ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 11, 2015

NANI MWINGINE MWENYE ZARI KUYANASA MAMILIONI...!!?

Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel Tanzania, Dangio Kaniki (kushoto) akimkabidhi mshindi wa droo ya sita ya promosheni ya “Jiongeze na Mshiko”, Rajabu Mwalapinga (kulia), mkazi wa Dar es Salaam, shillingi millioni tatu.
Afisa uhusiano na matukio, Bi Dangio Kaniki akiongea na mshindi aliyepatikana wakati wa kuchezesha droo ya saba ya wiki ya promosheni ya "Jiongeze na Mshiko" ambapo wateja wawili wa Airtel kutoka mikoa ya Kigoma na Dar es Salaam walipatikana akichukua taarifa za mshindi (kushoto) ni mkaguzi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha bwana Bakari Majid droo hii imechezwa jana katika makao makuu ya Airtel Moroco jijini Dar es saalam, Jumanne Septemba 1 2015.

WATEJA Wa Airtel wazidi kushida Mamilioni ya Pesa Dar es Salaam, Tanzania, Kampuni ya mawasiliano ya Airtel Tanzania imeendelea kuwafanya wateja wake mamilionea kupitia promosheni yake ya “Jiongeze na Mshiko”. 

Habibu Mwella Freuzi, mfanyabiashara kutoka Dar Es Salaam na Kitabu Ally, mkulima anayeishi Kigoma wamepatikana kuwa washindi wa million moja na million tatu baada ya droo ya kuchezesha droo ya nane katika ofisi za makao makuu ya Airtel jijini Dar Es Salaam.

Afisa Uhusiano na Matukio, Dangio Kaniki, alisema kuwa bado kuna zawadi nyingi kushindaniwa kati ya sasa mpaka Novemba atakapopatikana mshindi wa mwisho wa droo hii, atakayeondoka na kitita cha shililingi milioni 50. 

Hivyo aliwahimiza watanzania kuchukua fursa hii waliopatiwa na Airtel kujiinua kiuchumi Hadi sasa, promosheni ya “Jiongeze na Mshiko” ya Airtel imewafanya watanzania 16 mamilionea. Mamilionea zaidi wanategemewa kutokea katika promosheni hii iliyoanzishwa wiki saba zilizopita. 

Vile vile Airtel imewazawadia fedha taslimu washidi wa droo ya saba, ambao ni, Geri William kutoka Dar es Salaam na Lui Saulo Karunda, mkazi wa Kigoma. Wateja wanaweza kujinga na promosheni hii bure kwa kutuma ujumbe wenye neno "BURE" kwenda namba 15470, na kisha kuanza kupokea maswali kwenye simu zao na kujibu maswali bure bila gharama yoyote na kujikusanyia pointi.

Mteja atakapomaliza kujibu maswali ya bure atapata ujumbe utakaomuuliza kama angependa kujiunga na ngazi ya premier, ili kuwezeshwa kufunguliwa maswali zaidi na kujikusanyia pointi nyingi kwa zawadi zenye thamani kubwa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.