ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 1, 2015

JESHI LA POLISI KAHAMA LAMKAMA MTUHUMIWA WA MAUAJI

KAHAMA
Jeshi la polisi wilayani  Kahama mkoani shinyanga linamshikilia mtuhumiwa mmoja anayedaiwa kushiriki katika mauaji ya katibu wa Chama cha mapinduzi Kata ya  Isagehe mauwaji ambayo yalitekelezwa mwaka jana.

Mkuu wa jeshi la polisi wilayani Kahama Leonard Nyandahu amemutaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Thomas Malenge miaka 35 mkazi wa kijiji cha Mwalugulu ambapo mtuhumiwa huyo akiwa na wenzake 5 walimuuwa katibu wa CCM marehemu Daud Mbatilo.

Amesema kuwa mtuhumiwa huyo  na wenzake walikodiwa na mtu ambaye bado jeshi hilo linafanya uchunguzi kwa ujira wa kupatiwa kiasi cha shilingi milioni mbili  na kabla ya mauwaji hayo walipatiwa kiasi cha shilingi laki 6 na kutekeleza mauwaji hayo Desemba 03 mwaka jana.

Aidha jeshi hilo tayari limewanasa watuhumiwa wote 6na kwamba watuhumiwa watano walikwisha kamatwa na kufikishwa mahakamani lakini mtuhumiwa huyo aliyekamatwa jana mala baada ya tukioalitoloka kusikojulikana   hivyo juzi alilejea akidhani walisahau na kulialifu jeshi la polisi na kufanikiwa kumutia nguvuni.



Hata hivyo Jeshi la polisi linaendekea kumhoji mtuhumiwa ili kuweza kufanikiwa kumukamata mtu aliyefadhili mauwaji hayo ili wote waweze kufikishwa mahakamani kwa kosa la mauaji.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.