ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 18, 2015

MKUTANO WA KAMPENI YA MGOMBEA WA URAIS CCM DR. ALI MOHAMED SHEIN JIMBO LA MKOANI PEMBA

Mgombea Urais wa Zanzibar Kupitia CCM Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg Vuai Ali Vuai alipowasili katika viwanja vya mkutano vya Chokocho Wilaya ya Mkoani Pemba kwa ajili ya kampeni yake kwa wananchi wa Jimbo hilo la Mkoani.
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akiwa na Viongozi wa Siasa jukwaa kuu baada ya kuwasili katikac viwanja hivyo kwa ajili ya mkutano wake wa Kampeni katika viwanja vya mpira Black Wizard Chokocho Wilaya ya Mkoani Pemba.
Wanachama wa CCM wakimshangilia Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, alipowasili katika viwanja vya Mkutano wake wa Kampeni Jimbo la Mkoani Pemba.
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakiwa katika viwanja vya mkutano wa Kampeni ya Urais wa Zanzibar kupitia CCM katika viwanja vya Mpira Black Wizard Chokocho Pemba ,
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg Vuai Ali Vuai, akizungumza na Wananchi wa Wilaya Mkoani Jimbo la Mkoani Pemba akiwatambulisha Viongozi waliofuatana na Dk Shein wakati wa Mkutano wake wa Kampeni Pemba.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Pemba Mkoa wa Kaskazini Pemba Ndg Mberwa Hamad Mberwa akizungumza wakati wa Mkutano huo wa Kampeni ya Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein.
WanaCCM wakishangilia wakati wa Mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM uliofanyika katika viwanja vya mpira Black Wizard Chokocho Pemba Wilaya ya Mkoani.
 Mhe Zainab Omar akizungumza na Wananchi wa Jimbo la Mkoanni wakati wa Mkutano wa Kampeni ya Urais wa Zanzibar uliofanyika katika viwanja vya Chokocho, kumuombea Kura Rais wa Zanzibar Dk Shein kwa Wananchi wa Pemba ili kuendelea kupata maendeleo kupitia CCM.
Mhe Pandu Ameir Kificho akiwasalimia Wananchi wa Pemba Wakati wa Mkutano wa Kampeni ya Urais wa Zanzibar uliofanyika katika viwanbja vya Chokocho Mkoani Pemba.
Mhe Omar Yussuf Mzee akiwahutubia Wana CCM katika mkutano wa kampeni wa CCM katika viwanja vya Black Wizard Chokocho Mkoani Pemba na kuwataka wananchi kumchagua Mgombea wa CCM Dk Shein.
Viongozi wa Jukwaa kuu wakiinua mikono wakati wa mkutano huo kuashiria kumpigia kura Mgombea wa Urais wa Zanzibar mgombea wa CCM wakati wa mkutano huo wa kampeni.
Mhe Mohammed Aboud Mohammed akiwahutubia WanaCCM Kisiwani Pemba wakati wa Mkutano wa Kampeni ya Urais kupitia Chama cha Mapinduzi kuelezea Sera za CCM na mafanikio yaliopatika katika Uongozi wa Rais Dk. Shein, na kuwataka kumchagua kwa mara ya Pili Dk. Shein kuendelea kuleta maendeleo kwa Wananchi wake katika sekta mbalimbali za Jamii Zanzibar
Viongozi wa Jukwaa kuu wakisimama wakati Mgombea wa Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk Ali Mohamed Shein, akipanda jukwaani kuwahutubia Wana CCM katika mkutano wake wa kampeni kisiwanin Pemba uliofanyika katika viwanja vya mpira vya black wizard mkoani Pemba.

Mgombea wa Urais kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akiwahutubia Wananchi wa Jimbo la Mkoani kisiwani Pemba wakati wa mkutano wake wa Pili kisimwani Pemba kuomba ridhaa za kuchaguliwa tena kwa mara ya pili kuongoza Zanzibar kwa maendeleo ya Wananchi wa Zanzibar katika sekta mbalimbali za kijamii.
Baadhi ya Wanachama wa CCM Pemba wakimshangilia Mgombea wa CCM Dk Shein wakati akiwahutubia katika viwanja vya black wizard chokocho Pemba, wakati wa mkutano wake wa kampeni kisiwi humo.  
Mwanachama wa CCM akiwa katika viwanja vya kampeni akimsikiliza Mgombea wa CCM Dk Shein akiwa na picha ya mgombea Urais wa Zanzibar wakifuatilia mkutano huo.
Viongozi wa meza kuu wakifuatlia hutuba ya Mgombea wa Urais wa CCM Dk Shein wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya black wizard chokocho Mkoani Pemba.
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakimshangilia Mgombea wao wa CCM wakati akiwahutubia katika mkutano wake wa kampeni kisiwani Pemba katika viwanja vya black wizard chokocho Mkoani Pemba.
Viongozi wa Jukwaa kuu wakifuatilia mkutano wa kampeni wakati akihutubia Wananchi wa kisiwani Pemba katika mkutano wa kampeni ya Urais wa Zanzibar kupitia CCM. 
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Shein, akiwahutubia Wananchi wa Pemba katika mkutano wake wa Kampeni kisiwani huo uliofanyika katika viwanja vya mpira black wizard Chokocho Wilaya ya Mkoani Pemba. 
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi Jimbo la Mkoani Pemba Profesa Makame Mbarawa,wakati wa mkutano huo wa kampeni katika viwanja vya mpira black wizard mkoani Pemba. 
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge Jimbo la Mtambile CCM Ndg Khamis Salum Khamis wakati wa mkutano huo wa kampeni katika viwanja vya black wizard chokocho Pemba

Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge Jimbo la Kiwani CCM Ndg.Rashid Abdalla,wakati wa mkutano huo wa kampeni katika viwanja vya black wizard chokocho Pemba
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge Jimbo la Chambani Pemba Ndg. Mohammed Abdrahaman. Mwinyi,wakati wa mkutano huo wa kampeni katika viwanja vya black wizard chokocho Pemba
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi Jimbo la Mkoani Pemba. CCM Ndg Mmanga Mgengo,wakati wa mkutano huo wa kampeni katika viwanja vya black wizard chokocho Pemba
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi Jimbo la Mtambile Pemba. CCM Ndg. Mgaza Mohammed,wakati wa mkutano huo wa kampeni katika viwanja vya black wizard chokocho Pemba
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi Jimbo la Chambani Pemba. CCM Bi.Bahati Khamis Kombo,wakati wa mkutano huo wa kampeni katika viwanja vya black wizard chokocho Pemba
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi Jimbo la Kiwani Pemba. CCM Ndg Mussa Fumu Mussa,wakati wa mkutano huo wa kampeni katika viwanja vya black wizard chokocho Pemba
Mgombea Urais wa Zanzibar CCM Dk Ali Mohamed Shein, akiwatambulisha Wagombea Udiwani katika Wilaya ya Mkoani Pemba kupitia CCM, kwa Wananchi na kuwataka kuwapigia kura ya Ndio wakati wa uchaguzi Mkuu mwezom Oktoba 2015. wakati wa  mkutano huo wa kampeni katika viwanja vya black wizard chokocho Pemba
Mwanachama wa CCM akiwa na vyazi lake la kitenge la jengo la ASP wakati huo kwa sasa ni CCM akifuatlia mkutano huo, vitenge hivi vimetoka wakati wa miaka ya 70 kisiwani Zanzibar. 

Shekh akisoma dua baada ya kumalizikia kwa mkutano wa mgombea wa CCM Dk Ali Mohamed Shein, katika viwanja vya black wizard chokocho
Viongozi wa jukwaa kuu wakiitikia dua baada ya kumalizikika kwa mkutano wa kampeni ya Urais wa Zanzibar kupitia CCM.
Wananchi wakiitikia dua baada ya kumalizika kwa mkutano huo wa kampeni ya Urais kisiwani Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM akisalimiana na Vijana waliohidhuria mkutano huo wa kampeni yake katika viwanja vya black wizard chokocho Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Wazee wa Kijiji cha Chokocho kisiwani Pemba baada ya kumaliza mkutano wake wa kampeni ya Urais katika Jimbo la Mkoani Pemba.
Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot. zanzinews.com

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.