaa chakula cha usiku jijini Dar es Salaam katika hoteli ya Southern Sun baadae mwezi huu ambapo Mh Samuel Sitta(waziri wa uchukuzi) amekubali kuwa mgeni rasmi, karamu hiyo itaandaliwa ili kuchangisha fedha za kuwezesha miradi hiyo iweze kukamilika. "Bado tupo kwenye hatua za mwanzo za maandalizi lakini tunataraji karamu hiyo ya uchangishaji pesa ifanyike ama mwishoni mwa mwezi wa MEI au mwanzoni mwa mwezi Juni 2015. Pia Fundikira aliwashukuru Mh Aden Ragen(Mbunge wa Tabora mjini), Mh Munde Tambwe(Viti maalum), Sylvester Koka(Mbunge wa Kibaha) na wanachama na wote wa Better Living Aid kwa kuwezesha kifedha upulizwaji wa dawa kijiji cha Amani uliogharimu Tsh Laki 980.

Tembelea mtandao wa betterlivingaid.Blogspot.Com ujue zaidi kuhusu asasi hii na malengo yake au piga namba 0754 666620 kwa maelezo.

RAIS KIKWETE ATEUA MAJAJI WAWILI WA MAHAKAMA YA RUFAA



THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone:255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz

Fax: 255-22-2113425


Coat of Arms
PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

RaiswaJamhuriyaMuuganowa Tanzania, MheshimiwaJakayaMrishoKikweteamewateuaMajajiwawiliwaMahakamaKuuya Tanzania kuwaMajajiwaMahakamayaRufanikuanziaJumamosiiliyopita, Aprili 24, 2015, taarifailiyotolewa Dar es Salaam, leo, Alhamisi, Aprili 30, 2025 naOfisiyaKatibuMkuuKiongozi (KMK) imesema.
TaarifahiyoimewatajawajajihaokuwaniJaji  AugustineGherabastMwarijanaJaji Stella Ester Augustine Mugasha, ambaowotewamekuwaMajajiwaMahakamaKuuya Tanzania tokeawalipoteuliwaNovemba 28, 2006.
Kablayauteuzi wake, JajiMwarijaalikuwaJajiMfawadhi, Kitengo cha Biashara, MahakamaKuu, Dar Es Salaam. KablayakuwaJajiwaMahakamaKuualikuwaMsajiliwaMahakamayaRufanikatiyamwaka 2003 na 2006.
AliajiriwakamaHakimuMkaziDaraja la TatuFebruari 2, mwaka 1987, baadayakupataShahadayaSheriamwaka 1986.
NayeJajiMugasha, kablayauteuzi wake, alikuwaJajiMfawidhi, Dar es Salaam.AlikuwaMfawidhi, MahakamaKuu, Kanda ya Arusha naawali Kanda ya Moshi tangu 2009 hadialipohamishiwaMahakamaKuu, Dar Es Salaam.
AliajiriwakamaWakiliwaSerikalimwaka 1983 baadayakupataShahadayaSheriamwakahuohuo, 1983.

Mwisho.

Imetolewana:
KurugenziyaMawasilianoyaRais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

30 April, 2015