ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 18, 2015

CCM YAPITISHA JINA LA Dkt. TULIA ACKSON MWANSASU KUWANIA UNAIBU SPIKA: KUCHAGULIWA KESHO.

Mbunge mteule Mhe. Dkt Tulia Ackison Mwansasu aliyepitishwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwania nafasi ya Naibu Spika wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo kesho kunatarajiwa kufanyika kwa uchaguzi huo ndani ya ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma hapa akiomba kura kwa Mhe Vicky Kamata (Vitimaalum CCM) katika Hoteli ya New Dodoma leo

 Pitia sifa za mgombea huyu kijana katika nasafi ya Naibu Spika Dkt Tulia A Mwansasu mtaalamu wa Sheria

 Mhe. Shanif Hillan Mansoor (Jimbo la Kwimba) akiwa na Albert G Sengo mtangazaji wa Jembe FM na miliki wa Blog hii akijianda kufanya mahojiano baada ya kuapishwa kuzungumzia kero na changamoto za wananchi anazotaraji kuanza kuzifanyika kazi kama alivyowaahidi wananchi jimboni mwake.
 Mhe Dkt Tulia hongera kwa kupitishwa na Chama kuwania Unaibu Spika unafaa na kazi ni moja tu kuanzia sasa kuomba kura kwa waheshimiwa wenzako ni moja wa Makada wa CCM akimpatia neno hilo(wa pili kushoto) Albert G Sengo akisikiliza na Mhe Mansoor akifikiria neno la kusema kwa Mhe Dkt Tulia
 Mhe Mansoor akisema neno kwa Mhe Dkt Tulia kwamba tayari wewe ndo Naibu Spika tunasubilia kesho Wabunge kukupigia kura ili uibuke mshindi kwa kishindo hatuna shaka juu ya nafasi hiyo
 Wakati wa Waheshimiwa Wabunge kujumuika na familia, ndugu, jamaa na marafiki baada ya kuapishwa na hapa ni Mhe Kamata akifurahia na ndugu zake
 Mhe Dkt Tulia A Mwansasu (katikati) akisikiliza kwa makini ushauri wa Mhe Mbunge (kulia) na Mhe Richard Ndassa (Jimbo la Sumve) akisikiliza kwa makini alipowaomba wampigie kura kesho.
 Mhe Andrew Chenge aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkutano wa kumchagua Spika Job Ndugai wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jana alipopiga picha na jamaa leo katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Mhe Kemilembe Julias Lwwota (Vitimaalum CCM) akiwa na ndugu na marafiki nje ya ukumbi wa Bunge baada ya kuapishwa leo mjini Dodoma
Mhe Kemilembe Julias Rwota akiwa na ndugu na marafiki nje ya ukumbi wa Bunge baada ya kuapishwa leo mjini Dodoma

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.