ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 8, 2015

YANGA OUT KOMBE LA MAPINDUZI


NA SALEH JEMBE
YANGA imeng'oka katika michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kufungwa bao 1-0 na JKU.

Muuaji wa Yanga alikuwa Amour Mohammed ambaye alifunga bao katika dakika ya 72 na kuwapa Yanga wakati mzuri wa kusawazisha bila ya mafanikio.

JKU inayomilikiwa na Jeshi la Zanzibar imefanikiwa kuing'oa Yanga kwa bao hilo moja katika mechi kali na ya kuvutia kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Kutokana na ushindi huo, sasa JKU itacheza nusu fainali dhidi ya Mtibwa Sugar ambayo iliing'oa Azam FC leo mchana.

Yanga ilipoteza nafasi kadhaa za kufunga katika kipindi cha kwanza.

Lakini JKU walionekana kuwa tofauti na kucheza soka la kuvutia tokea mwanzo wa kipindi cha kwanza huku wakichezaji wake wakionana kwa pasi za uhakika zilizoonyesha kuna kitu wanatafuta.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.