ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 11, 2015

PICHA ZAIDI ZA MAFURIKO LAMADI WILAYANI BUSEGA MKOANI SIMIYU

Afisa wa Idara ya Kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega,Msingi Lyeme (pichani), mkoani Simiyu akiangalia moja ya nyumba  zilizoanguka kufatia mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika kijiji cha Lamadi wilayani Busega kama aliyonaswa na Kamera yetu. 


Baadhiya nyumba zilizobomoka na kuanguka kutokana na maji kujaa ndani kufatia mafuriko yaliyotokea katika kitongoji cha Kisesa Sokoni, Kijiji cha Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu jana kufatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini. 
Baadhiya nyumba zilizobomoka na kuanguka kutokana na maji kujaa ndani kufatia mafuriko yaliyotokea katika kitongoji cha Kisesa Sokoni, Kijiji cha Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu jana kufatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini. 
Baadhiya nyumba zilizobomoka na kuanguka kutokana na maji kujaa ndani kufatia mafuriko yaliyotokea katika kitongoji cha Kisesa Sokoni, Kijiji cha Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu jana kufatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini. 
Baadhi ya wakazi walioathilika na mafuriko katika kijiji cha Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu wakiwa nje ya maeneo ya nyumba zao baada ya kubomoka kufatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini. 
Baadhiya nyumba zilizobomoka na kuanguka kutokana na maji kujaa ndani kufatia mafuriko yaliyotokea katika kitongoji cha Kisesa Sokoni, Kijiji cha Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu jana kufatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini. 
Baadhi ya wakazi walioathilika na mafuriko katika kijiji cha Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu wakiwa nje ya maeneo ya nyumba zao baada ya kubomoka kufatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini. 
Maeneo ya nyumba za makazi katika mji wa Lamadi yaliyokumbwa na mafuriko.
Ni sehemu ya msaada wa chakula, blanketi na majiya kunywa vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Busega, DK. Titus Kamani kufatia kukumbwa na mafuriko.
Upakuzi...
Baadhi ya wananchi wa kitongoji cha Likungu-Lamadi wakiwa wamebeba msaada wa chakula, blanketi na majiya kunywa vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Busega, DK. Titus Kamani kufatia kukumbwa na mafuriko.
Baadhi ya wananchi wa kitongoji cha Likungu-Lamadi wakiwa wamebeba msaada wa chakula, blanketi na majiya kunywa vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Busega, DK. Titus Kamani kufatia kukumbwa na mafuriko.
Baadhi ya wananchi wa kitongoji cha Likungu-Lamadi wakiwa wamebeba msaada wa chakula, blanketi na majiya kunywa vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Busega, DK. Titus Kamani kufatia kukumbwa na mafuriko.
Baadhi ya wananchi wa kitongoji cha Likungu-Lamadi wakiwa wamebeba msaada wa chakula, blanketi na majiya kunywa vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Busega, DK. Titus Kamani kufatia kukumbwa na mafuriko.
Mkuu wa Wilaya ya Busega, Paul Mzindakaya (mwenye kofia), akitoa taarifa kwa waandishiwa habari kutoka vyombo mbalimbali waliokuwa katika kijiji cha Lamadi yalipotokea mafuriko.

NAVY KENZO KUPAMBA TAMASHA LA SAMAKI CARNIVAL HII LEO JIJINI MWANZA

Mpango mzima ni leo ndani ya ukumbi wa YunLong iliyokuwa Rock Beach zamani pande za Capripoint Mwanza. Njoo tule samaki. BOFYA PLAY KUSIKIA MPANGO

RAIS DK. KIKWETE ATAKIWA KUSAINI HARAKA HATI ZA ADHABU YA KUNYONGWA WAUAJI WA ALBINO

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Dk. Titus Kamani akizungumza juzi na wananchi wa Kitongoji cha Lukungu Kijiji cha Lamadi wilayani Busega wakati wa ziara yake ya kukagua uhai wa Chama hicho na utekelezwaji wa Ilani ya uchaguzi. 
Mbunge wa Jimbo la Busega, Dk. Titus Kamani, akimvisha aliyekuwa mmoja wa wanachama wa Chama cha Demkrasia na Maendeleo (CHADEMA) kati ya 47 waliyokihama chama hicho juzi katika Kijiji cha Lamadi kwenye mkutano wa hadhara wa wananchi wa Mbunge huyo.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Dk. Titus Kamani, akipandisha bendera ya CCM kuashilia uzinduzi wa Shina mojawapo kati ya kumi aliyozindua katika ziara yake ya kukagua uhai wa chama hicho wilayani Busega juzi. Picha na Peter Fabian.

NA PETER FABIAN, BUSEGA.
RAIS Dk Jakaya Kikwete ametakiwa kusaini haraka hati za watu waliopatikana na makosa ya mauaji ya Albino, ili adhabu ya kunyongwe hadi kufa itekelezwe jambo ambalo pia litasaidia kukomesha mauaji hayo yanayoibuka katika maeneo mbalimbali nchini.

Hayo yalisomwa juzi kwenye risala ya wananchi wa Kijiji cha Mwamagigisi wilayani Busega mkoani Simiyu, kupitia Kikundi cha Wajasiriamali wa CCM kijijini hapo kwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Dk. Titus Kamani alipofika kuweka jiwe la msingi la kufungua Ofisi na Shina lao la CCM .

Kikundi hicho kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa huo Dk Kamani, kimetoa sh 110,000 kusaidia mawasiliano ya walemavu wa ngozi (Albino) pindi wanapoona wako hatarini au kuna watu wanaowatilia shaka na kuonekana kuna dalili za kuwanyemelea.

Dk. Kamani alilitoa fedha hizo juzi wakati wa uzinduzi huo na uwekaji wa jiwe la Msingi, wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa Chama wilayani humo ambapo pia aliwahutubia wananchi waliohudhuria ikiwemo kuwakumbusha kujitokeza kujiandikisha katika daftari la kudumu ili kuwawezesha kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu.

Wakilaani mauaji ya Albino katika risara yao iliyosomwa na Odemba Bahai kwa Dk Kamani, wanakikundi hao walisema vitendo vya utekaji na mauaji ya walemavu hao vinawasikitisha, wanamuomba Rais Dk Kikwete asaini hati za adhabu za kifo za watu waliohumiwa kunyongwa hadi kufa, kutokana na mauaji hayo.

“Kuwafanya ndugu zetu Albino kuwa dili la kujipatia utajiri na kuwaua, ni kosa kubwa hata kwa Mungu, tunaomba mahakama ziharakishe kesi za watuhumiwa wa mauaji hayo na Rais wetu asaini hati za hukumu ya kuwanyonga watu waliohukumiwa kifo ili wanyongwe haraka hadi kufa.”

“…….Kuheshimu haki za binaadamu wenzetu hao tunatoa sh10,000 japo ni kidogo tulichonacho ili ziwasaidie walemavu wetu kununulia vocha za kupiga simu kwenye vyombo vya dola pindi wanapoona mtu aliye kwenye mazingira ya kuwanyemelea maeneo anayoishi,”. Ilisema sehemu ya risara hiyo.

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mwamagigisi na kujibu risara hiyo baada ya uzinduzi wa kikundi hicho, Dk Kamani alisema serikali ya CCM inalaani vikali mauaji ya walemavu hao na vikongwe na vyombo vya dola vimekuwa vikijitahidi kuwakamata wahusika na kuwafikisha kwenye mkono wa sheria.

DK. Kamani aliunga mkono mchango wa fedha za vocha zilizotolewa na wanakikundi hao na kuongeza sh 100,000 na kufanya mchango huo ufikie sh 110,000 ambazo zitakabidhiwa kwa viongozi wa Albino wa wilaya ya Busega.

Mwenyekiti huyo, pia katika ziara yake hiyo wilayani Busega alifungua mashina kumi ya wakereketwa wa CCM wakiwemo wana kikundi hao ambao aliwapiga jeki kwa kuwachangia sh milioni 1 huku mashina mengine akiyachangia kati ya sh 500,000 hadi 1,000,000 kila moja.

HAPPY BIRTHDAY BLOGGER CATHBERT ANGELO KAJUNA

Napenda kumshukuru Mungu kwa kunifikisha leo Aprili 10 (JANA) siku yangu ya kuzaliwa... Hakika Mungu ni mwema kwa kila jambo. Pia napenda kuishukukuru familia yangu, ndugu jamaa na marafiki kwa kuwa pamoja nami mpaka leo. Asanteni sana.

Friday, April 10, 2015

AHADI ZA MARAIS MKAPA (MSTAAFU) NA DK. KIKWETE HAZIJATEKELEZWA

 NA PETER FABIAN, MAGU. 

KATIBU wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mwanza (CCM), Miraji Mtaturu, ameitaka serikali kupita Wizara ya Maji kutekeleza haraka kwa vitendo, ahadi za Marais wa awamu ya tatu na nne ya kumaliza tatizo la maji na kuwapatia wananchi maji safi na salama wa Mji wa Magu Mkoani Mwanza. 
Mtaturu alisema kuwa Chama Tawala ‘kinalilia’ ahadi hiyo ambayo awali ilitolewa na Rais Benjamin Mkapa wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 1995 katika uwanja wa Sabasaba mjini hapa na Rais Dk Jakaya Kikwete mwaka juzi kwenye uwanja huo huo. 

Katibu huyo alisema kwamba kilio cha wananchi walichokitoa katika mkutano wa hadhara Aprili 2 mwaka huu kinaonyesha Wizara ya Maji bado inasuasua kumwajibisha Mkandarasi aliyepewa kazi hiyo, hivyo viongozi wa juu wa Serikali na Wizara wambane na kumuwajibisha Mkandarasi mshauri wa maradi huo ambaye ni Kampuni ya MS COWI (T) Ltd ya nchini Denmark. 
Mtaturu akihutubia maelfu ya wananchi wa mji wa Magui kwenye uwanja huo wa Sabasaba, Mtaturu alisema kazi ya serikali ni pamoja na kutekeleza ahadi ya Rais ambayo kimsingi ni agizo hivyo anashangazwa na kutotekelezwa haraka kwa mradi wa maji safi na salama kutoka katika chanzo cha ziwa Victoria, ulioahidiwa na marais hao.
 “Serikali inataraji kutumia kiasi cha fedha Euro milioni 5.3 zilizotengwa kwa ajili ya kutekeleza ujenzi wa mradi mkubwa wa maji katika Mji wa Magu na vijiji jirani lakini cha kushangaza kila mara Mkandarasi msanifu huyo amekuwa akitoa taarifa za kuendelea na upembuzi yakinifu, upembuzi hadi lini watu wanataka maji,” alisema Katibu huyo na kushangiliwa na umati wa wananchi.

 Aidha alieleza kuwa, Mkandarasi huyo anaonekana kuwa tatizo kwani wakati wa ziara zake wilayani Ukerewe na Sengerema, MS COWI (T) Ltd imeelezwa kuwa tatizo la kuchelewesha baadhi ya miradi ya maji na kila wataalamu wa maji wanapoulizwa wanatoa majibu ya danadana na yasiyo ya kulidhisha. 
“Mkandarasi huyu amezidiwa na kazi Wizara imbane na ikiwezekana imuwajibishe na kumnyima kazi sehemu nyingine, tunaiomba serikali kupitia Wizara kuanzia mwezi ujao (Mei) awe amemaliza Mkandarasi huyo wa usanifu wa mradi ili kazi ya ujenzi wa kuwawekea maji wananchi wa mji huu ikamilike,” alieleza.

 Awali akitoa taarifa kwa Katibu huyo, Mhandisi wa Maji wa Halmasha ya wilaya ya Magu, Joseph Bundala, alisema serikali imeingia mkataba na Benki ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya (EID) kujenga upya mradi wa maji wa mji huo ambao baada ya usanifu mzabubuni atatafutwa kuanza ujenzi. 

Bundala alisema ili kutatua kero hiyo kwa muda, Halmashauri ya wilaya yake imenunua pampu mpya na kufungwa katika chanzo cha maji cha Busulwa ambacho kwa sasa kinatoa huduma hiyo ambayo haijatosheleza kutokana na uchakvu wa miundombinu ya maji kuwa ya zamani. 
Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Paul Ntinika alisemakwa kushirikiana na wadau mbalimbali, halmashauri yake tayari imeisha chimba visima 18 na kufunga pampu za mkono katika maeneo ya Magu mjini (visima 6), Ilungu (3) Nyashimba (3), Kipeja (3) na Sagani visima vitatu.

SKYLIGHT BAND YAZIDI KUPASUA ANGA NA MUZIKI WA LIVE, NJOO USHUHUDIE LEO THAI VILLAGE

DSC_0616
Ni mwendo wa Nigerian Flava ni noma sana karibu leo ujione mwenyewe usisubirie kuadithiwa.

Aneth Kushaba AK 47(katikati) akiimba na waimbaji wenzake wa bendi ya Skylight ambao ni Ashura Kitenge(kushoto) na kulia ni John Music kwenye kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar.
Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower akiimba na kucheza moja ya Sebene la Kikongo pamoja Sony Masamba.
Sony Masamba ambaye ni mmoja wa waimbaji wa Skylight akiendelea kutoa burudani huku akisindikizwa na waimbaji wenzake kulia ni Sam Mapenzi na kushoto ni Joniko Flower.
Waimbaji wa Skylight Band wakiimba kwa moja ya nyimbo za bendi yao kwenye kiota cha Thai Village ijumaa iliyopita.
Sugua sugua mpaka itakate......Waimbaji wa Skylight Band wakicheza moja ya style zao zinazobamba mujini.
Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK 47 akiimba sambamba na msanii mwenzake Sam Mapenzi kwenye kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar.
Burudani ikiendelea kutolewa na wasanii wa Skylight Band.
Ashura Kitenge akiwapa raha mashabiki wa Skylight Band huku akisindikizwa na Aneth Kushaba AK 47(kushoto) pamoja na John Music (kulia)
Sugua Sugua mpaka utakate njoo leo ujifunze kusugua kama hawa mashabiki wa Skylight walivyojua mmoja ya Style ya kusugua
Sam Mapenzi akiendelea kutoa burudani kwa mashabiki wa Skylight band (hawapo pichani) huku akisaidiwa na waimbaji wenzake wa kwanza kushoto ni Ashura Kitenge akiwa smambamba na Sony Masamba(wa pili kutoka kushoto) pamoja na John Music (wa kwanza kulia) kwenye kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar
Ni mwendo wa Kusebeneka mpaka kieleweke kwa mashabiki na wapenzi wa Skylight Band
Ni happy mwanzo mwisho kwa mashabiki wa Skylight.
Mmoja wa mashabiki wa Skylight band akiogeshwa kwa vinywaji wakati wa kusherekea siku yake ya kuzaliwa kwenye kiota hiki cha Thai Village wakati band ya Skylight ikiendelea kutoa burudani.
Kumbukumbu zikichukuliwa hapa tunaweza kusema mpiga picha kapigwa picha
Wakati Sam Mapenzi akiimba wimbo wa "All of Me" mdada huyu ulimgusa sana mpaka akashindwa kujizuia akaamua afanye ya kwake.
Mdada akichukua selfie na msanii wa Skylight Band Sum Mapenzi baada ya kumkuna na weimbo wa "All of Me"