ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 11, 2015

MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CCM, EDMUND RUTARAKA ATANGAZA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA MOSHI MJINI.

Mtangaza nia wa nafasi ya Ubunge katika jimbo la Moshi mjini ,Edmund Rutaraka akiwasili katika ofisi za Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro,kwa ajili ya kikao na wajumbe wa halmashauri kuu ya chama hicho wa wilaya chenye lengo la kutangaza azma yake ya kugombea Ubunge katika jimbo hilo.
Mwenyekiti wa Makatibu, wa CCM,Kilimanjaro Nemes Kaingirila Maufi akizungumza wakati wa kikao malumu cha kutangaza nia kilichoitishwa kwa ajili ya Naibu kamanda wa vijana wilaya ya Moshi mjini na Mjumbe wa NEC wa chama hicho,Edmund Rutaraka (kulia) kutangaza nia ya kugombea Ubunge katika jimbo la Moshi mjini.
Baadhi ya wajumbe wa Halmashauri kuu ya  CCM wilaya ya Moshi mjini wakifuatilia mkutano huo.
Naibu Kamanda wa Vijana wa CCM Manispaa ya Moshi na mjumbe wa NEC ,Edmund Rutaraka akizungumza na wajumbe wa Halmshauri kuu  CCM ya wilaya ya Moshi mjini 
Mtia nia Edmund Rutaraka pia ametumia maji ya kunywa kutangaza Nia yake hiyo baada ya wajumbe wote walioshiriki mkutano huo kugaiwiwa yakiwa na lebo maalumu yenye maandishi pamoja na picha yake.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.