ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, December 10, 2015

JINSI WAFANYAKAZI WA TIGO WALIVYOSHIRIKI ZOEZI LA USAFI 9 DEC 2015

Meneja wa Kanda ya Ziwa Kampuni ya Mawasiliano ya simu Tigo Bwa. Edgar Mapande akifanya usafi katika moja ya mitaro sugu ipitishayo maji barabara inayoingia katika moja ya mitaa inayounganisha Soko la Mwaloni Kirumba jijini Mwanza, katika kuadhimisha sherehe za Uhuru wa Tanganyika ambapo safari hii Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufu aliamuru maadhimisho hayo kuadhimishwa kwa style ya kufanya usafi.
Meneja wa Kanda ya Ziwa Kampuni ya Mawasiliano ya simu Tigo Bwa. Edgar Mapande akiongoza wafanyakazi wenzake kuondosha uchafu ulioziba katika moja ya mitaro sugu ipitishayo maji barabara inayoingia katika moja ya mitaa inayounganisha Soko la Mwaloni Kirumba jijini Mwanza, katika kuadhimisha sherehe za Uhuru wa Tanganyika ambapo safari hii Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufu aliamuru maadhimisho hayo kuadhimishwa kwa style ya kufanya usafi.
Hali safi ya uhai katika usafi imeanza kuonekana.
Hapa ndipo eneo korofi zaidi kuliko maeneo yote.
Uhuru na usafi.
Zoezi hili lilifanyika kwa ushirikiano wa aina yake kwani hata majirani walio karibu na eneo hilo waliungana na wafanyakazi wa Tigo kukamilisha majukumu ya usafi.
Zoezi la hili la usafi lililofanywa na wafanyakazi wa Kampuni ya Mawasiliano ya simu za mkononi Tigo tawi la Mwanza lilihamasisha wadau mbalimbali wa maeneo yote karibu na soko la Mwalo wa Kirumba kufanya usafi kwa jitihada ya kupata mazingira yenye mwonekano sahihi....

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.